Showing posts with label SULLIVAN SUMMIT. Show all posts
Showing posts with label SULLIVAN SUMMIT. Show all posts

14 Jun 2008

Wapendwa,naomba mniwie radhi kwa kupotea hewani kwa muda mrefu.Nilikuja nyumbani kumuuguza mama mzazi lakini kwa bahati mbaya tarehe 29/05 Bwana aliamua kumchukua na kumrejesha kwake.Makanisani wanatuambia tulitoka kwenye mavumbi na tutarejea kwenye mavumbi.Nawashukuru nyote mlioshiriana nasi kumuombea mama apone na nyote mliotoa salamu za rambiarambi ambazo kwa hakika ndio zinazotuwezesha kuwa na nguvu ya kuingia tena bloguni.
Naomba kuwapatia makala chache ambazo kutokana na matatizo niliyokuwa nayo sikuweza kuzitundika hapa.Katika makala yangu ndani ya gazeti la Raia Mwema la tarehe 28/05 nilizungumzia suala la wagombea binafsi na kutabiri kwamba huo unaweza kuwa ndio kifo cha mafisadi.Makalahiyo ilikwenda kwa kichwa WAGOMBEA BINAFSI:KIFO CHA MAFISADI CHAJA. Katika toleo lililofuatia,yaani la tarehe 04/06,nilizunguzmia kuhusu utendaji kazi wa Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu,Bwana Salva Rweyemamu.Zaidi,soma makala hiyo yenye kichwa KAULI ZA MKURUGENZI IKULU KUHUSU BALLALI MKANGANYIKO MTUPU.Makala ya wiki hii,yaani iliyotoka Jumatano ya tarehe 11/06 inazungumzia Mkutano wa Sullivan uliomalizika huko Arusha hivi karibuni.Katika makala hiyo nimejaribu kuhoji iwapo Mkutano huo umekuwa/utakuwa na faida yoyote kwa Watanzania.Makala hiyo imebeba kichwa kisemacho MKUTANO WA SULLIVAN:WAZAWA WAMENUFAIKA VIPI?

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.