Mdau mmoja mkubwa wa blogu hii amenitumia ujumbe ufuatao,nami naomba niuwasilishe kama ulivyo
KM says:
20/09/2011 09:00 
mdau ninayefatilia kazizako twitter,facebook na kwenye hii blog yetu tuk
Baada ya kufuatilia kiungo (link) kilichobainishwa na mdau huyo nimegundua kuwa chanzo cha picha husika (ambacho ni jukwaa la mtandaoni la Jamii Forums) hakikuwasilisha picha husika kwa usahihi.
Naomba kutumia fursa hii kuomba radhi kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wote walioguswa na picha husika.Kuna nyakati waandishi hujikuta katika wakati mgumu kuthibitisha uhalisia wa kila habari,picha au chanzo cha habari/picha husika.
Lakini ni matumaini yangu makubwa kuwa kila msomaji wa blogu hii ataiga mfano wa mdau MK pindi kunapojitokeza mapungufu au makosa ya aina yoyote ile.Kwangu,kukosolewa ni miongoni mwa njia za kujifunza na kujirekebisha.Naomba kumshukuru sana mdau MK kwa ujumbe wake,na ninatumini tutazidi kushirikiana.