11 Dec 2013

Obama and the Danish Prime Minister share a joke during the memorial service as the First Lady looks on unimpressed
Moja ya picha zinazomwonyesha Rais Barack Obama 'akiwa karibu' na Waziri Mkuu wa Denmark, Helle-Thorning Schmidt,  huku mke wa Obama, Michelle,  akionekana kama asiye na furaha

  Selfie: David Cameron and Barack Obama took a picture of themselves alongside Denmark's prime minister Helle Thorning Schmidt
Obama, Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron na mwanamama Schmidt wakipata 'selfie' huku Michelle akionekana hana furaha

President Barack Obama and Danish prime minister, Helle Thorning-Schmidt talked closely to each other throughout the ceremony
Mrs Thorning-Schmidt then points out something of interest in the order of service

They then share a joke during the poignant memorial to Nelson Mandela
Obama na mwanamama Schmidt wakiwa wenye furaha tele, huku Michelle akionekana 'hana amani.'

Prominent role: U.S. President Barack Obama, who will deliver a eulogy at the service, is joined by First Lady Michelle (right)

'Abiria chunga mzigo wako...'

Cheers: When America's first couple flashed up on screen the crowd roared their approval of the U.S.'s first black President
Uwanja ulilipuka kwa chereko baada ya screens za uwanjani kumwonyesha Obama na mkewe baada ya kuchelewa kuwasili

Eulogy: U.S. President Barack Obama acknowledges the crowd as he delivers his speech at the memorial service for Nelson Mandela in Johannesburg

Eulogy: U.S. President Barack Obama delivers his speech at the memorial service for Nelson Mandela at the FNB soccer stadium in Johannesburg

'THANK YOU FOR SHARING MADIBA': HIGHLIGHTS OF OBAMA'S HEARTFELT EULOGY FOR NELSON MANDELA


To the people of South Africa - people of every race and walk of life - the world thanks you for sharing Nelson Mandela with us. His struggle was your struggle. His triumph was your triumph. 

Born during World War I, far from the corridors of power, a boy raised herding cattle and tutored by elders of his Thembu tribe - Madiba would emerge as the last great liberator of the 20th century. 

He was not a bust made of marble; he was a man of flesh and blood - a son and husband, a father and a friend. 

Mandela showed us the power of action; of taking risks on behalf of our ideals. 

Mandela understood the ties that bind the human spirit. There is a word in South Africa - 'Ubuntu' - that describes his greatest gift: his recognition that we are all bound together in ways that can be invisible to the eye; that there is a oneness to humanity; that we achieve ourselves by sharing ourselves with others, and caring for those around us.

It took a man like Madiba to free not just the prisoner, but the gaoler as well; to show that you must trust others so that they may trust you; to teach that reconciliation is not a matter of ignoring a cruel past, but a means of confronting it with inclusion, generosity and truth. He changed laws, but also hearts.

There are too many of us who happily embrace Madiba’s legacy of racial reconciliation, but passionately resist even modest reforms that would challenge chronic poverty and growing inequality. There are too many leaders who claim solidarity with Madiba’s struggle for freedom, but do not tolerate dissent from their own people. And there are too many of us who stand on the sidelines, comfortable in complacency or cynicism when our voices must be heard.

We will never see the likes of Nelson Mandela again. But let me say to the young people of Africa, and young people around the world - you can make his life’s work your own. Over thirty years ago, while still a student, I learned of Mandela and the struggles in this land. It stirred something in me. It woke me up to my responsibilities - to others, and to myself - and set me on an improbable journey that finds me here today. And while I will always fall short of Madiba’s example, he makes me want to be better.

Rare display of unity: President Obama shakes hands with Cuban leader Raul Castro in spite of the animosity between them
Tukio la kihistoria: Obama akisalimiana na Rais wa Cuba, Raul Castro

Two very different receptions: Mr Obama, who was greeted with prolonged applause, embraces South African president Jacob Zuma, who was loudly booed
Obama akim-hug Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini hukunKatibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon (kushoto) akiangalia

Wet, but well received: President Barrack Obama greets members of the crowd in the pouring rain after making his speech
Licha ya mvua, Obama aliweza kuwasalimia wananchi waliokuwa na shauku nae

Homage: Obama paid an emotional tribute to Nelson Mandela, thanking the people of South Africa for 'sharing' their former president with the world
Obama na walinzi wake

