Showing posts with label KINGUNGE NGOMBALE MWIRU. Show all posts
Showing posts with label KINGUNGE NGOMBALE MWIRU. Show all posts

10 Oct 2009


SOMA KAULI ZA BABU HUYU HAPA CHINI KISHA UELEWE KWANINI NATOA WITO AONEWE HURUMA KWA KUPUMZISHWA.

Ahofia wabunge wengi CCM kutorudi Bungeni
Na Keneth Goliama, Mbeya

MBUNGE wa kuteuliwa wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kingunge Ngombale Mwiru, amewashutumu viongozi wanaounda makundi ndani ya chama hicho na kuwaita waliochanganyikiwa.

Mbunge huyo aliapa kuwa matajiri wasipewe kipaumbele katika uongozi, kwani watu wakishakuwa na fedha wanajiingiza katika siasa kufanikisha malengo yao ya kibiashara.

Kingunge ambaye pia ni Naibu Kamanda UVCCM Taifa,aliyasema jana wakati akiwaapisha Makamanda wa Mkoa wa Mbeya kwenye ukumbi wa Mkapa.

Aliwataka makamanda hao kufanya kazi ya kuwashauri vijana na sio kuwaingiza vijana katika makundi yaliyopo ndani ya chama hicho.

Kingunge alisema kauli za baadhi ya viongozi kuwa, wabunge wengi wa CCM hawatarudi katika ubunge mwaka 2010 ni kweli kwa sababu kunahitajika mabadiliko katika uongozi ndani ya chama.

Hata hivyo, alisema wabunge hao wapya ni faraja kwa CCM kwa sababu watakuwa ni wakutoka ndani ya chama hicho.

Aliongeza licha ya Mkoa wa Mbeya ni mingoni mwa mikoa ambayo ilitoa watu waliokuwa mstari wa mbele kugombea uhuru , lakini sifa hiyo imeharibiwa na viongozi wachache.

Kingunge alisema baadhi ya viongozi mkoani hapa wanauhasama wa kugombea madaraka na kwamba sasa ugomvi huo unakiharibia chama.

Akiunga mkono jitihada za vijana wa mkoa huo kupambana na mafisadi, Kingunge aliwataka wasiache kutetea haki yao kwa sababu vijana ndio wenye nguvu katika maendeleo ya jamii na siasa.

Kingunge aliwaasa wanachama hao kukataa kurubuniwa na watu wenye fedha kwani kukubali kufanya hivyo ni kuua chama.

Baadhi ya viongozi wamefanikiwa kuwarubuni vijana kwa fedha ili waweze kujinufaisha wenyewe na kuharibu siasa mkoani hapa, alisema Kingunge

Alikionya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa, hakijui siasa ndio maanakimejaa matatizo matupu na uchaguzi wao ni ovyo na kwamba hakina uwezo wa kupewa kuongoza dola.

CHANZO: Mwananchi

HIVI ALIYECHANGANYKIWA NI NANI KATI YA KINGUNGE NA HAO ANAOWAITA "WAMECHANGANYIKIWA."MAJUZI,MTETEZI MAHIRI WA MAFISADI,YUSUPH MAKAMBA NAE ALITOA TAMKO LINALOSHOBIHIANA NA HILI LA KINGUNGE,MWANASIASA ALIYETUZUGA ENZI ZA MWALIMU KUWA NI MFUASI MAHIRI WA UJAMAA ONLY KUIBUKA MTETEZI MAHIRI WA MAFISADI.LEO,MIEZI MICHACHE KABLA YA UCHAGUZI MKUU,NAE ANAJITUTUMUA KUKEMEA MAFISADI!?HUKU NI KUCHANGANYIKIWA KUNAKONASIBISHWA NA KUZEEKA VIBAYA.

14 Aug 2009


Kingunge Ngombale Mwiru ni mkingwe,kiumri,kisiasa na kimadaraka.Japo umri si kigezo muhimu cha kuwa na busara,ukongwe katika fani flani unatarajiwa kuambatana na busara.Lakini hali si hivyo kwa Kingunge.Kuna nyakati baada ya kifo cha Nyerere baadhi ya watu walitarajia kuwa Kingunge angefanikiwa kuendeleza mema ya Mwalimu hasa kwa vile tuliaminishwa kwamba mwanasiasa huyu (Kingunge) ana damu ya Ujamaa kiasi cha kuachana na mambo ya imani ya kidini.Tuliambiwa dini ya Kingunge ni Ujamaa.

