26 May 2010

Tanzania imeshuhudia vituko vingi mwezi huu wa Mei,kutoka Rais Kikwete kutetea takrima  hadi mtumishi wa Bwana Askofu Kilaini kudai kuwa Kikwete bado ni chaguo la Mungu,kutoka sakata la Masauni kufoji umri (oh Mungu, inawezekanaje?) hadi kifungo cha Liyumba (wengine wanadai alistahili kunyongwa kabisa).Na kutoka kauli ya Waziri Kombani kuwa daraja la mto Kilombero litajengwa katika awamu ya pili ya Kikwete (as if JK ameshashinda uchaguzi) hadi ajali ya gari la msafara wa JK.Makala hii inajaribu kuibua maswali kuhusu hili la mwisho,yaani ajali hiyo.


Kwa mujibu wa vyombo vya habari,uchunguzi mkali unaendelea ku-establish chanzo cha ajali hiyo.Lakini wakati uchunguzi huo ukiendelea tayari kuna wingu limeigubika ajali hiyo huku kukiwa na maswali kama ilitokana na hujuma,au uzembe au ni bahati mbaya tu.

BAHATI MBAYA: Kwa mujibu wa Msemaji Mkuu wa Jeshi la Polisi,ajali hiyo ni bahati mbaya.Gazeti la Tanzania Daima limemnukuu Msika akisema, “Tunaamini ni ajali ya bahati mbaya ambayo ilisababishwa na matatizo ya kiufundi, lakini jambo la kushukuru kiongozi wetu hakupata madhara kwa matukio yote mawili.” Yah,inawezekana ni bahati mbaya.Lakini kichekeksho ni pale Msika kutoa kauli hiyo kabla ya uchunguzi.Majibu rahisi katika maswali magumu?Well,hiyo ndio Bongo yetu.Kauli hiyo ya Msika inaweza kupewa nguvu na kauli nyingine iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu,Salva Rweyemamu,aliyenukuliwa na gazeti hilohilo la Tanzania Daima (toleo la Jumapili) akisema "hitilifu za magari alizokabiliana nazo Rais Kikwete zilikuwa ni za kawaida".Again,tunashuhudia watu walokabidhiwa dhamana muhimu wakikurupuka kutoa majibu mepesi hata kwenye masuala nyeti.Yani kuchomoka tairi ya gari la kiongozi wa nchi ni kitu cha kawaida!Au ni kwa vile ajali kubwa zimezoeleka sana kiasi kwamba hiyo ya msafara wa JK inaonekana 'cha mtoto'?

HUJUMA: Kwa mujibu wa gazeti la Tanzania Daima,kamanda Msika haamini kuwa ajali hiyo ilisababishwa na hujuma.Anasema, "Nasisitiza hatuamini kama kulikuwa na hujuma na ndiyo maana hatutafanya uchunguzi kuhusu matukio yote mawili, lakini kwa suala kama kulikuwa na uzembe wa ukaguzi wa gari, mtafute Salva (Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu), ndiye anaweza kulizungumzia.” Kwa mara nyingine tena tunashuhudia Msika akitoa majibu ya hisia zake (na pengine Jeshi analoongoza) badala ya kusubiri matokeo ya uchunguzi wa kitaalam.Hivi kulikuwa na ugumu gani kwa Msemaji huyo wa jeshi la polisi kutoa jibu lenye mantiki kwamba 'tusubiri matokeo ya uchunguzi badala ya kufanya guesswork'?
Tanzania Daima linakwenda mbali zaidi na kuihusisha ajali hiyo na matukio ya mbalimbali ambapo Rais amekuwa akipewa taarifa potofu (rejea Muswada wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi na taarifa za vikao kati ya TUCTA na Serikali).Kwa mtizamo mpana,gazeti hilo linajaribu kueleza kuwa yayumkinika kuhisi kuwa ajali hiyo ni muendelezo wa 'hujuma' zinazofanywa dhidi ya Rais Kikwete.

