
Wanasayansi wanataraji kwamba ndani ya miaka 30 ijayo, itawezekana kutengeneza na kutunza ujauzito nje ya tumbo la mama. Teknolojia hiyo inayofahamika kama ectogenesis imekuwa ikifanyiwa kazi katika maabara tangu mwaka 200, na majaribio ya awali yalikuwa ya kutengeneza na kutunza mimba ya panya nje ya tumbo la panya ' wa kike.'
Wakati wanaounga mkono teknolojia hiyo wanadai itapunguza vifo vya watoto wakiwa tumboni kwani itarahisisha kufanya uangalizi na ufuatiliaji, wapinzani wake wanadai kuwa itaingilia utaratibu wa asili wa uzazi. Wengine wanadai kuwa hatua hiyo itaondoa hatua muhimu ya mahusiano kati ya mama na mtoto tangu akiwa tumboni.
Ectogenesis ni makuzi ya kiumbe kichanga (organism) nje ya mwili, na inatokea kwa baadhi ya wanyama na bakteria. Katika kutengeneza na kutunza mtoto nje ya tumbo la mimba, mfuko 'feki' wa uzazi wahitaji 'mrija feki wa uzazi ' (fake uterus) ili kukipatia kiumbe lishe na hewa ya oksijeni. Pia mipira maalum itahitajika ili kuwezesha kiumbe kichanga 'kujisaidia' (kutoa uchafu mwilini). Chupa inayohifadhi 'mimb' itaunganishwa na mitambo itakayofuatilia makuzi ya 'kichanga' na mimba kwa ujumla.
Kwa taarifa kamili BONYEZA HAPA
CHANZO: Daily Mail
0 comments:
Post a Comment