Leaving: Mr Obama waves to the camera as he walks out of the ceremony with the First Lady
Obama akiwapungia mkono wanahabari

Fitting setting: A general view of the arena which was the location of Mr Mandela's first speech in Johannesburg after he was released from prison in 1990
Mwonekano wa uwanja wa FNB yalipofanyika maombolezo ya kumuaga Mandela

'His triumph was your triumph': President Barrack Obama is shown on a big screen as he delivers his eulogy to flag-waving and umbrella-holding mourners
Screen kubwa ikimwonyesha Obama wakati anahutubia

Mutual respect: President Obama speaks to Nelson Mandela's widow Graca Machel during the memorial service

Giving his condolences: President Obama kisses Nelson Mandela's widow Graca Machel during the memorial service
Obama akitoa pole kwa mjane wa Mandela, Graca Machel

Leaders: Tony Abbott, John Key and David Cameron, prime ministers of Australia, New Zealand and Britain respectively, at the service
Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron (kulia) akiongea na Mawaziri Wakuu wa Australia, Tony Abbot (kushoto) na New Zealand, John Key

Arrival: Mr Cameron, Mr Clegg and John Major walking in to the FNB Stadium this morning
Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron, Naibu Waziri Mkuu, Nick Clegg, na Waziri Mkuu wa zamani, Sir John Major, wakiwasili

Support: Gordon Brown, who paid tribute to Mandela in the Commons yesterday, with his wife Sarah and George W. Bush
Rais wa zamani wa Marekani, George W Bush akiongea na Waziri Mkuubwa zamani wa Uingereza Gordon Brown na mkewe Sarah

Sombre occasion: Members of Nelson Mandela's family take their seats amid heavy rain ahead of his memorial service at the FNB Stadium in Soweto, near Johannesburg
Familia ya Mandela

Embarrassing: South African Jacob Zuma was roundly booed by the crowd when he got up to deliver his tribute to Mr Mandela
Rais Jacob Zuma akihutubia, ambapo alizomewa mara kadhaa

Winnie Madikizela-MandelaGraca Machel
Winnie Mandela na Graca Machel

Close: The two women refer to each other as 'sisters' even though they were both married to the same man
Winnie na Graca wakisalimiana

Respect: Nelson Mandela is shown on a giant screen inside the stadium as thousands of South Africans and global dignitaries file into the ground
Uwanjani

Empty seats: The 94,000-capacity stadium was reportedly only two-thirds full which may have due to the adverse weather conditions
Waombolezaji

Who's who of world leaders: VIPs and dignitaries watch from the tribune as rain lashes down during the memorial service
Viongozi wa mataifa mbalimbali duniani walioshiriki maombolezo ya kumuaga Mandela
Paying tribute: World leaders converged on the FNB Stadium in Soweto, the Johannesburg township that was a stronghold of support for the anti-apartheid struggle that Mandela embodied
Rais Jakaya Kikwete na Mama Salma walikuwa miongoni mwa washiriki
Rivals: But George W. Bush, pictured with wife Laura, apparently got on well with his predecessor Bill Clinton, pictured with wife Hillary and Chelsea
Marais wa zamani wa Marekani, George W Bush na mkewe Laura (juu), na Bill Clinton na mkewe Hillary na binti yao Chelsea

Clintons: The ex-President and the former Secretary of State arrived separately but were seen leaving together
Clinton, Hillary na Chelsea

Controversial: Reviled Zimbabwean President Robert Mugabe is questioned by reporters as he makes his way into the stadium
Rais wa Zimbabwe,  'Jongwe' Robert Mugabe akiwasili

Stars: U2 singer Bono and South African actress Charlize Theron talking in the crowd at the ceremony
Supastaa Bono wa U2 na mcheza sinema mwenyecasili ya Afrika Kusini, Charlize Theron

Ally: FW de Klerk, who was awarded the Nobel Prize along with Mandela for his role in ending apartheid, arrives with his wife Elita
Rais wa mwusho wa utawala wa Makaburu, Frederick De Clerk

'He has done it again... people from all walks of life, all here, united': UN Secretary General Ban Ki-Moon pays tribute to Mr Mandela
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon akihutubia

