Showing posts with label Prank. Show all posts
Showing posts with label Prank. Show all posts

1 Apr 2016

Baada ya kada wa muda mrefu wa CCM, Balozi Juma Mwapachu kutangaza kurudi CCM baada ya kukihama chama hicho tawala wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliopita, aliyekuwa mpigadebe maarufu wa mgombea urais kwa tiketi ya UKAWA, Waziri Mkuu wa zamani Frederick Sumaye, ametangaza kujiunga tena na chama hicho tawala.

Taarifa zaidi zinaeleza kuwa kuna uwezekano wa wana-UKAWA wengine, mgombea wa kiti cha urais, Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa na aliyekuwa kada mkongwe Kingunge Ngombale Mwiru, kufuata mkumbo wa Balozi Mwapachu na Sumaye, ambapo tetesi zinadai kuwa wanaweza kutangaza kurejea CCM muda wowote kuanzia sasa.

Kwa habari kamili na picha, BONYEZA HAPA

1 Apr 2014

Rais Kikwete akihutubia mamia ya Watanzania wanaoishi hapa Uingereza
Baada ya sokomoko lilodumu kwa siku kadhaa sasa kuhusu mchakato wa kupata Katiba mpya, hatimaye Rais Jakaya Kikwete ametangza kulivunja Bunge hilo akibainisha kwamba ni vigumu kwa mazingira yaliyopo kufikiwa mwafaka wowote ule, sambamba na dhamira ya kuokoa fedha za umma.

Rais aliyasema hayo alipoongea na Watanzania wanaoishi hapa Uingereza, ambapo yupo kwa ziara ya kidola ya siku tatu. Kwa maelezo kamili bofya HAPA

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.