Showing posts with label MIZENGO PINDA. Show all posts
Showing posts with label MIZENGO PINDA. Show all posts

7 Nov 2008


Na John Daniel, Dodoma 

SERIKALI imeeleza kukasirishwa na gumzo la uvujaji wa mitihani na tatizo la vyeti visivyo halali na kuahidi kumulika upya kwa ukali zaidi Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) na kuhakikisha tatizo hilo linakwisha. 

Akijibu maswali ya papo kwa hapo bungeni jana, Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, alisema ni aibu kwa Taifa kuzungumza kuvuja kwa mitihani mara kwa mara na kwamba analazimika kulizungumzia suala hilo kwa kuwa ni tatizo lililopo, lakini ni wakati muafaka wa kulikomesha. 

Katika swali lake kwa Waziri Mkuu, Mbunge wa Viti Maalumu, Bibi Magdalena Sakaya (CUF), aliitaka Serikali kutoa tamko kutokana na tatizo hilo, ambalo lililikumba Taifa hivi karibuni na kusababisha wanafunzi wa kidato cha nne kuahiroisha kufanya mtihani wa Hisabati. 

Pia Mbunge huyo aliitaka Serikali kutoa tamko akiihituhumu NECTA kwamba ndiye mhusika mkuu wa kuchapisha na kuuza vyeti bandia mitaani, jambo linalochangia kushusha kiwango cha elimu nchini. 

"Kwanza ni aibu sana kwa Taifa mitihani inavuja ni aibu kwa wazazi kununua mtihani mtaani, rai yangu kwa wazazi na Watanzania wote, tukatae tatizo hili, tumekubaliana na Waziri wa Elimu chombo chetu hiki NECTA lazima kiangaliwe kwa ukali zaidi,” alisema Bw. Pinda. 

Alisema licha ya mtihani wa Hisabati ulioandaliwa kwa ajili ya kidato cha nne mwaka huu kuvuja, lakini mitihani mingine haikuvuja na badala yake baaadhi ya watu waliibuka na kuuza makaratasi mitaani na kuvutia hisia za watu kwamba ndiyo mitihani halisi. 

CHANZO:
Majira

KUKASIRISHWA PEKEE NA KUINGALIA NECTA KWA UKALI ZAIDI PASIPO KUWAWAJIBISHA WAHUSIKA ITASAIDIAJE KUTATUA TATIZO HILI?

17 Oct 2008

Picha kwa Hisani ya MichuziJr
Pinda ataja sababu za kilimo kuwa duni
IMEELEZWA kuwa kilimo cha Tanzania bado kiko duni, kutokana na wakulima wengi kulima bila ya kutekeleza kanuni za kilimo bora na hivyo kuchangia kushuka kwa uzalishaji wa mazao mbalimbali nchini. 

Hayo yamesemwa jana na Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda katika ukumbi wa Bz mkoani Morogoro wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kuhamasisha kilimo, uliohusisha mikoa ya Kigoma, Mbeya , Ruvuma , Rukwa , Iringa na Morogoro . 

Waziri Pinda alisema kuwa kilimo cha Tanzania bado duni kutokna na eneo linalolimwa ni kidogo na tija ni ndogo, ambapo alisema inakadiliwa kuwa eneo linalofaa kwa kilimo ni hekta milioni 44 na eneo linalotumika ni sawa na asilimia 24 ya eneo hilo. 

Alisema kuwa kwa upande wa kilimo cha umwagiliaji lina hekta milioni 29.4 hata hivyo eneo linalotumika ni sawa na hekta 290,000 sawa na asilimia moja . 

“Ni vyema tukaangalia kuongeza maeneo ya kulima kama kweli tumedhamiria kuongeza tija katika sekta ya kilimo," alisema Waziri Pinda . 

Aidha waziri Pinda aliongeza kuwa mbali na changamoto hiyo katika sekta ya kilimo bado huduma za ugani ni duni na kudai uzoefu unaonesha kuwa wakulima wengi wanalima bila ya kufuata kanuni za kilimo bora . 

Alisema kuwa hali hiyo imekuwa ikisababisha kilimo chao kushuka na kutokuwa na tija na mavuno yao kuwa kidogo, hali ambayo wizara inatakiwa kujiuliza ina maofisa ugani wangapi mikoani na vitendea kazi kiasi gani viko katika ofisi zao, ikiwa pamoja na kujiwekea mipango ya kazi. 

Waziri Pinda alisema kuwa sababu nyingine zinazochangia hali hiyo ni matumizi duni ya teknolojia za kilimo cha kisasa hasa matumizi ya jembe la mkono, badala ya matrekta. 

Alisema kuwa takwimu zinaonesha kuwa asilimia 70 ya wakulima nchini hutumia jembe la mkono na asilimia 20 hutumia plau wakati asilimia 10 hutumia matrekta takwimu ambayo ni ndogo katika kufikia malengo ya uzalishaji na kuboresha sekta ya kilimo nchini.


CHANZO: Majira

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.