Showing posts with label HAKI TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label HAKI TANZANIA. Show all posts

30 Mar 2009

HAYA NI MAONI YA NDUGU YANGU,BLOGA MWENZANGU DAVID MUSIKA.NAYAWASILISHA KAMA YALIVYO

ajali ngapi zilizowahi kutokea bila kuundiwa tume ya uchunguzi kwani hii ina nini? tena watu walikufa ni wawili tu! kule arusha,Tanga watu wangapi walikufa katika ajali na hatukusikia tume? kuna nini kinataka kufichwa hapa? kwanza kabisa inabidi chenge awe jela kwa kuendesha gari bila bima ya gari kwa miaka 2! ebu fikiria ungekuwa wewe unaedesha bila bima ya gari wacha kupata ajali? nahisi bado tanzania hatuna usawa!mbona yule kijana aliyemuua chacha wangwe hakupewa dhamana? au tuseme hao marehemu ndiyo walioua chenge katika ajili hiyo wangepewa dhamana? jamani lazima tutenda haki kwa kila mtanzania kwa vile ni haki ya mtanzania kuwa na haki katika nchi yake.kumwachia mzee chenge huru ni kuendeleza matabaka ya walionacho na wasio nacho. .

NAAMINI WAPENDA HAKI WOTE WANAUNGA MKONO MTIZAMO WA MR MUSIKA.HAKI SHURTI ITENDEKE PASIPO KUANGALIA MATABAKA.
(Pichani juu ni siku Chenge alipopokelewa kishujaa jimboni kwake baada ya kulazimika kujiuzulu kufuatia tuhuma za kumiliki vijisenti huko Jersey,UK.Unaweza kujiuliza inakuwaje watu wenye akili zao timamu wajazane namna hiyo kumlaki mtuhumiwa wa ufisadi.....jibu la swali hilo linaweza kutoa mwangaza wa namna vita ya ufisadi ilivyo ngumu,hususan kwenye kuondoa mentality ya kuwaenzi white-collar criminals).

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.