Showing posts with label TAARIFA YA MSIBA. Show all posts
Showing posts with label TAARIFA YA MSIBA. Show all posts

20 Nov 2011


KWA NIABA YA WASOMAJI WA BLOGU HII NINATOA POLE NYINGI KWA BLOGA MWENZETU DINAHICIOUS KWA MSIBA MKUBWA WA KIFO CHA BABA YAKE MZAZI.

KAMA MTU NILIYEKWISHAPOTEZA MZAZI,NINAFAHAMU KIBINAFSI MAJONZI NA UCHUNGU VINAVYOAMBATANA NA KUPOTEZA MZAZI.KIFO NI KIFO LAKINI CHA MZAZI KINAGUSA SANA.KWA BAHATI MBAYA,HAKUNA MANENO YANAYOJITOSHELEZA KUMFARIJI MFIWA ZAIDI YA KUUNGANA NAYE KWA SALA KUMWOMBEA MAREHEMU APATE PUMZIKO LA MILELE NA MWANGA WA MILELE,APUMZIKE KWA AMANI.

HATA HIVYO,NILIPOFIWA NA MAMA MZAZI MWAKA 2008,PADRE ALIYEONGOZA IBADA YA MAZISHI ALISEMA HAYA: "SOTE TUMELETWA DUNIANI NA MUNGU KWA UPENDO WAKE USIOMITHILIKA.KAMA WANADAMU,TUNAPENDA TUWE PAMOJA SIKU ZOTE.LAKINI BABA YETU ALIYETULETA DUNIANI ANATUPENDA ZAIDI,NA HIVYO ANAWEZA KUTUCHUKUA WAKATI WOWOTE UKE.PAMOJA NA UCHUNGU TUNAOKUWA NAO TUNAPOONDOKEWA NA TUMPENDAYE,NI VEMA KUFAHAMU KUWA JAPO SIE TULIMPENDA MAREHEMU LAKINI BABA YETU (MUNGU) ALIMPENDA ZAIDI NA HIVYO AMEAMUA KUMCHUKUA.NA KWA VILE TUNAJUA ANA UPENDO MKUBWA BASI NA TUPATE FARAJA KUWA HUKO AENDAKO ATAPUMZISHWA KWA AMANI NA UPENDO."

NATAMBUA MANENO HAYA YANAWEZA YASISAIDIE KUPUNGUZA MAJONZI LAKINI YANAWEZA KULETA FARAJA KATIKA KIPINDI CHA MAJONZI YA MSIBA.

POLE SANA DINA,TUPO PAMOJA KATIKA SALA.

PUMZIKO LA MILELE UMPE EE BWANA NA MWANGA WA MILELE UMWANGAZIE APUMZIKE KWA AMANI AMEN

13 Oct 2011


Rejea taarifa ya msiba wa Mzee Said Muhammad Sikamkono mazishi yatafanyika kesho tarehe 13/10/2011 katika makaburi ya Hainalt Garden of Peace saa nane mchana. Ila kabla ya makaburini tunaombwa wote tufike msikiti wa Sakina Walthamstaw (basi namba 179) saa sita na nusu mchana. Msiba uko nyumbani kwa marehemu Woolwich Dorkyard ambako wote tunakaribisha muda wowote kujumuika na familia ya marehemu wakati huu wa majonzi .Wakina mama pia wanaweza kufika msikitini au nyumbani kwa marehemu kwa ajili ya kutoa pole.

Address ya sehemu ya msiba ni;

Woolwich Ferry
405,Frances Street, London.
SE18 5JU.

Kwa maelezo zaidi  tafadhali wasiliana na;

07813539025 - Haruna mbeyu.Katibu Jumuiya ya Watanzania -london

07766454596 - Abdallah Mdidi

23 Jul 2011


FAMILIA YA TULLY NGONYA(MAMA MARIA) NA IKUPA NGONYA WANASIKITIKA KUWAARIFU MSIBA WA BABA YAO MPENZI MZEE J.D. NGONYA ALIEFARIKI LEO ASUBUHI 23.7.11.
KAMA ILIVYOKUWA DESTURI YETU TUNAWAOMBA WOTE TUKUTANE TUWAFARIJI WAFIWA WAKATI WA KIPINDI HIKI KIGUMU.
MSIBA UPO 38 TRELLECK ROAD, READING RG1 6EN. 
BWANA AMETOA, BWANA AMETWAA JINA LAKE LITUKUZWE MILELE. AMEN.
TAFADHALI MJULISHE NA MWENZAKO

Imetumwa na Urban Pulse Creative

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.