15 Aug 2014

Hebu pata picha: unaingia kwenye email yako unakutana na ujumbe kwamba usubiri kwa muda kwa vile 'internet imejaa.' Kama lengo lilikuwa kusoma tu emails zako, yaweza kuwa sio big deal. Lakini kama uliingia kwenye e-mail ili utume CV kwa mwajiri, au utume assignment yako kwa mwalimu/mhadhiri, basi kwa hakika hali hiyo itakuwa na athari kwako.

Taarifa zinaonyesha kwamba kupotea hewani kwa mitandao kunaweza kuwa jambo la kawaida huko mbeleni kufuatia Internet kuanza kuishiwa nafasi.Jumanne wiki hii, makampuni mbalimbali yaliingia hasara kubwa kufuatia kupotea mawasiliano ya internet kutokana na ufinyu wa nafasi.

Mtandao maaarufu wa kuuza na kununua bidhaa, eBay, ulikuwa miongoni mwa wahanga wa tukio hilo la Jumanne, ambapo ulipotea hewani kwa takriban siku nzima na kukwamisha shughuli lukuki zinazofanyika katika mtandao huo wa biashara.

Maelfu kwa maelfu ya wateja walishindwa kuingia kwenye akaunti zao za eBay huku malalamiko mengi yakiwasilishwa na wateja kutaka warerejeshewe fedha walizonunulia bidhaa.

Inaelezwa kuwa chanzo cha tatizo hilo kilikuwa kinachofahamika kama Border Gateway Protocal (BGP). Makampuni yanayotumia internet na mitandao mignine mikubwa hutumia 'barabara' (route map) hiyo yenye mamia kwa maelfu ya 'njia' kupelekeana taarifa kupitia mtandaoni. Video ifuatayo yaelezea kwa undani zaidi:



Katika mazingira ya kawaida, mtu anapotembelea tovuti anategemea mashine zioitwazo 'router' kukumbuka njia salama katika mtandao mpana wa Internet. Hata hivyo 'routers' za zamani zinapata wakati mgumu kumudu teknolojia mpya- kwa mfano simu za kisasa (smartphones) na Tablets ambazo sio tu zina watumiaji wengi bali pia huongeza muda ambao mtumiaji huwa mtandaoni. Hali hiyo imepelekea 'foleni' kubwa mtandaoni na kusabababisha baadhi ya routers kukabiliwa na changamoto ya kumbukumbu (memory) na uwezo wa kuzifanyia kazi data.

Mfano sahihi wa kilichotokea ni pale ubongo wa binadamu unapozidiwa na uwezo wa kukumbuka vitu njiani baada ya safari ndefu.

Ili kukabiliana na tatizo hilo, routers zinabidi kuboreshwa zaidi katika uwezo wa kumbukumbu na kufanyia kazi data.

Wataalamu wanadai kwamba tatizo hilo litazidi kujitokeza huko mbeleni hasa kwa kuzingatia kuongezeka kwa mauzo ya simu za kisasa na Tablets.

CHANZO: Imetafsiriwa kutoka gazeti la Daily Mail la hapa Uingereza

Endelea kupata habari za teknolojia kwa kutembelea blogu hii, na kwa urahisi zaidi, bonyeza hapo juu kwenye menu palipoandikwa TEKNOLOJIA


0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.