19 Jan 2013



THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIADIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone:


255-22-2114512,2116898

E-mail:
[email protected]

[email protected] Fax: 255-22-2113425
PRESIDENT’S OFFICE,THE STATE HOUSE,P.O. BOX 9120,DAR ES SALAAM
.
Tanzania
.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
RAIS wa Jamhuriya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa JakayaMrisho Kikwete anaanza ziara rasmi ya Kiserikali nchini Ufaransa leo, Jumamosi, Januari 19, 2013, kwa mwaliko wa Rais wa Ufaransa,Mheshimiwa Francois Hollande.Rais Kikwete na ujumbe wake aliondoka nchini usiku wa kuamkialeo, Jumamosi, kwa ndege ya Shirika la Ndege la Uswisi kuelekea Ulayakwa ajili ya ziara hiyo.Mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja waNdege wa Charles DeGaul mjini Paris leo jioni, Rais Kikwete ambaye anafuatana na MamaSalma Kikwete atapokelewa rasmi katika Ufaransa kwa gwaride nakupokelewa na Waziri wa Misaada ya Maendeleo wa Ufaransa,Mheshimiwa Paschal Canfin.Kwa mujibu wa ratiba, kesho, Rais Kikwete atakutana na kufanyamazungumzo na Mama Frannie Leautiera mbaye ni Mtendaji Mkuu waMfuko Private Fund na baadaye atakutana na Mama Marie ChristineSaragosse, Mtendaji Mkuu wa
Redio France International (RFI).
Mkutano huo utafuatiwa na kikao kati ya Rais Kikwete na Jumuiya yaWatanzania wanaoishi nchini Ufaransa.Keshokutwa, Jumatatu, Rais Kikwete atakutana na kufanyamazungumzo na Mheshimiwa Francois Hollande, Rais wa Ufaransakwenye Kasri ya nchi hiyo ya Elysee Palace.Mazungumzo kati ya Rais Kikwete na Rais Hollande yatafuatiwana chakula cha mchana ambako Rais Kikwete atakaribishwa naWaziriwa Mambo ya Nje wa Ufaransa, Mheshimiwa Laurent Fabius. Baada yachakula hicho cha mchana, Rais Kikwete atakutana na kuzungumza na

Bwana Yves Louis Darricarere, Rais wa Kampuni ya Mafuta yaKimataifa ya Total.Mazungumzo hayo yatafuatiwa na mazungumzo mengine kati yaRais Kikwete na Kiongozi wa Madhehebu ya Ismailia Duniani H.H TheAga Khan na baada ya hapo, Rais Kikwete atakwenda Kasri laLuxemburg kukutana na kuzungumza na Rais wa Bunge la Seneti laUfaransa, Mheshimiwa Jean Pierre Bel.Usiku wa Jumatatu, RaisKikwete atakula chakula cha usiku naRais wa zamani wa Ufaransa, Mheshimiwa Valery Giscard d’Estaingambaye ni Mwenyekiti wa
Tanzania Wildlife Conservation Foundation
. Jumanne, Rais Kikwete atakuwa na siku nyingine yenye shughulinyingi ambako miongoni mwa mambo mengine atakutana na kufanyamazungumzo na mabalozi wa Afrika wanaowakilisha nchi zaokatikaUfaransa, na atakutana na Mheshimiwa Abdou Diouf, KatibuMkuu wa Umoja wa Kimataifa wa Nchi Zinazongumza Lugha yaKifaransa na Rais wa zamani wa Senegal.Rais Kikwete pia atashiriki majadiliano kuhusu masuala yakimataifa yaliyoandaliwa na Taasisi ya Mahusiano ya Kimataifa yaUfaransa – Institute Francais Des Relations International (IFRI) naatakutana na kuzungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika laMaendeleo ya Kimataifa la Ufaransa (AFD).Rais Kikwete ataondoka nchini Ufaransa Jumatano, Januari 23,2013, kwenda Uswisi ambako atatembelea Makao Makuu ya Shirikishola Soka Duniani (FIFA) mjini Zurich na baadaye kwenda Davoskuhudhuria mkutano wa mwaka huu wa Shirika la Uchumi Duniani –
World Economic Forum (WEF).
Imetolewa na
:Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu
.Dar es Salaam.19 Januari, 2013
Kuna mambo mawili  ya msingi yanayohusiana na taarifa hii:

 KWANZA, Ziara hii ya Rais Kikwete huko Ufaransa inazidi kuthibitisha kuwa Rais ameamua kuziba masikio kwa kelele kuwa ANASAFIRI MNO.Na kelele hizo si za chuki wala hazimaanishi 'Rais aote matende kwa kwa kutotoka nje ya Ikulu.' Ukweli ni kwamba safari hizi za mfululizoni mzigo mkubwa kwa nchi yetu ambayo inakabiliwa na jumla ya wastani ya deni la nje na ndani la takriban shilingi 40,000,000,000,000 (TRILIONI 40)! 

 PILI, ni fedheha kwa Rais Kikwete kupokelewa na Waziri wa Misaada ya Maendeleo wa Ufaransa.Hii inaonyesha kuwa ziara hiyo si muhimu kwa nchi hiyo,japo Rais Kikwete baadaye atakutana na Rais Hollande wa Ufaransa.Mkuu wa nchi anapozuru nchi nyingine shurti apokelewe na mwenyeji wake,yaani mkuu mwenzie wa nchi.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.