3 Sept 2014


Mnyanyasaji wa mtandaoni, Peter Nunn (pichani) anakabiliwa na uwezekano wa kifungo jela baada ya mahakama kumkuta na hatia ya kumtumia mbunge Stella Creasy  wa jimbo la Walthamstow kwa tiketi ya Chama cha Labour, hapa Uingereza, tweets za kutishia kumbaka.

Mnyanyasaji huyo alitumia mtandao wa kijamii wa Twitter kumwandama mbunge huyo aliyemwita mchawi katika tweets zake.

Nunn alijitetea kwamba hakuzungumzia suala la kumbaka mbunge huyo bali ujumbe  wake ulikuwa utani tu.

Kadhalika alikanusha kuendesha kampeni ya chuki dhidi ya mwanasiasa huyo wa kike, ambaye alikuwa akimsapoti mwanaharakati wa masuala ya wanawake  (feminist), Caroline Criado-Perez, katika kampeni ya  kudai noti ya Paundi 10 ya Uingereza iwe na picha ya mwanamke mwingine zaidi ya Malkia Elizabeth wa Pili ilivyo sasa.

Mnyanyasaji huyo ambaye ni dereva kutoka mji wa Bristol jana alipatikana na hatia ya kutuma ujumbe wa kudhalilisha na kutisha kwa kutumia mtandao wa wazi wa kielektroniki kati ya Juni 28 na Agosti 5 mwaka jana.

Jaji wa mahakama ya wilaya Elizabeth Roscoe alisema, "yeye (Nunn) anasema hadhani mbunge huyo na mwenzie walikwazwa na ujumbe wake. Hapana, siwezi kuamini maelezo hayo hata kidogo."

"Nina uhakika timilifu kabisa kuwa tweets zake zilikuwa na malengo mabaya."

Nunn alionekana kutahayari wakati hukumu hiyo dhidi yake inasomwa.katika mahakama ya City of London.

Baada ya hukumu hiyo, mbunge huyo ambaye hakuwepo mahakamani ali-tweet "sasa kesi ya mnyanyasaji Twitter imekwisha, ujumbe upo wazi: tishio ni tishio, iwe kwenye karatasi, picha au uso kwa uso."

Mnyanyasaji huyo alizana kampeni yake ya za kubughudhi Julai 29 mwaka jana, siku 5 baada ya Benki Kuu ya Uingereza kutangaza kuwa Jane Austen, mwandishi wa riwaya wa Kiingereza wa karne ya 18 atakuwa  sura mpya katika noti za Paundi 10.

Nunn aliposti tweets luluki dhidi ya kwa mwanasiasa huyo wa kike, ikiwa ni pamoja na video 6. Katika tweet yake moja, alieleza kuwa njia mwafaka ya kumbaka mbunge huyo ni kwa kumzamisha majini kwanza.

Baadaye ali-tweet "kama huwezi kutishia kumbaka mtu maarufu (celebrity), kuna haja gani ya kuwa nao?"

Nunn atahukumiwa tarehe 29 mwezi huu na waendesha mashtaka wameeleza kuwa wataomba kibali cha kumzuwia kuwasiliana na Mbunge huyo mwanamke.

CHANZO : Daily Express 

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.