12 Apr 2011



Hatimaye habari za "tiba ya miujiza ya Babu wa Loliondo" zimefunikwa kidogo,at least kwa muda,baada ya chama tawala CCM kufanya mabadiliko yanayoitwa makubwa katika safu za uongozi wake.Katika mabadiliko hayo,kamati kuu ya chama hicho ililazimika kujiuzulu na kufuatiwa na uteuzi wa wajumbe wapya.

Tukio hilo linaonekana kuwagusa Watanzania wengi na tayari baadhi yao wameanza kumpongeza Mwenyekiti wa chama hicho,Rais Jakaya Kikwete,kwa kile kinachotajwa kama "maamuzi magumu na mazito".

Hebu nikuulize msomaji mpendwa.Hivi ukiamua kuanzisha urafiki na jambazi unategemea hatima yake itakuwa nini?Na pindi ukitambua kuwa urafiki huo unakupeleka kubaya,na hatimaye kuamua kuachana na jambazi huyo,unastahili sifa gani?

Mfano huo unamhusu Kikwete na CCM kwa ujumla.Wakati baadhi yetu wanapiga vigeregere vya pongezi kutokana na "ujasiri wa Kikwete" kinachopuuzwa ni ukweli kuwa ni Kikwete huyuhuyo aliyewawezesha watu kama Edward Liowassa na Rostam Aziz kufikia hapo walipo sasa.

Baada ya Mwalimu Julius Nyerere "kumzuia" kuongoza Tanzania mwaka 1995,Kikwete alijenga uswahiba na Lowassa na Rostam kwa minajili ya kuchukua urais mwaka 2005 baada ya Rais Benjamin Mkapa kumaliza miaka yake 10.Mbinu chafu zilizotumiwa na wanasiasa hao watatu zinafahamika kwa takriban kila mmoja wetu.Utatu huo usio mtakatifu uliounda genge hatari linalojulikana kama "Wanamtandao".Genge hilo lilifanya kila mbinu kuhakikisha kuwa lazima Kikwete anakamata urais mwaka 2005.Na hatimaye walifanikiwa baada ya kujipenyeza katika kila nyanja ya jamii ya Tanzania.

Baada ya kuukwaa urais,Kikwete aliwaruhusu washirika wake kufanya mambo wapendavyo kana kwamba Tanzania ni kampuni ya mtu binafsi.Sijui ni kujisahau au kuvimbiwa,haikuchukua muda kwa maswahiba hao wa Kikwete kuanza kufanya mambo "ndivyo sivyo".Kufupisha stori,skandali kama za Richmond,EPA,nk kwa kiwango kikubwa ni matokeo ya moja kwa moja ya harakati za wanasiasa hawa.

Sasa,kilichotokea Dodoma na kupachikwa jina "kujivua magamba" ni sawa kabisa na mfano niliotoa hapo awali wa mtu kujenga urafiki na jambazi.Baada ya Kikwete kumaizi kuwa asipokuwa makini anaweza kujikuta akifiwa na CCM mikononi mwake,amelazimika kujitenga na maswahiba waliomsaidia kuukwaa urais.

Kwanini basi naamini kuwa Kikwete hastahili pongezi zozote kutokana na uamuzi wa kuwatosa maswahiba zake?Kwanza,hata huko "kuwatosa" kwenyewe kumefanyika katika mazingira ya uoga.Inaelezwa kuwa matakwa ya waliohitaji mageuzi ndani ya chama hicho yalikuwa kuwatimua kabisa Lowassa,Rostam na Chenge.Lakini kinyume chake,Kikwete akaamua kuvunja kamati kuu nzima.Usisahau msemo wa Kiswahili kuwa kilio cha wengi ni harusi.

Je ni kweli kwamba kamati kuu nzima ilikuwa na mapungufu ya kulazimisha kuivunja yote?Je kamati kuu nzima ilikuwa ya kifisadi kwa vile tu miongoni mwao kulikuwa na watuhumiwa wa ufisadi?

Ukweli unabaki kwamba Kikwete hakuweza kuwa na jeuri ya kuwatosa Lowassa,Rostam na Chenge kama mtu mmoja mmoja na badala yake akaamua kuchukua kile wanachoita Waingereza "blanket decision" ambapo waliomo na wasiomo wakajikuta wanabwagwa.

Tukiweka hilo kando,kuna hoja ya pili ambayo ni nafasi ya waliotoswa kuendeleza kile kile kilichopelekea kuondolewa kwenye kamati kuu in the first place.Lowassa,Rostam na Chenge wanaendelea kubaki wabunge wa CCM,huku Lowasssa akiendelea pia kuongoza kamati influential ya Ulinzi na Usalama.Je kwa nafasi walizobaki nazo wanasiasa hao hawawezi kujitutumua kuendeleza harakati zao?Muda utatueleza.

Lakini pia tunapaswa kumwangalia Kikwete sio tu kama Mwenyekiti wa CCM bali pia Rais wa nchi.Kama tukiamini kuwa ujasiri wake ndio uliopelekea maamuzi hayo "magumu" ndani ya chama chake,kwanini basi huko serikalini inamwia vigumu kuondoa rundo la uozo linalohatarisha future ya nchi yetu?

Na ieleweke kwamba wakati chama kinaendeshwa kisiasa zaidi,serikali inaendeshwa kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizopo,au zinazoweza kutengenezwa kwa makusudi maalum.