Kwa bahati mbaya (au kwa makusudi) Watanzania hawatapata fursa ya kujua ukweli kuhusu tukio hilo.Kwanini nahitimisha hivyo?Well,labda mwenzangu umeshasahau kuhusu ripoti ya chanzo cha milipuko ya mabomu huko Mbagala.Najua kwa wengine,nikitaja Mbagala wanakumbuka zaidi kuhusu mwana-Bongofleva Diamond kuliko ukweli kwamba kuna wenzetu walipoteza maisha yao,tukaambiwa tume imeundwa kuchunguza milipuko hiyo,tukaonyeshwa picha ripoti ikikabidhiwa kwa waziri husika,na hadithi ikaishia hapo.Na kama hufahamu,tume iliyoundwa kuchunguza milipuko hiyo ilitumia fedha za walipa kodi.Sasa sijui wana-tume waliamua kufanya uchunguzi wao baa kisha 'kutokana na kilevi' wkaafikiana kuwa hakuna haja ya kuweka hadharani ripoti hiyo.

UZEMBE: Ni rahisi zaidi kuhisi kuwa ajali hiyo sio bahati mbaya au hujuma bali ni uzembe kwa kuangalia mlolongo wa matukio ya uzembe yanayojiri mara kwa mara.Kwa bahati mbaya,au makusudi,baadhi ya matukio hayo yanamhusisha Rais Kikwete moja kwa moja.Hebu angalia ishu ya Masauni,kwa mfano.Katika kudhibiti songombingo kati ya (Benno) Malisa na Bashe huko UVCCM,JK alionelea ni vema Mwenyekiti wa Umoja huo atoke Zanzibar.Na huyo ndiye Masauni.Kwa hiyo tunapozungumzia 'fojari' ya umri wa Masauni tunapaswa pia kukumbuka nani aliyemuibua.

Lakini tofauti na uzembe uliozoeleka katika shughuli mbalimbali za serikali,huu wa ajali ya gari la Rais hauwezi kuhusishwa na rushwa.Unajua,mara nyingi neno 'uzembe' linatumika kupunguza makali ya neno 'rushwa'.Yaani,utaskia mtu flani 'alifanya uzembe kusaini mkataba flani' lakini ukweli ni kwamba mtu huyo hakuwa mzembe bali alikuwa makini katika kuhakikisha teni pasenti inakwenda kwenye akaunti yake.

Kwanini ajali hii inaweza kuwa matokeo ya uzembe?Kwa wenye ufahamu wa usalama wa kiongozi kama rais,gari analotumia linapewa uangalizi wa hali ya juu kama ilivyo kwa afya,ustawi na usalama wake kwa ujumla.Kuna mlolongo wa watu (wanaolipwa vizuri tu) wanaowajibika kuhakikisha kuwa kila atakachotumia rais kipo katika hali nzuri (na ya juu kabisa).Sitaki kuingia kwa undani sana katika hili kwa sababu zangu binafsi,lakini nachoweza kusema hapa ni kuwa kuna wazembe flani ambao hawakutilia maanani hitilafu zilizojitokeza katika chombo cha usafiri wa rais.

Tatizo linaloweza kuwa limepelekea uzembe huo ni MAZOWEA.Nadhani kuna wanaokumbuka masahibu yalomkumba JK wakati wa kampeni yake huko Mwanza mwaka 2005.Naamini pia kuna wanaokumbuka balaa lilomkumba Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi pale aliponusurika kupigwa akiwa msikitini jijini Dar.Nahisi pia kuna wengi wanaokumbuka habari za msafara wa Kikwete kurushiwa mawe huko Mbeya.Matukio yote hayo yanaweza kuhusishwa na ajali hii ya gari la Rais,na yote yananyooshea kidole uzembe mahala flani.

Nihitimishe makala hii kwa kuusia kwamba matukio kama hilo la ajali ya gari la Rais yataendelea kutokea kama tutaendelea kukabidhiana majukumu kwa minajili ya urafiki (au kishkaji,kama wasemavyo mtaani.Tunapoweka kando professionalism na kuruhusu umimi tutambue kuwa tunajichimbia kaburi letu sie wenyewe.Ujuzi na uzoefu hauwezi kuwa replaced na udini,urafiki au kujuana.

Mwenye macho na asome,mwenye masikio na asikie.

You have been warned!

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.