22 Aug 2011


Imetumwa na mdau Kato Lukaija

Wapo watu wanoamini kwamba pakipatikana suluhisho la matatizo ya biashara na uchumi kati ya bara na Zanzibar, basi kero za muungano zitakua zimekwisha. Hawa wanafanana na viongozi wetu wanaoamini kwamba muungano wa kiuchumi wa Afrika mashariki ni atua itakayotosheleza kuleta muungano wa kisiasa na kiutamaduni .Kwa mtazamo huu, uchumi ndio msingi wa kila jambo, liwe la kitamaduni,kisiasa au kitaifa. Na ndio maana nguvu zinaelekezwa zaidi kwenye diplomasia ya uchumi.

Lakini Muungano wetu,pamoja na kuunganisha uchumi wetu kwa matumizi ya sarafu moja,bado umegubikwa na hali ya kutosikilizana.Hali imekua hivyo kwa muda mrefu. Kwa hiyo kero zake,kama mijadala mingi inavyoonesha,haisababishwi na matatizo ya uchumi peke yake. Kuna tatizo la utata wa historia yenyewe ya muungano.

Kuna historia mbili za Muungano. Watu wa bara wanaona Muungano ni matokeo ya Mapinduzi ya Zanzibar yalioundoa utawala wa kitumwa wa Waarabu. Lakini nje ya madarasa rasmi ya historia hiyo,wapo vijana wanaharakati wa Zanzibar, kama Harith Ghasany,mwandishi wa KWAHERI UKOLONI,KWA HERI UHURU. Wanaharakati hawa wanadai kwamba Mapinduzi ya Zanzibar ni tunda la usuda ya Nyerere na kanisa dhidi ya waislamu na waarabu wa Zanzibar.Hivyo Muungano unaonekana kama ukoloni.

Hali hii inahitaji Wazee wakae na kukubaliana kuandika historia moja.  Wafanye kama Rais Kagame. Pamoja na kuangaikia uchumi,Kagame amehakikisha kwamba historia ya kweli ya mauaji ya 1994 ndio inayofundishwa na watu wote.Kagame anajua kwamba mtu haishi kwa mkate tu,ila kwa kila neno litokalo kwa bwana. Kwa hiyo vijana tunaomba wazee waandike historia moja tu. Wazee  wakisimamia historia moja tu, Muungano wetu utapona.

                             ------Kato Lukaija,  P.O.BOX 10351, DAR ES SALAAM.
                                         

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.