Associates: Jimmy Carter, Kofi Annan and Henry Kissinger arrived at the memorial service together
Rais wa zamani wa Marekani, Jimmy Carter (kushoto), Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Koffi Annan, na Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje wa Marekani, Henry Kissinger

Father of the country: Many, like this little boy, refer to the former president using his tribal name, Madiba
Mtoto akiwa na bango la kumbukumbu ya Mandela

9 Dec 2013

Happy birthday Tanzania
Happy birthday ME
#tweetgram #instamood #tagstagram #instadaily #instagramhub #statigram #igdaily #ignation

Ninapenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijali mwaka mwingine katika uhai wangu. Tarehe kama ya leo, miaka kadhaa iliyopita, familia ya Mzee Philemon Chahali na mkewe marehemu mama Adelina Mapango (Mungu ailaze roho yake mahali mema peponi) ilipata mtoto wa tano, wa kiume, na kumpa jina la Jamhuri kwani alizaliwa siku ya Uhuru na Jamhuri. Baadaye mtoto huyo alibatizwa na kupewa jina la Mtakatifu Evarist. 

Mwaka uliopita ulikuwa na majaribu kadhaa, kubwa zaidi ni tukio ambalo kamwe sintolisahau maishani mwangu, tarehe 2 ya mwezi Februari mwaka huu ambapo vyombo vya usalama hapa Uingereza vilinifahamisha kuwa kulikuwa na tishio la kuaminika (credible threat) dhidi ya maisha yangu. Wakati hadi leo sifahamu kwa undani kuhusu waliohusika na mkakati huo wa kidhalimu, wala kufahamu wanausalama wa hapa walifanikiwaje kujua kuhusu mpango huo, habari isiyopendeza ni ukweli kuwa hadi leo bado naishi kwa tahadhari. Wanausalama wa hapa wamekuwa wakini-update mara kwa mara, lakini wanasisitiza kuwa kwa vile hawajapata taarifa yoyote kuwa tishio hilo dhidi ya uhai wangu limekwisha, sina budi kuendelea kuzingatia ushauri wao kuhusu hatua za tahadhari kwa usalama wangu. Kwa hakika ni jambo gumu na la kuogofya lakini kwa sasa imekuwa ni sehemu ya maisha yangu ya kila siku. Hata hivyo, kwa ulinzi wa Mungu na jitihada zangu mwenyewe, ninatumaini kuwa nitaendelea kubaki salama.

Kwa bahati nzuri (au mbaya?) siku yangu ya kuzaliwa inagongana na siku ya kuzaliwa kwa Tanganyika (Tanzania Bara). Nasema kwa bahati nzuri kwa vile inapendeza kushea birthday na nchi yangu. Hata hivyo, kwa bahati mbaya (makusudi?) mwenendo wa birthday buddy wangu Tanzania Bara si wa kuridhisha hata kidogo. Kwa upande mmoja taifa letu linabakwa na mafisadi huku umasikini ukizidi kukua. Kwa hakika ni  vigumu kubashiri hatma ya taifa letu angalau miaka 10 ijayo.

Hata hivyo, kwa vile leo ni sikukuu yetu ya kuzaliwa, basi sina budi kuitakia Tanzania Bara heri na baraka ya kuzaliwa na kujitakia happy birthday mie mwenyewe pia. Ndio maana kichwa cha habari kinasema HAPPY BIRTHDAY TANZANIA BARA, HAPPY BIRTHDAY ME!

