31 Aug 2010





Mwezi Juni mwaka huu tuzo maarufu ya kimataifa iitwayo Ashden Awards iilitolewa kwa wahusika kadhaa duniani zikiwepo nchi za Afrika Mashariki. Tuzo hiyo hutolewa na shirika maalum lililoundwa na duka maarufu la matajiri wa Uingereza yaani Sainsbury Kutoka katika Ashden Trust Charity ambapo mlezi wake akiwa ni Prince Charles. Lengo lake ni kusaidia kurekebisha na kuboresha mazingira duniani . Tuzo ya mwaka huu ilitolewa kwa watafiti na wabunifu waliotengeneza zana za kutengeneza umeme kutokana na nguvu asilia za jua yaaani Solar Energy.
Ingawa wabunifu walitoka mataifa mbalimbali ya Marekani, Asia na Afrika washindi pia walihusisha Kenya, Uganda na Tanzania.
Umeme Jua, Bio gas( Gas Itokayo kwenye kinyesi cha ng'ombe) ni zana ambayo itawasaidia watu maskini hasa wanaotoka nchi kama yetu Bongo vijijini.
Baada Ya Mafanikio makubwa la movie ya £ovely Gamble Urban Pulse wakishirikiana na Msanii/ Mhariri Freddy Macha Wamepewa mzigo mwingine wa kutengeneza documentary ambayo itakuwa hewani tarehe 2 sept 2010 na kurushwa katika tv za hapa ukerewe na mabara mengine ya ulaya.
Hivyo basi utawala wa Urban Pulse Unawaletea trailer ya documentary hiyo hapo juu.

Baada ya uzinduzi tutawapatia kipindi chote
Asanteni sana
Urban Pulse Creative

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.