10 Feb 2009

Pengine mie mshamba.Huenda ndio matokeo ya kutozaliwa Ocean Road hospital i.e. "kuja mjini ukubwani".Au labda huu ndio "ukale",au tuseme "kutokwenda na wakati."Lakini nabaki kuwa mmoja wa watu wanaoiona tarehe 14 ya mwezi Februari,Valentine's Day-Siku ya Wapendanao-kuwa siku ya kawaida kama siku nyingine katika mwaka.Na nisemapo "siku ya kawaida" simaanishi tu kwamba ina masaa 24 kama siku nyingine bali pia napigilia msmari kwenye umuhimu wa siku yenyewe.

Kwangu,na kwa misingi yangu ya Uafrika,kumpenda mwandani wangu ni suala la kila siku.Napojimudu kumnunulia zawadi,basi hilo ni suala la kila wakati pasipo kutegemea mwezi au majira.Kwangu,siku ya wapendanao ni kila siku niliyo kwenye mapenzi ya dhati.

Sina takwimu sahihi kuhusu Siku ya Wapendano huko nyumbani lakini nachokumbuka ni kwamba ilianza kuchukua kasi sambamba na zama za mageuzi katikati ya miaka ya 80 (mid-1980s),mageuzi yaliyopelekea mabadiliko kwenye nyanja za siasa,uchumi,jamii na utamaduni.

Sina ugomvi na wanaoienzi siku hiyo,hususan wale walio kwenye mapenzi ya dhati,lakini nina walakini na wale wanaoigeuza siku hiyo kama fursa ya utapeli wa mapenzi (ntafafanua) na commercialization ya siku yenyewe.Naam,siku hiyo hutumiwa na baadhi ya matapeli wa mapenzi "kuthibitisha" mapenzi yao kwa watapeliwa.Iko hivi:unaye-spend nae Siku ya Wapendanao ndio mpenzi wako wa dhati (unaweza kubisha lakini ndio kanuni zisizo rasmi za siku hiyo huko mtaani).Matapeli wanaweza kuzungukia nyumba ndogo zote na kuishia kulala na aidha mama watoto au nyumba ndogo kuu.Uzoefu unaonyesha kuwa wake/mama watoto ni victims wakuu wa Valentine's Day,ambapo waume kudanganya kuhusu semina za dharura nje ya mji au udhuru wowote utakaomwezesha mume tapeli kulala nje,ni mambo ya kawaida.Ndio maana katika siku hiyo baadhi ya akinamama huwawakia waume zao wanaozuga kuleta rundo la maua na kuwauliza "badala ya kuleta vichanja vya mchicha,wewe unatuletea hiyo mimaua...je tutakula ugali na maua?"Sio kwamba wana hasira na maua,bali umuhimu wake unakuwa umepotezwa na matendo kati ya tarehe 15 ya mwaka uliopita hadi mkesha wa Siku ya Wapendanao.
Takwimu zisizo rasmi (au ziite za kimbeya) zinadai kwamba ni rahisi zaidi kwa kabwela kupata chumba cha kupanga mwaka mzima huko Masaki,Oysterbay,Mikocheni na sehemu nyingine za "kishua" kuliko kupata chumba cha usiku mmoja tu kwenye guest houses katika Valentine's Day (labda booking iwe imefanyika mapema zaidi).





0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.