16 Feb 2011



Pichani ni Mbunge John Komba wa CCM 'akiwa makini' kwa kuuchapa usingizi Bungeni Dodoma.Hata huyu naye anastahili 'zawadi' ya milioni 90?

Hivi kweli inaingia akilini kusikia kwamba Serikali ya Kikwete ina mpango wa kuwapatia wabunge shilingi milioni 90 kila mmoja "kwa sababu inazojua yenyewe?Majuzi tu tumesikia habari kwamba Serikali hiyo hiyo inatembeza bakuli kwa wahisani ili wasaidie 'kuokoa jahazi' la hali mbaya ya Bajeti ya 2010/11.

Lakini pia tunakumbuka Kikwete alivyokuwa mkali kwa watumishi wa umma walipotishia kugoma kushinikiza kulipwa mishahara inayoendana na hali halisi ya maisha.Sasa kama ilishindikana kuwalipa wafanyakazi wa umma mishahara bora haya mabilioni ya kuwazawadia wabunge yanatoka wapi?

Naona kuna kila jitiahada za watawala wetu kukaribisha yanayojiri huko Arabia na Mashariki ya Kati.Japo inauma kuona mabilioni ya shilingi yakizawadiwa kwa waheshimiwa kama huyo anayechapa usingizi,lakini hatua hiyo inaweza kuwa blessing in disguise kwa maana kwamba huenda ikawahamasisha Watanzania kuiga mifano ya 'walalawima' wenzao wa Tunisia na Misri,na hatimaye kufanikiwa kuleta 'Uhuru wa Pili' (wa kwanza ulikuwa wa kumwondoa mkoloni.Wa pili ni wa kuwaondoa mafisadi)

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.