1 Aug 2010

Baada ya kusubiriwa kwa muda mrefu,hatimaye kampuni ya HTC imetangaza rasmi kwamba watumiaji wa simu aina ya HTC DESIRE watapatiwa toleo jipya (version 2.2) la mfumo wa kuendesha simu (operating system -OS- ya Android linalofahamika kama Frozen Yorghut (Mtindi wa Mgando) kwa kifupi Froyo.Kwa mujibu wa taarifa mbalimbali,Froyo itaanza kusambazwa hewani (OTA-over the air) wiki hii kwa wenye HTC Desire ambazo "hazijafungwa" (unlocked) na baadaye kwa "zilizofungwa" (locked) kabla ya kusambazwa kwa simu nyingine zinazotumia OS hiyo ya Android.

Inatarajiwa kuwa Froyo itaziboresha zaidi simu za Android,kwa mfano HTC Desire,ambayo inalinganishwa kwa karibu na "mama wa simu zote",Apple iPhone.Binafsi,nimekuwa nikitumia HTC Desire kwa takriban miezi mitano hivi na kwa hakika ni simu iliyojitosheleza kwa takriban kila kitu.Tatizo pekee hadi sasa,na ambalo limepatiwa ufumbuzi kwenye toleo la Froyo,ni kutoweza kuhifadhi Apps (applications) kwenye memory card hivyo kupelekea simu kuwa na Apps za muhimu tu ilhali kuna maelfu kwa maelfu ya Apps kwenye "soko" la vidude hivyo (Market).

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.