Showing posts with label MUHAMMAD IBN SIRIN. Show all posts
Showing posts with label MUHAMMAD IBN SIRIN. Show all posts

5 May 2010

Je una ndoto za kupata shahada ya juu?Basi jaribu shahada ya uzamifu (doctorate) ya ndoto,jambo linalotarajiwa kuwa halisi nchini Saudi Arabia. 

Yusuph al-Harthy,Msaudia mahiri katika kutafsiri ndoto,ana mpango wa kuanzisha taasisi ya kitaaluma itakayotoa shahada ya kwanza na ya uzalimi,na hata shahada ya uzamifu (PhD) katika ndoto na maono,kwa mujibu wa gazeti la Al-Hayat.

"Kutafsiri ndoto ni kwa asili yake ni njia ya kutoa ushauri nasaha,alisema Harthy ambaye anaendesha tovuti ya kufundisha namna ya kukokotoa maana ya ndoto.Taasisi anayotarajia kuanzisha kitashirikiana na chuo kikuu kimoja cha Uarabuni ambacho bado hakijatajwa.

Dini ya Kiislam ina historia ndefu ya kutafsiri ndoto,huku mwananzuoni wa aliyezaliwa karne ya 7,Muhammad Ibn Sirin,mwenyeji wa Basra katika Iraki ya leo,akitambulika kwa mchango wake wa kuhariri daftari (catalogue) za tafsiri za ndoto.

Harthy,ambaye hujadili ndoto kwenye vituo vya radio na shoo za runinga,haafikiani na mtizamo wa Wizara ya Saudia inayoshughulikia masuala ya Uislamu kwamba tafsiri ya ndoto sio sayansi inayoweza kufundishwa bali ni jambo linalotokana na hamasa (inspiration).

Imetafsiriwa kutoka tovuti ya Shirika la Habari la AFP

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.