6 Dec 2013













WIKI iliyopita nilizungumza na rafiki yangu mmoja, Mtanzania mkazi wa hapa Uingereza, ambaye alikuja likizo huko nyumbani hivi karibuni. Katika maongezi yetu, rafiki yangu huyo alionekana kuguswa na mambo kadhaa aliyoyashuhudia huko. Pengine kushangazwa kwake huko kulichangiwa na ukweli kwamba amekuwa mkazi wa hapa Uingereza kwa takriban miaka 20, na hutembelea huko nyumbani kwa nadra.
Katika hali ya kusikitisha, alikaribishwa nyumbani na 'wahalifu wa kola nyeupe' (white collar criminals), ambao katika mazingira ya kushangaza walifanikiwa kumwibia simu tatu. Kwa maelezo yake, wizi huo unaelekea kufanywa na wahusika katika uwanja wa ndege, lakini kilichomkera ni suala hilo kuonekana la kawaida kabisa kwa aliowaeleza.
Baada ya tukio hilo la wizi alipata fursa kadhaa za 'kuyaona maisha halisi ya Tanzania zaidi ya simulizi za mtandaoni au kwingineko. Anasema wakati kwa kuangalia haraka haraka, Jiji la Dar es Salaam limepiga hatua kubwa kwa majengo na idadi ya magari, hali huko vijijini ya kusikitisha mno. Alibainisha kuwa wakati wengi wa ndugu, jamaa na marafiki jijini Dar walionekana kuridhika na maisha (angalau kimaongezi), hali ya vijijini imetawaliwa na kukata tamaa ya maisha, huku dalili za umasikini zikiwa zimetawala kila kona.
Lakini moja ya mambo yaliyomgusa zaidi ni uwajibikaji ofisini. Alinieleza kuwa alipokuwa Dar alikaribishwa katika baadhi ya ofisini na rafiki zake kadhaa wenye nyadhifa muhimu katika sehemu wanapofanya kazi. Kwa kiwango kikubwa, wengi wa mabosi hao hawakuonekana kuchukulia majukumu yao ya kiofisi kwa umakini na baadhi hawakusita kumwambia "hii ndiyo Bongo bwana," kwa maana ya 'Who cares?' (Nani anajali?) hata wakiboronga kazi.
Alichobaini ni kwamba wengi wa mabosi hao 'wanakula vizuri' na mabosi walio juu yao, aidha makao makuu au wizarani. Kadhalika, katika nyingi ya ofisi alizotembelea aligundua kuwa wengi wa mabosi ni kama 'miungu-watu' kiasi kwamba uwezekano wa watumishi wa chini kuwakosoa mabosi wao, hata kama ni kwa manufaa ya ofisi husika, haupo.
Kingine alichoshuhudia ni jinsi ofisi za mabosi hao zilivyosheheni samani za gharama kubwa. Japo rafiki yangu huyo ni mmoja wa mameneja wachache Watanzania hapa Uingereza, alibaki mdomo wazi kuona sofa, televisheni na vikorombwezo vingine vya thamani ya juu katika takriban kila ofisi ya bosi aliyemtembelea. Alieleza kuwa inaonekana kama ni fasheni fulani kwa kila kiongozi katika taasisi kuhakikisha ofisi yake ni kama Ikulu ndogo kutokana na kusheheni samani za gharama na vitu vingine vya gharama kubwa.
Kadhalika, licha ya wengi wa marafiki zake hao wenye nyadhifa kumjulisha kuwa wanalipwa mishahara minono, walionekana kutumia muda mfupi ofisini, huku katika muda huo mfupi wakiwa ‘bize’ na masuala binafsi kuliko ya kiofisi. Anasema baada ya maongezi ya takriban nusu saa katika ofisi ya kigogo fulani, alijisikia kama anachukua muda muhimu wa kigogo huyo na hivyo kuamua kuaga. Kwa mshangao, kigogo huyo alimlazimisha waendelee na maongezi huku akidai hana jambo muhimu la kufanya ilhali taasisi anayoiongoza inalalamikiwa na wananchi kwa utendaji kazi kwa 'kasi ya konokono.'
Kuhusu ufisadi, alinihakikishia kuwa umekuwa ni kama utamaduni muhimu katika taasisi nyingi (angalau alizozitembelea huko nyumbani). Alinipa mfano wa ofisa mmoja mwandamizi katika taasisi moja ya umma ambaye amepangishiwa nyumba na taasisi hiyo na analipiwa dola 1,500 za Marekani (sina hakika ni kwa mwezi au kwa mwaka). Kichekesho ni kwamba yeye ndio mmiliki wa nyumba hiyo. Kwa hiyo licha ya kukaa bure katika nyumba anayoimiliki bado analipwa kodi ambayo ni mamilioni ya shilingi za Kitanzania.
