7 Jan 2009




MWANGALIE MZAZI HUYU ASIYE NA AIBU KATIKA PICHA HII ILIYOPATIKANA KWA HISANI YA Father Kidevu.AMEJAWA NA TABASAMU WAKATI ANAMPELEKEA BIA MWANAE AMBAYE KWA MAKISIO HAZIDI MIAKA MITANO.TENA BIA YENYEWE NI SAFARI,AMBAYO HATA WANYWAJI SUGU WANAELEWA INAVYOMPELEKESHA MNYWAJI.INGEKUWA KWENYE NCHI ZINAZOJALI HAKI YA MTOTO NA WAJIBU WA WAZAZI,HUYU FISADI WA MALEZI ANGESHACHUKULIWA HATUA.KWANINI AMRITHISHE MWANAE ULEVI BADALA YA VITU VYA MUHIMU ZAIDI KWA FUTURE YA DOGO HUYO?HEBU ANGALIA VIDEO HII HAPO CHINI YENYE HABARI KUHUSU MZAZI ALIYECHUKULIWA HATUA KWA KILICHOELEZWA KUWA NI KOSA LA KUMPA SAPOTI MWANAE APIGANE.
KAMA WENZETU WANAWEZA,WHY NOT US?


1 comment:

  1. Huyu kawekeza kwa mwanae. Lakini tatizo ni kile awekezacho na yule amwekezeaye. Hajiharibii yeye kama anavyoiharibia jamii. Na kwa hakika nyumbani hatuna mamlaka ya jumla kwa jamii toka kwa serikali. Unaona watoto wanavyonyanyaswa, wanavyotumikishwa na sasa wanavyoleweshwa tena mbele ya hadhira bila ya wa kuuliza. Inasikitisha saana.

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.