23 Jul 2014

Mtandao wa kijamii wa Twitter unazidisha ushindani miongoni mwa apps za ku-chat, hususan Whatsapp, kwa kuboresha huduma yake ya ujumbe wa moja kwa moja (Direct Message) au DM kama inavyojulikaza.

DM ni tweets zinazotumwa faragha kati ya watu wawili 'wanaofuatana' (follow each other), au kwa ujumbe wa moja kwa moja kwa watu maarufu wenye akaunti zilizohakikiwa (verified) ambazo zinawawezesha kupokea ujumbe wa aina hiyo hata kwa watu wasiowa-follow.

"Katika wiki chache zijazo, tutatambulisha update itakayorahisisha kufuta DM kiurahisi mtandaoni na katika simu au tablet," wameeleza Twitter,na kuongeza, "pia tutatambulisha update kwa iPhone na Android itakayomwezesha mtumiaji kuona historia nzima ya DMs.

DM zinawakwaza watumaiji kutokana na limit ya tarakimu 140 na mapungufu katika ku-sync kati ya mtandao na simu au tablet.

Mafanikio ya Whatsapp yalijidhihirisha mwezi Februari mwaka huu baada ya app hiyo kununuliwa na Facebook kwa dola bilioni 19, na sasa app hiyo inatumiwa na watu zaidi ya milioni 500.


ENDELEA KUTEMBELEA BLOGU HII KUFUATILIA MAENDELEO YA HABARI HII NA NYINGINEZO KWA KUBONYEZA KIPENGELE CHA 'TEKNOLOJIA' HAPO JUU

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.