18 Dec 2012


London's number one African talk show, The Sporah Show held  a Winter Celebration with friends, family, Crew, Guests,  Sponsors and partners at it's studios in the East end of London! It was a fun filled evening with lots to eat and drink while enjoying  top notch entertainment from artists, comedians, dancers and performers. The entire staff of the Sporah show including Sporah herself donned Afro wigs and set the mood for an evening of light hearted fun. The staff also treated guests to their own version of the electric slide.  Items were auctioned with proceeds going to the Keith Heart Foundation of which host Sporah Njau  is ambassador. 


MC OF THE NIGHT, PAULINE LONG
Pauline Long 
She is a Kenyan based in the UK well known for being a founder/CEO of Miss East Africa UK beauty pageant, Mr East Africa UK beauty pageant and co-founder and co-producer of Miss West Africa. She is also a regular writer for African news Newspaper and a regular guest at BEN TV,the voice of Africa radio and BBC channels. Pauline is recipient of two prestigious awards, most innovative kenyan in the UK and entrepreneurship innovation award.


Pauline Long opening the Sporah show Christmas party 2012

Pauline Long welcoming Guest of the night The Tanzanian High Commissioner to the UK, His Excellency Peter Kallaghe

Tanzania High Commissioner to the UK, walking on Stage.

Pauline handing microphone to H.E Peter Kallaghe.


TANZANIA HIGH COMMISSIONER TO THE UK,  H.E PETER KALLAGHE GIVING OUT THE SPEECH

The Crowd listening to the Tanzania High Commissioner in the UK, what he had to say about Sporah and The sporah Show

TEAM SPORAH - AFRO HAIR WAS THE THEME OF THE EVENING.


TEAM SPORAH PERFORMING CANDY BY CAMEO
Sporah Introducing The Sporah Hot Corner

BOGOSSY THE DJ.

We express our gratefulness to everyone who gave out the items for the auction such as the designers who donated their special pieces  and Ngozi for the skin and hair products  whereby all proceeds will go to the Keith Heart Foundation

IT'S NOT JUST THE SEASON TO OPEN GIFTS BUT ALSO THE SEASON TO GIVE BACK TO THE COMMUNITY.
The Sporah Show Team showing the designer dresses to the guests to be auctioned and the money raised will be donated to the Keith Heart Foundation.

Pauline long auctioning the Gold Dress by Julia Lorenz.

The auction is still going on and now its time for the African Print Jumpsuit by Maureen Amooti

THE CROWD!
Guests paying close attention to the auction.


KIDS HAD A CHANCE TO INTERVIEW SPORAH.!
One of the Kids asked Sporah on what could be her motives into promoting children with special talents on her talk show.

Ohh Sporah... so we can actually be the main guests on the sporah show??


              NOW LET'S TAKE A LOOK AT THE RED CARPET      
Sporah with The guest of honour, High Commissioner of Tanzania H.E Peter Kallaghe

The Mc of the night Pauline Long, Hon Peter Kallaghe and Sporah

Pauline Long, Mr and Mrs Peter Kallaghe and Sporah


Hon. Peter Kallaghe


Mrs Joyce Peter Kallaghe



Yan Xiang the director of Owin Studio Limited and a friend.

Trudy Hampton and Sporah

Pilly and Cameroon from Vogue Magazine


Mavis Amankwah: The Founder of Rich Vision and Sleek MakeUP (ICT Project Manager)
                    M.A Benson , The CEO Show4Africa

             Leah from Leah Africandesign

Jazz Ellington - The Voice UK

The Founder of Miss Black Africa UK, Sporah and Miss Black Africa UK

Andrew and Jully Kennett


Sporah and the number one UK based Tanzanian blogger Jestina George and her husband Mr Dullah Meru.

Sporah and Keith of THE KEITH HEART FOUNDATION

Sporah and Ethel Elaka ( Zambian Singer)

                Patrick Weir (Flyer Newspaper)


Sporah with one of the presenters in Show 4 Africa 

Jackline Wabara and Valentine the Artist

Clisha and AlecoolClothing with Sporah

Miss Congo UK

Miss Congo UK and the Organiser
Miss Malaika UK

Miss Cameroon UK

MCL dance group and  MUM

             
              Team Rich Visions.
One of the organisers Miss Black Africa UK and Sporah


Ngozi,  The CEO of m3 Cosmetics

                   MC Moseh and a friend

                    Mariam Mungula

            Shally Dee From Show4Africa

Erica Brodnock

         
                         Mr East Africa UK


Marika Rauscher - The Opera Singer

Dorothy The Talent Guru owner and her Crew

                    Glorianne Francis , The Founder of Miss Zim Diamond

                        Team Rich Visions

Keith Heart Foundation Crew

                             OTHER IMPORTANT GUESTS


THE TEAM SPORAH ON THE RED CARPET
                               THE SPORAH SHOW CREW

 SOME  GUESTS HAD SPECIAL GIFTS  FOR SPORAH.!


