28 Apr 2011



Kujali "vipaji" vyetu,kutojua vipaumbele vyetu au ufisadi wa kiakili?

Tukiamini takwimu kutoka huko Loliondo kuwa wastani wa wagonjwa wanaofika sehemu hiyo matibabu ni 2000 kwa siku,kwa wiki ni watu 14,000,kwa mwezi ni (wastani) 42000-au tukuze makadirio na kufanya watu 50,000 kwa mwezi,na tunaambiwa "Babu" alianza matibabu kitambo kidogo kabla habari hazijashika moto kwenye mwezi Februari,basi kuna uwezekano takriban watu milioni moja wameshapatiwa tiba na mtumishi huyo wa Mungu. (habari zinasema alianza matibabu tangu mwaka 2009,lakini kwa minajili ya kuamsha tafakuri tufanye alianza mwezi Januari mwaka jana.


Swali moja gumu ambalo nashindwa kabisa kupata jibu lake ni USHUHUDA KUTOKA KWA WALIOPONA.Hivi kweli kati ya watu milioni moja,au kwa kumtendea haki tuseme watu nusu milioni,hakuna hata 100 kati yao wanaoweza kutangaza hadharani kuwa walikuwa na ukimwi kisha wakapona baada ya kupewa kikombe?Vyombo vyetu vya habari vimekuwa bize zaidi kuripoti matukio badala ya kuchunguza ufanisi wa tiba hiyo ya kikombe.


Anyway,hebu soma habari ifuatayo kuhusu namna "Babu" anavyotukuzwa kama VIP flani.Msafara kwenda kwenye msiba wa mwanae ukiongozwa na polisi na maafisa usalama,stahili zinazotolewa kwa viongozi wa juu wa kitaifa kama vile Rais,Makamu wa Rais na Waziri Mkuu.




Babu aenda msibani chini ya ulinzi

MCHUNGAJI Ambilikile Mwasapila anayetoa tiba ya magonjwa sugu huko Samunge Loliondo, juzi jioni aliondoka hapa kwenda Babati, Manyara kuhudhuria mazishi ya mtoto wake huku safari yake hiyo ikiratibiwa na Serikali na akipewa ulinzi mkali wa maofisa usalama na polisi.

Aliondoka Samunge saa 12:20 jioni na gari la Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro akiwa na maofisa hao wa usalama, polisi na wasaidizi wake.Kabla ya kuondoka Samunge, watu mbalimbali walikuwa wamejitolea kumpatia usafiri mchungaji huyo lakini walizuiwa kutokana na sababu za kiusalama.

"Tulikaa kama kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya, tukaona ni busara tuchukue jukumu la kumsafirisha Mchungaji hasa kutokana na sababu za kiusalama," alisema ofisa mmoja mwandamizi wa serikali wilayani hapa.Alisema mchungaji huyo atalindwa akiwa msibani na atakaporejea Samunge.

CHANZO: Mwananchi

TAFAKARI

1 comment:

  1. Watanzania hatuna dogo, sasa huyu babu anahitaji eskoti ya nini!

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.