Showing posts with label RICHMOND. Show all posts
Showing posts with label RICHMOND. Show all posts

2 Jan 2008


Makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la RAIA MWEMA inatoa changamoto ya kuwa na mashujaa watakaoweza kupambana na dhuluma,ujambazi na ufisadi dhidi ya nchi yetu.Nimetumia mifano ya mashujaa wawili,Wesley Autrey na John Smeaton kupigia mstari umuhimu wa kufanya maamuzi ya haraka (yasiyohitaji semina elekezi au kuundiwa tume ya kuchunguza tume) yatakayowanufaisha wengi.Ili kukabiliana na mafisadi na wababaishaji wengine ni lazima tuwe na "have-a-go heroes" katika fani mbalimbali,hususan uandishi wa habari na sheria,ambao wataibana TAKUKURU inapokurupuka kusema dili la Richmond lilikuwa safi ilhali Bunge limeunda tume ya kuchunguza ishu hiyo,au watambana Mwapachu anaposema uhalifu utadhibitiwa ilhali miezi kadhaa sasa imeshapita tangu akabidhiwe orodha ya wahalifu na hatujaskia kilichoendelea,au kuwabana wale wababaishaji waliotishia kwenda mahakamani baada ya kutajwa hadharani kuwa ni mafisadi,au hata kumuuliza JK kuhusu kauli yake ya mwanzoni kabisa kwamba anawajua wala rushwa na anawapa muda wabadilike...je kwa mtazamo wameshabadilika au hiyo deadline aliyoitoa kwa wala rushwa hao haijapita?

Pamoja na habari na makala nyingine zilizokwenda shule,bingirika na uungane nami mtumishi wako hapa

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.