Kikwete huyuhuyu ndiye aliyetamka mara baada ya kupata urais mwaka 2005 kuwa anawafahamu wala rushwa kwa majina,na kwamba anawapa muda wa kujirekebisha.Sote tunafahamu kuwa wala rushwa sio tu hawajajirekebisha bali pia wamepuuza indefinite deadline hiyo ya Kikwete.

Sijui ni usahaulifu au hatupo makini,baadhi ya wenzetu wameshasahau kuwa katika kampeni za uchaguzi mkuu uliopita hivi majuzi tu Kikwete huyuhuyu alisimama majukwaani kuwapigia debe Lowassa,Rostam na Chenge huku akiwamwagia sifa lukuki.

Kama haitoshi,Kikwete alimudu kuwatetea "live" alipoongea na waandishi wa habari huku akisisitiza kuwa wanasiasa hao hawajatiwa hatiani na kinachodaiwa dhidi yao ni tuhuma tu.Sasa kama huo ndio ukweli,how come basi safari hii kawatosa ilhali hawajawahi kutiwa hatiani?

Na watatiwaje hatiani katika mazingira ya sasa ambapo sheria zipo tu kwa ajili ya kuwabana wamachinga,wezi wa kuku,walalahoi wanaoshindwa kumudu kulipa kodi kutokana na umasikini wao na Watanzania wengine wa kawaida,ilhali vigogo wakiachwa wafanye wapendavyo?

Hivi kweli tumesahau mzaha wa hukumu dhidi ya Chenge katika kesi yake ya kuua watu wawili kwa kuwagonga na gari ambalo bima yake ilikuwa imesha-expire?Kuna Watanzania wangapi wanaosota jela sio kwa vile wameshatiwa hatiani bali hawana uwezo wa kuwahonga waendesha mashtaka na mahakimu?

Don't get me wrong kuwa labda namchukia Kikwete.Hapana.Sina tatizo naye kama Jakaya Kikwete bali tatizo langu lipo kwenye udhaifu wa uongozi wake kama Rais Jakaya Kikwete.

Tusiwe wepesi wa kuamini kila jambo linapotokea hata kabla ya kupima ufanisi wake.Kadhalika,tusiwe wepesi wa kupuuza historia,kwa mfano kusahau kuwa Kikwete huyu huyu alituahidi maisha bora kwa kila Mtanzania na matokeo yake imeishia kuwa maisha bora kwa kila fisadi.

Unaweza kunihoji kwanini nawasihi kuwa na subira kabla ya kukimbilia kupiga vigeregere vya furaha na pongezi kwa maamuzi ya "kijasiri" ya Kikwete,lakini wakati huohuo mie pia nakimbilia kumwaga lawama na kusambaza "sumu ya kutotarajia mema" badala ya kusubiri matokeo.

Jibu langu ni jepesi.Historia inamhukumu Kikwete.Amekuwa mahiri zaidi wa kutoa ahadi lakini mwepesi sana wa kusahau ahadi zake.Historia pia inatukumbusha kuwa hata Lowassa alipojiuzulu kwa kuhusika kwake kwenye skandali ya Richmond Kikwete alimpongeza na kudai kilichomkumba swahiba wake huyo ni ajali tu ya kisiasa.Na Waziri Mkuu Mizengo Pinda akapigilia msumari kwa kudai kuwa sikum moja Lowassa anaweza kurejea kwenye uongozi serikalini.Kwanini basi sasa tuamini kuwa kutoswa kwa wanasiasa hao ndio mwisho wa yote wanayolifanyia taifa hili?

Mwisho,nadhani tumezowea mno kuona madudu kiasi kwamba hata kiongozi anapotimiza wajibu wake tunalazimika kumpongeza.Kwanini hatujipongezi kwa kunawa uso au kupiga mswaki kila tunapoamka?Yah,hatujipongezi kwa vile vitendo hivyo ni wajibu wetu wa kila siku.

Kwanini hatujipongezi kwa kwenda makazini au mashuleni?Alichofanya Kikwete sio ujasiri bali kimsingi ni wajibu wake kama kiongozi.Na kwa hakika hakipaswi kuishia huko CCM pekee,chama chenye wanachama pungufu ya watu milioni tano wakati nchi yetu ina watu takriban milioni 50,bali kama yupo serious kweli na anajua kwanini yupo Ikulu,basi ni lazima aanze kusafisha uozo uliopo kila kona.

Kuna tofauti kubwa kati ya jambo jema linalostahili pongezi na utekelezaji wa wajibu.Alichofanya Kikwete ni the latter:ametekeleza wajibu wake kama kiongozi.Jambo jema linaloweza kutufanya tummwagie rundo la pongezi ni pindi atakapoamka usingizini na kutambua nchi inateketea kwa ufisadi huku virusi vya udini vikizidi kuzagaa katika jamii yetu kutokana na jitihada za matapeli wa kisiasa wanaowatumia wazembe wanapoouza vipaumbele vyao (kwa mfano wanaopotosha kuwa upinzani dhidi ya mchakato wa mabadiliko ya katiba unatokana na chuki ya Wakristo kwa Muislam Kikwete.This is way too low,na tusipokuwa makini tutaanza kutetea vibaka,majambazi,makahaba,mafuska,wabakaji,nk kwa vile tu wanatoka dhehebu flani).

1 comment:

  1. HIV KKWT,UMEFANY NN AMBACHO HT WW UKITOKA MADRKN TUKUKUMBK,MWNZK MKP ALIJENG MASHULE,UWANJA NA HATA DOLA IT WAS ALMST =1000.SS WW..HUON HT AIB

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.