2 Apr 2011


Baadhi ya magazeti ya Tanzania yanaelekea kutothamini kabisa uwepo wake mtandaoni.Hivi inaingia akilini kweli kwa msomaji kutembelea tovuti ya gazeti na kukutana na "habari mpya" za Februari 3,2011?Hiyo ndio hali niliyokutana nayo kwenye tovuti ya gazeti la Tanzania Daima.

Awali,gazeti hili lilikuwa makini sana katika kuweka habari mpya kwenye tovuti yake lakini sijui "kirusi" gani kimewakumba.Tovuti yao imeendelea kuwakaribisha wasomaji na ujumbe kuwa ipo "off-line kwa matengenezo".Matengenezo gani hayo ya zaidi ya mwezi mzima?

Tatizo la msingi kwa magazeti yetu mengi ni dhana potofu kuwa toleo la mtandaoni ni kama fadhila kwa wasomaji.Pengine dhana hiyo inajengwa na ukweli kwamba matoleo ya mtandaoni husomwa bure,na hivyo kuwafanya wahusika kujiona kama "wanafanya kazi ya Kanisa" (yaani isiyo na ujira).

Sasa,kama wanataka habari zao zisomwe mtandaoni kwa malipo wanaweza kuanzisha huduma ya kulipia (paywall).Lakini kama wameamua kwa hiari yao kuanzisha tovuti na kuweka habari zisomwe bure basi wanapaswa kuwajibika kwa kutuwekea habari mpya kama inavyostahili.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.