Showing posts with label Occupy Wall Street. Show all posts
Showing posts with label Occupy Wall Street. Show all posts

16 Oct 2011

Kitu cha karibu na taaluma ya uchumi nilichomudu kukisoma ni Book Keeping(ambayo niliambulia C kwenye mtihani wa Kidato cha Nne) na Commerce (ambayo niliachana nayo Kidato cha Pili).Naomba nikiri,mie ni kilaza wa hesabu,na alama D niliyoipata katika Hisabati kwenye Mtihani wa Kidato cha Nne ilikuwa ni kama A kwangu kwani nilikuwa natarajia F.Sasa kwenye uchumi kuna mambo ya Statistics,which means namba (hesabu).Kuashiria udhaifu wangu kwenye namba,wakati ninasoma shahada ya pili ya uzamili (Shahada ya Uzamili ya Utafiti katika Utafiti wa Siasa-Master of Research in Political Research) nililazimika kuomba ku-drop somo la Quantitative Analysis.Aibu?No,ni ukweli huo!

Anyway,lengo la post hii sio kuzungumzia udhaifu wangu wa namba wala kuelezea kuhusu shule yangu bali ni swali linalonisumbua kuhusu kinachoendelea katika sehemu nyingi za nchi zilizoendelea ambapo kumekuwa na upinzani mkali dhidi ya uroho wa taasisi za fedha (mabenki,nk).

Lakini pengine kabla ya kuelekea huko,swali la msingi linaweza kuwa hili.Inakuwaje nchi kama Ugiriki ikumbwe na msukusuko wa kiuchumi ilhali akina sie (Tanzania) tunaonekana kama "tunapeta" tu?Pamoja na Ugiriki,nchi nyingine ambazo zinasumbuliwa na kuyumba kwa uchumi ni pamoja na Hispania,Ureno,na Italia (ambazo pamoja na Ugiriki zinaunda kinachoitwa PIGS-Portugal,Italy,Greece na Spain).

Hebu wachumi nifahamisheni.Hivi hao PIGS si wapo bora zaidi kiuchumi ukilinganisha na nchi kadhaa za Afrika?Sasa mbona sie tupo kama hakuna tatizo la uchumi?Au sie ni sugu?Au uchumi wetu ni kama haupo?

Halafu kuna hili la harakati dhidi ya uroho wa taasisi za fedha ambazo kwa kimsingi zimeanzia mtaa wa Wall (Wall Street) jijini New York na kupewa jina la Occupy Wall Street,na sasa zinaelekea kusambaa sehemu mbalimbali duniani kama picha zifuatazo zinavyoonyesha.Je,kwanza,kuna uwezekano wa harakati hizo kuhamia nchi masikini?Pili,kwani hazijatugusa hadi sasa?Au ni yale yale ya uchumi usiokuwepo na hivyo kutokuwa na umuhimu wa kuulalamikia?

Nitashukuru sana kama kuna mchumi yeyote atakayeniandikia kwa barua pepe [email protected], kisha nitachapisha hapa,na ninaahidi kuandika makala kwenye jarida la Raia Mwema na kumtaja mchumi mwenye jibu mwafaka

Enewei,hebu tuangalie picha za harakati za "Occupy Wall Street" zilivyosambaa sehemu mbalimbali duniani



 Wall Street,New York,Marekani

 Tokyo,Japan

 Seoul,Korea ya Kusini

 Sydney,Australia

  Sydney,Australia

 Hong Kong

 Zurich,Uswisi

 Seoul,Korea ya Kusini

 Roma, Italia

 Hong Kong

 Frankfurt,Ujerumani

 Roma, Italia

 Stockholm, Sweden

 London,Uingereza

 London,Uingereza

 Sydney, Australia

 Hong Kong

 Julian Assange na waandamani jijini London
 London
London

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.