Lakini wakati alishuhudia baadhi ya Watanzania wenzetu wanaoishi maisha ambayo hata kwa sie huku Uingereza ni ya kufikirika tu, kuna hali tofauti kabisa aliyoshuhudia hapo hapo jijini Dar es Salaam. Alinieleza kuwa katika baadhi ya maeneo aliyoyaita ya 'uswahilini' alishuhudia kilo ya sukari ikiuzwa kwa vijiko ili wananchi wasio na uwezo wamudu kununua ‘vijiko’ kadhaa kwa ajili ya chai. Binafsi, nilishawahi kusikia taarifa kama hiyo kabla kuja huku lakini sikupata fursa ya kushuhudia bayana.
Kwa mujibu wa maelezo ya rafiki yangu huyo, kuna baadhi ya familia 'uswahilini' jijini Dar es Salaam zinaishi katika chumba kimoja, ambapo baba, mama na watoto hawana faragha yoyote. Kadhalika, alieleza kuwa katika maeneo hayo ni jambo la kawaida kwa binti kuondoka 'kwenda kutafuta hela' na wazazi hawana kizuizi kwani bila hivyo siku inaweza kupita bila 'mkono kwenda kinywani.'
Kufikia hapa, ninapenda kukuomba samahani msomaji mpendwa kwa 'simulizi' hii ndefu. Lakini nimekusudia kuifanya mada ya makala hii ili angalau iibue tafakuri kuhusu mwelekeo wa jamii yetu na hatma ya taifa letu. Katika maelezo ya rafiki yangu, kitu kimoja kilicho bayana ni pengo kubwa kati ya walio nacho na wasio nacho (nafasi hairuhusu kuelezea uzoefu wa rafiki yangu kuhusu 'vijana wenye utajiri wa ajabu' ilhali shughuli wanazofanya hazieleweki).
Pengo hilo linachangia sana hali ya 'who cares' kwani kimsingi kwa wenye uwezo, mtizamo ni 'nani anajali ilimradi mie nile kama mbuzi ninayekula kwa urefu wa kamba yangu?' Na kwa walalahoi nao, mtizamo ni huo huo wa 'nani anajali kama wanafilisi nchi yetu ilhali nimemudu kupeleka mkono kinywani?'
Kuna tatizo jingine ambalo niliwahi kulizungumzia katika moja ya makala zangu huko nyuma; upungufu wa tabaka la kati unaochangia kukwamisha jitihada za kulisaidia au kulikomboa tabaka la walalahoi au kupambana (angalau kwa njia za amani) na tabaka la vigogo ili angalau kujenga jamii yenye usawa. Kwa tabaka la kati (ninatambua kuna wanaohoji kama kweli Tanzania yetu ina tabaka hilo), wengi wa waliomo humo wanatamani kuwamo ndani ya tabaka la vigogo na pale matamanio hayo yanapokuwa magumu basi wanajifariji kwa kuishi kama vigogo. Mfano mwepesi ni wababaishaji tunaowashuhudia wakituza maelfu ya shilingi kwenye dansi au sherehe ilhali hali zao binafsi kiuchumi ni taabani.
Na kama kuna kasumba ‘kongwe’ kwa tabaka hili, au pengine 'ugonjwa' unaosumbua Watanzania wengi ni kupenda sifa zisizo na msingi. Si jambo la ajabu kushuhudia mtu mwenye kipato cha wastani tu akijihangaisha kuishi 'maisha ya maonyesho' kwa minajili tu ya kupata sifa mtaani. Na baadhi ya 'mabishoo' hawa ni watu wasio na msaada wa familia na jamii hususan katika maeneo yao ya asili. Sasa ni wazi kuwa ni vigumu kwa ‘kizazi hiki cha wapenda sifa' kuwa na mchango wowote kuunganisha nguvu na tabaka la walalahoi kulibana tabaka la vigogo kujenga jamii iliyo sawa.
Nimalizie makala hii kwa kukuhamasisha wewe msomaji wa makala hii kufikiria zaidi ya maslahi yako binafsi. Msingi wa maendeleo ya nchi kama hapa Uingereza ulijengwa na vizazi vilivyoishi miongo, kama si karne, kadhaa zilizopita. Je, tunapata fursa ya kutafakari Tanzania yetu itakuwaje angalau miaka 50 ijayo? Tukumbuke kuwa pasipo jitihada za makusudi kubadili mwenendo wa mambo huko nyumbani, basi hatutokuwa na jinsi ya kuzuia wajukuu zetu kuyashambulia makaburi yetu kwa hasira huku wakishangaa jinsi tulivyowaachia nchi iliyo tupu kwa raslimali na jamii iliyo tupu kimaadili.
INAWEZEKANA, TIMIZA WAJIBU WAKO

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.