19 Oct 2018



Kwamba Daudi Albert Bashite ni mhusika mkuu katika utekelezaji wa mpango wa kijahili wa kutemka mfanyabashara maarufu Mohammed Dewji sio suala la siri. Na wala haihitaji uelewa mkubwa wa uchungui wa matukio ya kihalifu kubaini uhusika wa Bashite.

In fact, kabla ya Mo kutekwa, mfanyabiashara mwingine maarufu jijini Dar naye alinusurika kutekwa na vijana wa Bashite. Na majuzi, mfanyabiashara huyo amelazimika kumwaga shehena ya bidhaa baharini baada ya Bashite kutishia kumbambikia kesi kuhusu shehena hiyo.

Ni siri ya wazi kwamba Bashite amekuwa akiwanyanyasa wafanyabishara mbalimbali, akidai mamilioni ya shilingi, huku aktishia kuwabambikizia kesi za madawa ya kulevya iwapo watakataa. Huyo Mo mwenyewe “alishatolewa upepo” mara kadhaa na Bashite.

Kwa upande mwingine, Bashite amefika hapo alipo kwa kubebwa na watawala wetu. Baada ya kumpiga Mzee Warioba kwenye mchakato wa Katiba mpya, Rais wa Awamu ya Nne Jakaya Kikwete akamzawadia Bashite ukuu wa wilaya. 

Na katika mazingira ya kushangaza, Rais Magufuli akaona Bashite hastahili kuwa mkuu wa wilaya bali apewe ukuu wa mkoa kabisa. Ninaweza kusema bila kuuma maneno kuwa huu ni mmoja wa maamuzi mabovu kabisa ya Rais Magufuli. Na huenda akatambua hilo huko mbeleni akiendelea kumkumbatia jahili huyo.
Baada ya kupewa ukuu wa mkoa, Bashite akatokea kuwa mtu wa karibu kabisa wa Magufuli. Hata alipovamia studio za Clouds Media Group, Mkuu huyo wa nchi akawamtetea vikali kijana huyo aliyetenda kosa la jinai. Hiyo ikampa Bashite jeuri na kiburi kikubwa.

Mara kadhaa, Magufuli alikuwa akimmwagia sifa Bashite akidai ndio Mkuu wa Mkoa mchapakazi kuliko wote. Mchapakazi kwa kufeli kisha kufojic heti na jina lake? Mchapakazi kwa kudai rushwa kwa wafanyabishara mbalimbali? Mchapakazi kwa yeye na “mlevi mbwa” Kitwanga kumpa yule mbwa Musiba shilingi milioni 7 za kututangaza akina sie kuwa ni watu hatari?

Kumdekeza Bashite na kumpendelea hata pale alipofanya uahlifu ndio kumemfanya haramia huyu kufikia hatua ya kufanikisha mpango wa kumteka Mo Dewji. Bashite ni kiumbe hatari kabisa na janga kubwa kuliko yote katika historia ya Tanzania. Na amin nawaambia, hata alindwe vipi na baba yake, mwisho wa jahili huyu utakuwa mbaya sana. 

Na sio kama ninamtetea Magufuli, ila hili la kumteka Mo, ni mpango binafsi wa Bashite alioufanya kwa niaba ya washirika wake kutoka nje ya nchi. 

Naamini hadi kufikia muda huu, watu wa Kitengo wameshamfahamisha Magufuli kuwa ‘mwanae’ Bashite ndio aliyemteka Mo, na anajua alipo. 

Na hapo ndio tunabaki kujiuliza: je Magufuli atakuwa tayari kuhatarisha urais wake na “kumbeba” tena Bashite? Tayari kuna dalili hizi maana mpaka wakati ninaandika makala hii, Bashite alikuwa hajakamatwa wala kuhojiwa, achilia mbali kutumbuliwa.
Magufuli anaachia fursa adimu ya kujitenga na kijana huyo mhuni ambaye amefanya jithada kubwa kuuharibu utawala wa “baba yake.” Kama kuna mtu mmoja amechangia sana kumfarakanisha Magufuli na Watanzania wengi si mwingine bali Bashite.

Kwa kumchukulia hatua Bashite, Magufuli angeuwa ndege wengi kwa jiwe moja. Kwanza, kumtimua Bashite kungemfanya aonekane kuwa sio tu amekerwa na kutekwa kwa Mo Dewji na bali pia “kujisafisha” yeye mwenyewe dhidi ya tuhuma kuwa huenda waliomteka Mo ni watu wa serikali yake Magufuli.

Lakini pia, kwa kumtumbua Bashite, Magufuli angejiweka kando na mtu ambaye amefanya kila linalowezekana kuchafua jina la “baba yake.” Kama nilivyotanabaisha awali, Bashite amechangia mno kuwafanya Watanzania wengi tu kutoipenda serikali ya Awamu ya Tano.

Pengine kubwa zaidi ya yote ni ukweli kwamba, kwa Magufuli kuchukua hatua dhidi ya Bashite itamsaidia kujenga mahusiano bora na wafanyabiashara wakubwa ambao wamekuwa wahanga wakubwa wa uonevu wa Bashite.

Lakini kubwa zaidi katika hili ni Magufuli kuepusha uwezekano wa wafanyabiashara hao kuungana na maadui wake (Magufuli) hususan ndani ya CCM ambako kuna makundi kadhaa yenye dhamira ya kumfanya awe Rais wa muhula mmoja kama sio kumng’oa kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Ni vigumu kubashiri kwa hakika kuwa hatimaye Magufuli atamwaga Bashite lakini kilicho bayana ni kwamba ana option moja tu: amlinde ahatarishe uraia wake au ambwage ajitengenezee mazingira mazuri ya urais wake. Ifahamike mapema kuwa ikitokea Magufuli kamtumbua Bashite basi Tanzania italipuka kwa mayowe na vigelegele kana kwamba imeshinda Kombe la Dunia.

Mwisho, hatua za Magufuli dhidi ya Bashite ndio ufumbuzi pekee wa sakata la kutekwa kwa Mo. Yaani akikamatwa na kuhojiwa, ataeleza Mo yuko wapi, na hivyo kuwezesha kupatikana kwa mfanya biashara huyo tajiri si Tanzania tu bali pia ni mmoja wa matajiri wakubwa Afrika na duniani kwa ujumla. Ni matumaini yangu kuwa Magufuli atatambua kuwa akiendelea kumlea Bashite basi huenda “akaondoka nae.”


0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.