30 Aug 2010

Nimekutana na habari hii huko Jamii Forums,nami naiwasilisha kama ilivyo:

Dola kuishughulikia CHADEMA
DAWATI LA HATUDANGANYIKI limepokea taarifa za kuaminika kutoka vyanzo vyake kuwa kuwa mara tu baada ya mkutano wa uzinduzi wa kampeni za CHADEMA, siku ya Jumamosi tarehe 28 Agosti 2010 wakuu wa Idara ya intelejensia walikutana na timu ya Kampeni ya CCM kwa ajili ya kutoa mlisho nyuma, na kupanga mikakati ya kuikabili CHADEMA, na yafuatayo yalijiri:-
a)Idara ililazimika kutolea ufafanuzi sababu zilizopelekea shauri wake wa kutaka matangazo ya TBC ya mkutano wa uzinduzi wa Kampeni za CHADEMA kurejeshwa mara moja baada ya kukatizwa. Walieleza kuwa ilitokana na maelfu ya wananchi waliohudhuruia mkutano huo kuwa wa kwanza kugundua kukatishwa kwa matangazo hayo na kuamua wenyewe, bila ya kushawishiwa na kiongozi yeyote kuchukua hatua kali sana dhidi ya TBC. Viongozi wa CHADEMA walistukia tuu mkutano ukitaka kuvurugika kwa wananchi kudai vikali kurejeshwa kwa matangazo hayo. Ilielezwa kuwa kuvurugika kwa mkutano ikwa sababu ya kukatishwa kwa matangazo ya chombo cha umaa kama TBC iimeelezwa kuwa ingekuwa ni aibu kubwa kwa Serikali na TBC.
b)Idara ilitoa taarifa kuwa licha ya umati wa watu waliohudhuria kutofikia ule wa mkutano wa uzinduzi wa CCM, lakini kwa kuwa umati huo kila mtu alijinyanyua kutoka atokako na kuja Jangwani kwa ajili ya CHADEMA tofauti na maandalizi makubwa ya usafiri, fedha, burudani za kila aina, viburudisho n.k yaliyofanywa na CCM kuwafikisha watu kwa maelfu Jangwani. Hizo ni dalili mabaya na ni tishio kubwa kwa CCM. Na ikaamuliwa kuwa iandaliwe mikakati ya kuwakatisha tamma wananchi wenye mapenzi na CHADEMA.
Mkakati :- Ilamuliwa kuwa upandikizwe mgogoro baina ya viongozi wa CHADEMA na mgombea wake Dr W. Slaa; na kuwachonganisha na wapiga debe wao akina Marando, Shibuda, Mpendazoe n.k kwa nia ya kuwakatisha tamaa wenye mapenzi na CHADEMA na wote wanaotarajia kuwapigia kura wagombea wa CHADEMA.
Iliamualiwa kwa kuwa wananchi wanampenda sana Dr W Slaa, zisambazwe habari kuwa aelewani na Mwenyekiti wake Ndg Freeman Mbowe kwa sababu Dr Slaa sio kutoka kabila la wachagga. Ilikubaliwa kuwa taarifa hizo zianze kusambazwa wiki inayoanzia Jumatatu ya tarehe 30 Agosti 2010. Na tathmini ifanyike kujua mafanikio yake wakati zinatungwa mbinu mpya.
Iliamuliwa kuwa magazeti ya New Habari Corporation ikiwemo Mtanzania, Rai n.k yaanze kutumika kwa kazi hiyo wakati waandishi zaidi wa kufanya kzai hiyo wakitafutwa.
Ili wananchi wenye mapenzi mema na CHADEMA waweze kusadiki taarifa zitakazosambazwa ilikubaliwa kuwa magazeti yatakayotumika yaanze kwanza kwa kipindi kifupi kuandika habari njema kuhusu CHADEMA na wagombea wake; na baada ya mashabiki wake kuyaamini magazeti na vyombo hivyo vya habari ndipo kazi ya kuisamabaratisha CHADEMA ianze rasmi.
Ili kutekeleza mipango hiyo waandishi wa gazeti la Mtanzania walipatiwa maelekezo ya kurekebisha kichwa cha habari na maudhui ya habari za uzinduzi wa CHADEMA zilizochapishwa tarehe 29/8/2010, kwa lengo hilo.
Vyombo vya habari vya Serikali ya ikiwemo magazeti ya Daily News na Habari Leo na TBC na redio za TBC vilielekezwa kuanza mara moja kazi ya kuipamba CHADEMA kama chama na watu wa fujo mbele ya jamii makakati amabo unadaiwa kufanikiwa sana kuisambaratisha CUF mwaka 2005, wakati Mkuu wa chombo kimoja cha dola alipodai siku moja kabla ya upigaji kura wamekamata shehena ya majambia yenye rangi za bendera za CUF
c)Pingamzi la CHADEMA dhidi ya Jakaya Kikwete mkutano ulikubaliana kuwa kuaniza sasa idara ihakikishe kuwa inamgeuzia kibao Dr Slaa na kusambaza habari kwa wafanyakazi na umma kuwa DR Slaa anapinga wafanyakazi kuongezwa mishahara ndio maana CHADEMA inamuwekea pingamizi mgombe wa CCM Jakaya Kikwete kwa kitendo cha kuwaongezea mishahara watumishi wa umma katika kipindi hiki cha kampeni.
Dawati litaendelea kuwahabarisha!!!!!!!

If it's true,hivi hii sio local version yetu ya Watergate?

1 comment:

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.