Pamoja na mapungufu ya hapa na pale,Nyerere anaendelea kukumbukwa kwa jitihada zake za kujenga jamii yenye kukaribia usawa na kuchukia unyonyaji.Sijui Kingunge akifa tutamkumbuka kwa lipi zaidi ya kuzeekea kwake kwenye siasa pasipo tija na hili jukumu jipya alilojipachika la u-Baba wa Taifa wa Mafisadi.Kingunge ni mnafiki mkubwa kwa vile wakati anadai kuwa viongozi wa kanisa "wangeufyata" laiti Mwalimu angekuwa hai,sijui yeye Kingunge angemwambia nini anaposimama kidete kutetea mafisadi.

Haya ndio madhara ya kuviacha vikongwe madarakani hadi vinapoteza uwezo wa kufikiri.Na huyu ni mshauri wa kiongozi wa nchi!Kama uwezo wake binafsi wa kufikiri umefikia kikomo atawezaje kumshauri mtu mwingine,achilia mbali kiongozi wa nchi?

Kwanini adai waraka wa kanisa utawagawa Watanzania lakini akae kimya pale chama chake cha CCM kilipocheza karata-tatu ya kisiasa kilipoahidi (katika manifesto yake ya uchaguzi 2005) uanzishwaji wa mahakama ya kadhi kwa Waislam?Binafsi,sina tatizo na uanzishwaji wa mahakama ya kadhi iwapo mambo flani muhimu yatazingatiwa,lakini kwa uendeshaji wa mambo kwa mtindo wa zima moto,au pata potea,ni dhahiri uamuzi huo wa mahakama ya kadhi unaweza kulipeleka pabaya taifa.Narudia,tatizo sio uanzishwaji au kuwepo kwa mahakama hiyo,bali ni ubabaishaji wa viongozi wetu katika kushughulikia uanzishwaji na uwepo wake pasipo kuathiri umoja wa kitaifa.

Na kikongwe huyu (Kingunge) mbona yuko kimya hadi leo baada ya chama chake kusuasua katika utekelezaji wa ahadi hiyo ya uanzishwaji wa mahakama ya kadhi?Kama uamuzi wa CCM kutaja katika manifesto yake juu ya suala hilo ulikuwa hatari (kwa mujibu wa wanaodhani hivyo),kitendo cha chama hicho kurushiana mpira kila kinapoulizwa na waahidiwa (Waislam) kuhusu utekelezaji ni cha hatari zaidi.

Tatizo la Kingunge kuhusu waraka wa kanisa haliko kwenye kile anachodai "kuijua vizuri nchi yetu" bali wasiwasi wake kwamba pindi waraka huo ukitekelezwa kwa vitendo basi yeye na mafisadi anaowatetea watakuwa katika wakati mgumu.Kwa lugha nyingine,Kingunge anatetea maslahi ya tabaka alilomo na analoliwakilisha (mafisadi).

Hivi ni lini umewahi kumsikia Kingunge akikemea ufisadi?Hivi Kanisa lingetoa wapi wazo la kujana waraka huo laiti kikongwe hiki cha siasa kingesimama kidete kuendeleza harakati za Mwalimu kupambana na unyonyaji?Badala ya kutueleza yeye anafanya nini kuhakikisha nchi inakwenda vizuri anakimbil;ia kukosoa wengine kuwa wanataka kuipeleka nchi pabaya.

Halafu inakera zaidi kumskikia babu huyu akijifanya kama yeye ndio mwenye hatimili ya historia,mwelekeo na chochote kuhusu Tanzania.Eti anakemea wenzake "wanaodakia hoja pasipo kujua vema tumefikaje hapa..."Tumefika hapa tulipo kwa sababu ya watu kama Kingunge,wanafiki waliojifika kwenye ngozi wa kondoo wakati wa Mwalimu kumbe ni mbwa mwitu wa kifisadi waliokuwa wakisubiri Mwalimu aondoke kwenye ulingo wa siasa kisha watufisadi.

Kingunge ni mtu hatari sana,na asipodhibitiwa ataiingiza nchi katika machafuko.Kishajizeekea,hajali litakalotukumba kwa vile ashachuma vya kutosha na anamsubiri Muumba amrejeshe mbele ya haki (na huko atakuwa na maswali lukuki ya kujibu atapokutana na Mwalimu).Ni muhimu kwa wanaomlea kikongwe huyu wakamhurumia kwa kumpatia pumziko haraka,la sivyo "atazidi kulikoroga".

Mungu ibariki Tanzania na waangamize mafisadi na watetezi wao,hususan wale wanaotaka ligi
na wachunga kondoo wako.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.