EXCLUSIVE GOODY BAGS FROM THE SPORAH SHOW
The guest of honour HON PETER KALLAGHE and the wife Mrs Joyce Kallaghe, receiving  the goody bags from Sporah.

 Christmas has arrived early.!

Pauline Long grabs her Goody Bag from Sporah, Beautiful.

Jestina George, Pauline Long, Mr and Mrs Kallaghe, Lulu unique pearl and Sporah posing with their goody bags.

Marika posing for the Camera before receiving her goody bag.

Ohhh Thank You Sporah...!!!!!





Thank you to everyone who came to our christmas party on the 14th December 2012. Thank you for attending and for making things so much fun!! We had a blast hosting it and hope everyone else had fun too.  Thank you also to all the individuals who donated items for the auction and the people who participated in it and this includes  MoneyGram  and  Promota Magazine  for the items in the goody bags. Once again "Thank you for making our christmas party a great success"

      WE WISH YOU A MERRY CHRISTMAS AND A HAPPY NEW YEAR.



14 Dec 2012



JUMAPILI iliyopita niliungana na ‘somo wangu’ Tanzania Bara kusherehekea siku yetu ya kuzaliwa. Japo tulizaliwa miaka tofauti, na hivyo birthday yetu ya majuzi ilikuwa ni ya kutimiza umri tofauti pia, lakini kama ilivyo ada, siku ya kuzaliwa huwa na umuhimu mkubwa kwa mhusika.
Kinyume na wengi ambao huadhimisha birthdays kwa nderemo na vifijo, binafsi kumbukumbu ya siku yangu ya kuzaliwa hunipa fursa mwafaka ya kutafakari nilikotoka, nilipo na niendako, sambamba na kumshukuru Mungu na kumwomba uhai zaidi.
Kadri miaka inavyokwenda mbele, na kadri umri wangu na wa Tanzania Bara unavyozidi kuongezeka, ndivyo ninavyojikuta nikielemewa na mzigo wa tafakuri kuhusu ‘somo wangu’ Tanzania Bara (ninatumia jina hili badala ya ‘Tanzania’ kwa sababu wenzetu wa Tanzania Visiwani walipata uhuru siku tofauti na sisi wa Bara).
Lundo la mawazo linalozidi kukua kadri ninavyoadhimisha birthdays zangu na ‘somo wangu’ Tanzania Bara linatokana na ukweli kwamba kwa kiasi fulani yayumkinika kuhisi kwamba nchi yetu badala ya kwenda mbele ni kama inarudi nyuma.
Kuna wanaohoji kuhusu suala zima la uhuru. Tulimtimua mkoloni ili tujitawale, tunufaike na rasilimali zetu badala ya rasilimali hizo kumnufaisha mkoloni pekee. Lakini kinachoendelea sasa ni ukweli mchungu kwamba ‘mkoloni mweupe’ kaondoka, na nafasi yake imechukuliwa na ‘mkoloni mweusi, Mtanzania mwenzetu.’ Takriban skandali zote kubwa zilizotikisa (na nyingine zinazoendelea kutikisa) taifa letu zimehusisha Watanzania wenzetu.
Mara kadhaa nimekuwa nikitumia kauli hii: “”angalau wakati anatukandamiza na kutunyonya, mkoloni alikuwa na excuse (isiyokubalika) kuwa Tanganyika-wakati huo- haikuwa nchi yake. Hakuwa na uchungu nayo. Lakini sasa hawa wanaotafuna nchi yetu kwa kasi ni wenzetu. Ni wanafamilia wenzetu, ndugu, jamaa au marafiki zetu. Na kibaya zaidi, wengi wao wamesomeshwa kwa jasho la Watanzania haohao wanaofisadiwa kwa kasi.”
Kwa hiyo kimsingi, mafisadi wa Kitanzania hawana ‘excuse’ (kisingizio) kwa vile si tu wanayoiangamiza ni nchi yao pia lakini hata wahanga wa ufisadi huo ni watu wanaowahusu kwa karibu.
Lakini kuna jambo ‘jipya’ lililojitokeza mwaka huu wakati wa maadhimisho ya sherehe za uhuru wetu. Katika kongamano lililofanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, baadhi ya wanasiasa vijana walinukuliwa wakitoa kauli zinazoashiria kuwa wangependa kuona sheria za uchaguzi zinabadilishwa na kuwazuwia ‘wazee waliozaliwa kabla ya Uhuru wasigombee urais.’
