14 Jun 2014

Tunaomba radhi kwa picha hizi ambazo ni graphic. Tumejitahidi kuficha sura ya marehemu
Mwili wa mtu aliyeuawa kutokana na shambulio hilo la bomu

Mtu mmoja ameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika shambulio la bomu karibu na msikiti huko Zanzibar. Kwa mujibu wa polisi, shambulio hilo lilitokea katika eneo la Stone Town kwenye sehemu ya biashara ya Darajani.

Mashuhuda wa tukio hilo walieleza kwamba miongoni mwa majeruhi ni waumini waliokuwa wanatoka kuswali katika msikiti ulio jirani na eneo hilo.

"Tunafanya uchunguzi kutambua aina ya bomu, waliohusika na shambulio hilo na lengo lao. Tunaomba wananchi kutupatia taarifa," alisema afisa mwandamizi wa jeshi la Polisi, Mkadam Khamisi.

Taarifa zaidi kuhusu tukio hili la kusikitisha zitawajia kadri zinavyopatikana

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.