26 Apr 2011


Wait a minute!Hivi jina "Mzee wa Kijiko" si lilikuwa la mwanamuziki wa dansi Ally Choki

Well,mazingaombwe ya kuibuka kwa watu wanaodai kupewa nguvu na Mungu kuponyesha magonjwa sugu yanaendelea baada ya mkazi mmoaj kuibuka na kudai anatibu kwa kijiko.Hebu soma mwenyewe habari kamili hapa chini

Fatuma Maumba, Mtwara

BAADA ya Mchungaji mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Masapila kuanza kutoa dawa ya kikombe katika Kijiji cha Samunge, kilichopo Loliondo Mkoa wa Arusha, mkoani Mtwara ameibuka mtu mmoja anayetibu kwa kutoa dawa ya kijiko.

Kutokana na kuwapo kwa mtu huyo, Ahmad Linangwa maarufu kama Mzee wa Kijiko, wananchi wengi wamekuwa wakifurika katika Kijiji cha Moma Wilaya ya Mtwara Vijijini, Mkoa wa Mtwara kwa ajili ya kupata dawa ya kijiko.

Akizungumza na MTANZANIA nyumbani kwake kijijini hapo juzi, Linangwa alisema kabla ya kuanza kutoa dawa hiyo inayotibu magonjwa sugu ukiwamo ukimwi, awali aliota na kupewa maelekezo na Mwenyezi Mungu namna ya kuchanganya miti ya aina tatu kwa ajili ya kupata dawa hiyo.

“Pamoja na kupewa maelekezo hayo Aprili 18 mwaka huu, pia niliambiwa baada ya kuchanganya miti hiyo, nivilige kitu kama goroli kisha nichanganye na maji pori ambayo nitayagema kwenye mti unaoitwa Mtamba.

“Nikishafanya hivyo, maji hayo niwape wagonjwa nao watapona magonjwa yanayowasumbua,” alisema Linangwa.

Kwa mujibu wa Lingangwa, kabla ya kuanza kuwapa wagonjwa dawa hiyo, alianza kuinywa yeye wakati alipokuwa porini akiiandaa.

“Nilianza kuinywa nikiwa kule porini, nilipomaliza kuinywa, nilikimbilia nyumbani haraka ili kama ni sumu iniue wakati nimeshafika nyumbani lakini sikufa.

“Kwa hiyo watu waje watumie dawa hii, haina masharti yoyote kwani kama mtu anatumia dawa za hospitali anaweza kuendelea na dawa hizo bila wasiwasi, kama unakunywa pombe, au unavuta sigara, dawa yangu haina matatizo,” alisema Mzee wa Kijiko.

Kutokana na kuwapo kwa matibabu hayo, nauli kwa pikipiki na bajaji zimepanda kutoka Mtwara Mjini hadi kijijini Moma.

CHANZO: New Habari

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.