Huko nyuma nilishawahi kuandika makala ambayo, pamoja na mambo mengine, ilipingana na mtizamo wa Mbunge wa Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya CHADEMA, Zitto Kabwe, ambaye alinukuliwa na vyombo vya habari akidai kuwa harakati za kuleta maendeleo haziwezi kusimamiwa ipasavyo na watu waliozaliwa kabla ya Uhuru.
Katika makala hiyo nilitanabahisha bayana kuwa niliuona mtizamo huo wa Zitto kuwa ni wa kibaguzi. Na niliweka wazi hofu yangu kwamba tukianza kuwabagua wazee, tunaweza kuishia kuwabagua wanawake, wakristo/waislamu, wanene/wembamba, nk kwani sumu ya ubaguzi hutapakaa.
Kilichotokea baada ya Kongamano hilo ni kama mjadala wa umri wa mgombea urais kuhamia kwenye mtandao wa kijamii wa twitter ambako watu mbalimbali waliojitokeza kuchangia hoja zao, mie nikiwa miongoni mwao.
Binafsi, ninakubaliana na wenye mtizamo kuwa Katiba yetu inawabagua vijana kwa kulazimisha kuwa mgombea urais lazima awe na umri fulani na kuendelea. Na ubaguzi huo unakera kwa sababu hakuna uthibitisho wowote kuwa mtu mwenye miaka 40 ana uwezo bora zaidi wa kuongoza kuliko mwenye miaka 39.
Lakini binafsi ninaona hoja hii ya ‘vijana kubaguliwa’ inapindishwa makusudi na wanasiasa wenye uchu wa madaraka. Wanataka kuitumia ajenda ya umri/ujana/uzee kama turufu tu ya kufikia malengo yao ya kisiasa.
Na kutumia ajenda hiyo kusingekuwa tatizo laiti wasingeleta hoja kwamba watu waliozaliwa mwaka fulani wasiruhusiwe kugombea urais. Haiwezekani kupigania usawa kwa kuendesha ubaguzi.
Nadhani tatizo la msingi la wanasiasa wenye mtizamo huo ni ufinyu wa uelewa wao wa tatizo la msingi linaloisumbua na kuikwaza nchi yetu kuendelea. Na kinachonikera zaidi ni ukweli kuwa wapiga debe wa hoja hiyo ni wanasiasa wenye akili na uelewa mkubwa kabisa.
Tumefika hapa tulipo - yaani masikini wa hali ya juu huku nafsi zetu zikiwindwa na mafisadi wanaonekana kana kwamba wanataka kuhakikisha nchi yetu inakombwa hata kile kidogo tulichonacho- si kwa sababu ya waliozaliwa kabla au baada ya uhuru bali majambazi waliofanikiwa kupata nyadhifa ambazo wanazitumia kuifilisi nchi.
Majambazi hawa (samahani, sina neno mwafaka la kuwaelezea) ni wabinafsi wasio na uchungu na nchi yetu wala na Watanzania wenzao. Ni watu wasioguswa na ukweli kwamba kwa kuiba fedha zetu na kuzificha huko Uswisi na kwingineko, wanawaathiri pia ndugu, jamaa na marafiki zao.
Neno jepesi na mwafaka ni uhaba (wa makusudi au wa kimfumo) wa uzalendo. Kila mzalendo anajihangaisha kuifikiria nchi yake kwa hali ilivyo sasa na itakavyokuwa huko mbele. Na uzalendo hauna umri. Aliyezaliwa kabla ya uhuru au baada ya uhuru anaweza kuwa mzalendo alimradi atangulize maslahi ya nchi na wananchi mbele ya maslahi yake binafsi.
Hoja kwamba wazee wetu wameishiwa na uwezo wa kufikiri ni sawa na kuwatukana baadhi yao ambao bila wao leo hii tusingeweza hata kuwa na huo mwaka tunaodai uwe kipimo cha aidha kuruhusiwa au kutoruhusiwa kugombea.
Badala ya wanasiasa hao vijana kuhangaika na akina nani hawastahili kugombea urais kwa vile walizaliwa kabla ya uhuru ni vema wakielekeza jitihada hizo kutuambia ni akina nani wanaosababisha mgao ‘wa milele’ wa umeme, ni kina nani walioficha fedha zetu huko Uswisi, na mafisadi wengine wanaotuibia kila kukicha.
Nimalizie makala hii kwa kuwakumbusha wanasiasa hao vijana kwamba sumu wanayopanda ya ubaguzi haitoishia katika kuwabagua wazee tu bali inaweza kuelekezwa kwa makundi mengine ya kijamii yanayoonekana vikwazo kwa ‘vijana’ hao kutimiza malengo yao ya kisiasa.
UMOJA NI NGUVU UTENGANO NI UDHAIFU


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.