31 Mar 2020


Huenda kuna watakaosema wakati huu ambapo nchi na dunia ipo kwenye kipindi kigumu kutokana na janga la krona, si muda mwafaka wa kutupiana lawama. Lakini vipi kama lawama hizo zinaweza kusaidia kuleta mabadiliko chanya katika jitihada za kukabiliana na janga hilo?

Kuna mfululizo wa matukio yanayoashiria bayana kuwa Rais Magufuli ana mapungufu ya kiuongozi kila wakati Tanzania yetu inapokumbwa na majanga. Tukio kubwa zaidi ni lile la tetemeko la ardhi Kagera ambapo kwanza alipuuza kutembelea wahanga kwa siku kadhaa, na alipoamua kuwatembelea, akaishia "kuwasemea ovyo" kwa kudai si yeye aliyesababisha tetemeko hilo.


Kwanini tukio hili ni kubwa zaidi? Si tu kwa vile liliathiri watu wengi lakini pia kwa sababu Magufuli anatokea eneo hilo. Kwa lugha nyingine, kama anaweza "kuwafanyia hivyo ndugu zake," kwaninia shindwe kwa "watu baki"?

Matukio mengine ambayo yalipuuzwa na Magufuli ni pamoja na maombolezo ya askari wetu waliouawa huko DRC walikokuwa wakishiriki operesheni za kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda amani nchini humo. Licha ya kuwa Amiri Jeshi Mkuu, hakushiriki kuaga miili ya mashujaa wetu hao.


Janga jingine kwa taifa ambalo Magufuli alilipuuza nivifo vya wanafunzi kadhaa wa shule ya St Lucky huko Arusha

Kadhalika, Magufuli alipuuzia janga jingine lililotokea kanda ya Ziwa ambapo mamia walifariki katika ajali ya kivuko cha MV Nyerere


Na akapuuzia pia janga la mlipuko wa lori la mafuta uliopolekea vifo kadhaa

Na kama alivyopuuzia janga la vifo vya mashujaa wetu waliouwa huko DRC, Magufuli hakutokea kwenye kuaga miili ya polisi waliouawa huko MKIRU, licha ya kuwa Amiri Jeshi Mkuu

Katika janga hili la korona, mwenendo wake tangu mwanzo umekuwa ni mwendelezo wa dharau zake kwa majanga yanapolikumba taifa letu. Baada ya Waziri wa Afya Ummy Mwalimu kutangaza kuwa korona imeingia Tanzania, ilimchukua Magufuli siku 10 hivi kuongea lolote kuhusu janga hilo.

Na alipofungua mdomo wake, akaongea vitu vya ovyo kabisa. Akiwa Kanisani, aliweka kando uanasayansi wake na kudai kuwa "ukimwi unaua, malaria inaua, na ajali pia zinaua," na kusema kuwa "tunatishana sana (kuhusu korona). Haya si maneno ya kuyatarajia kutoka kwa kiongozi mkuu wa nchi ambaye pia ni mfariji mkuu.



Baadaye akahutubia taifa na kuendelea kutoa ujumbe usio na tija.



Baada ya ukimya wa siku kadhaa akaibukia tena huko Dodoma ambapo wakati taifa likiwa kwenye hofu na mashaka ya janga hilo la korona, mkuu huyo wa nchi akaonekana akifanya mzaha kwa kujilaza kwenye mawe.



Na majuzi alionekana akipuuza ushauri wa kitaalamu dhidi ya maambukizi ya korona unaowataka watu kuepuka mikusanyiko.

Na hii ilikuwa baada ya matukio makubwa mawili huko Dodoma yaliyosababisha mkusanyiko - kikao cha baraza la mawaziri na wakuu wa vyombo vya dola, na baadaye kupokea ripoti za TAKUKURU na CAG.
Image

Image

Kwa minajili ya kumbukumbu, mwaka juzi, mwanasiasa nguli wa upinzani Tundu Lissu alihoji kasumba hiyo ya Magufuli kujitenga na majanga ya kitaifa.

Huu sio tu ni mwaka wa tano tangu Magufuli aingie madarakani lakini pia ni mwaka wa uchaguzi mkuu mwingine (kama ataruhusu). Waweza kujiuliza "anapata wapi jeuri hiy ya kupuuzia majanga ya kitaifa miaka yote hii na hata mwaka huu wa uchaguzi?" Jibu ni kwamba anafahamu fika kuwa haitomgharimu chochote. Kwa upande mmoja wapinzani wetu wamekuwa watu wa maneno zaidi kuliko vitendo, ilhali wananchi nao wakiwa bize na ubuyu. Laiti Magufuli angehisi "kuna adhabu inamsubiri" asingefanya dharau hizi. 

Lakini hata kama wapinzani wameshindwa kushikia bango hilo, na wananchi wako bize na ubuyu, ni jukumu letu sie wachache wenye uthubutu wa kukosoa kutochoka kukemea maovu kama haya. Maana sote tukikaa kimyaatadhani tunaafiki kasumba hiyo isiyopendeza.

Nimalizie makala hii kwa ujumbe huu muhimu kuhusu janga la korona.



0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.