1 Dec 2014

World AIDS Day 2014 Theme

UKIMWI ulikuwepo na bado upo, na hadi sasa dalili za kuutokomeza ugonjwa huo bado ni ndogo kwani hakuna kinga wala tiba.

Una na fasi ya kuchangia mapambano dhidi ya ugonjwa huu

ACHA ZINAA

KUWA MWAMINIFU

IKISHINDIKANA, TUMIA KINGA

Lakini badala ya kuamini tu kuwa upo salama, ni muhimu pia kufanya vipimo vya ugonjwa huo ili kutambua kama upo salama au umeathirika. Ukiwa salama, Mshukuru Mungu na endelea kuwa makini. Ikitokea bahati mbaya kuwa umeathirika, usikate tamaa kwani kuna matibabu mbalimbali na ya uhakika ya kumwezesha mwathirika wa ugonjwa huu kuishi maisha marefu (japo si tiba kamili).

Iwapo ndugu, jamaa au rafiki yako ameathirika, usimtenge. Mpatie kila aina ya sapoti ikiwa ni pamoja na kum-treat kama binadamu mwenzio. 

Sikiliza wimbo huu wa 'Mshikaji Mmoja' wa msanii wa Kitanzania JOSLIN ambao una mafunzo mengi kuhusu UKIMWI (isipokuwa hitimisho kuwa "ukiupata ni kifo") 

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.