Showing posts with label KAFULILA. Show all posts
Showing posts with label KAFULILA. Show all posts

5 Jan 2010


ASEMA SIASA SI CHAGUO LAKE

Salim Said na Fidelis Butahe

NAIBU Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe ameibuka tena na kutonesha majeraha ya mgogoro uliokuwapo ndani ya chama chake, akisema haridhiki na uamuzi wa chama hicho kuwaengua David Kafulila na Danda Juju.

Ingawa Kabwe hakutaja jina, kauli yake kupinga maamuzi ya kuwavua madaraka wanachama hao; imeonyesha kumzungumzia Katibu Mkuu wa Chadema Dk Willibrod Slaa kwa vile ndiye aliyesema Kafulila na Danda si kitu ndani ya chama hicho na kwamba, anaweza kuwashughulikia bila vikao vya chama.

"Mimi sipendi siasa za kinafiki, uamuzi wa kuwavua nyadhifa zao kina Kafulila haukuniridhisha kwa sababu haukuwa mzuri, ingawa ulipitishwa na mamlaka husika, katika vikao husika," alisema Kabwe katika kipindi cha Jambo Tanzania kilichorushwa na Televisheni ya Taifa (TBC1) jana asubuhi na kuongeza:

"Unajua unaweza ukawa na maamuzi yaliyofanywa katika vikao halali, lakini yasikuridhishe, pia unaweza ukawa na maamuzi katika vikao hivyo hivyo yakakuridhisha. Lakini mimi sikuridhishwa na mamuzi ya kina Kafulila kuvuliwa nyadhifa zao."...INAENDELEA HAPA

PAMOJA NA HESHIMA KUBWA NILIYONAYO KWA ZITTO LAKINI NADHANI KUENDELEA KWAKE KUNG'ANG'ANIA ISHU YA AKINA KAFULILA KUNAMPOTEZEA HAIBA YAKE YA KISIASA MIONGONI MWA WAPENDA MABADILIKO YA KISIASA HUKO NYUMBANI NA WANANCHI KWA UJUMLA.

HAYA MALALAMIKO YATAENDELEA HADI LINI?NA YANAENDELEA KWA FAIDA YA NANI?KAFULILA NA NA MWENZIE WALIKUWA WAAJIRIWA WA CHADEMA.MWAJIRI ANAWEZA KUMPANDISHA AU KUMSHUSHA CHEO MWAJIRIWA WAKE KULINGANA NA TARATIBU NA KANUNI ZA AJIRA HUSIKA.NA IWAPO MWAJIRIWA ATASHUSHWA CHEO KINYUME NA KANUNI HUSIKA BASI ANA HAKI YA KUPELEKA MALALAMIKO HAYO SEHEMU HUSIKA KAMA SI KUCHUKUA HATUA YA KUACHA KAZI KAMA WALIVYOFANYA WANASIASA HAO.HADI HAPO TATIZO LIKO WAPI?

JE ZITTO HADHANI KWAMBA KUTOAFIKIANA NA MAAMUZI YA NGAZI ZA JUU KATIKA CHAMA CHAKE NI SAWA NA KUTAFIKIANA NA CHAMA CHENYEWE AMBACHO YEYE NI KIONGOZI PIA?JE ZITTO SI SEHEMU YA UONGOZI ULIOFIKIA MAAMUZI YA KUWASHUSHA VYEO AKINA KAFULILA (HATA KAMA SI YEYE BINAFSI ALIYEFANYA HIVYO)?HIVI HAKUNA COLLECTIVE RESPONSIBILITY NDANI YA CHADEMA?

PENGINE BADALA YA KUENDELEA KULALAMIKA PASIPO DALILI YA MALALAMIKO HAYO KULETA MABADILIKO NI VEMA KWA MH ZITTO KAMA CHADEMA BADO INAFAA KUWA MAKAZI YAKE KISIASA.VINGINEVYO ITAKUWA KAMA KELELE ZA AKINA MWAKYEMBE KULALAMIKIA UFISADI NDANI YA CCM ILHALI WAO NAO NI SEHEMU YA CHAMA KILICHOGEUZA UFISADI KUWA SERA YAKE.IT SIMPLY DOESN'T MAKE SENSE.

NADHANI KUNA UMUHIMU WA KUIGA BUSARA ZA MKE (RASMI) WA TIGER WOODS KATIKA NAMNA ANAVY-HANDLE SKANDALI ZA UZINZI ZINAZOMKABILI MUMEWE.MWANAMAMA HUYO AMEKUWA MAHIRI KUKWEPA VYOMBO VYA HABARI LICHA YA TETESI KUWA ATAMBWAGA MUMEWE.ANAACHA WANAHABARI NA WAMBEYA WENGINE KUENDELEA NA SPECULATIONS ZAO LAKINI MAAMUZI YAKE YA MOYONI ANAYAJUA YEYE.AKIMTALIKI MUMEWE AU AKIENDELEA NAE,SIFA MOJA KUU ITAKAYOMWANDAMA NI UMAHIRI WAKE KATIKA KU-DEAL NA MATUKIO MAZITO KAMA HILO LA MUMEWE.


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.