17 Jun 2015

I am not in anyway whatsoever pretending to act like mie ndo mwenye uchungu saaana na Tanzania yetu ila kuna vitu ukivisikia kutoka huko nyumbani vinaumiza sana. Nimepata taarifa za kusikitisha sana. Goes like this: kuna watumishi flani wa serikali katika taasisi moja nyeti sana waliokuwa wakitumia utumishi wao katika taasisi hiyo kufanya kila aina ya maovu: kukodisha silaha kwa majambazi, kuwatapeli watu kwa kuwapelekea katika ofisi nyeti ili kujenga imani yao kisha kuwaliza...lakini kibaya zaidi, ninataarifiwa kuwa watu hao baada ya kufukuzwa kazi wanaendelea na uhalifu wao.Kibaya zaidi, hawa sio wahalifu wa kawaida, ni watu waliofunzwa kukabiliana na uhalifu...kwahiyo wanajua mbinu za kuepuka vyombo vya dola.

Kinachoniuma ni kwamba taasisi husika ilichukua uamuzi wa kuwafukuza kazi badala ya kuwapeleka jela, kwa sababu makosa yao kisheria yana adhabu moja tu: JELA. Sasa kwa vile baadhi ya wahusika walikuwa na mhusiano na vigogo flani, wakasamehewa kwa kufukuzwa kazi tu.Lakini naambiwa balaa wanalosababisha huo mtaani ni balaa.

Hili ndilo tatizo kubwa linaloikwaza Tanzania yetu: KULINDANA. Si kwamba wahusika walipoamua 'kuwasamehe' wahusika hao walikuwa hawajui madhara watakayosababisha mtaani, lakini kutokana na ubinafsi wao na kutojali madhara yatakayowakumba Watanzania wenzao, wakaamua kuwalinda wahalifu hao.

Ninaifuatilia taarifa hii kwa karibu, na nitaendelea kuwahabarisha.Nina majina ya wahusika lakini kuna taratibu flani inabidi nizifuate ili nisiishie kuwapa watu kisingizo cha 'kuvujisha siri za nchi.'

Jamani, Tanzania ni yetu sote.Tusifikirie tu kuhusu leo.Kuna kesho, mwaka kesho na miaka kadhaa huko mbele.Tunawaandalia nini wajukuu zetu?

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.