14 Nov 2010

Image and video hosting by TinyPic
The man himself.The Haymaker.A professional KO (Knock Out) Artist.A handsome assassin

Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic
David Haye akitoa kichapo cha nguvu

Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic
Image and video hosting by TinyPic

Image and video hosting by TinyPic

Machampioni wa zamani.Lennox Lewis (kushoto) na Frank Bruno.Wote ni Waingereza
Picha kwa hisani ya magazeti ya The Guardian na The Daily Mail

12 Nov 2010


Raymond Kaminyoge
TANGU Machi mwaka jana alipostaafishwa kazi na Rais Jakaya Kikwete, akiwa Mkuu wa Wilaya ya Mbalali, Mbeya, Hawa Ngulume amekuwa haonekani hadharani wala kusikika kwenye vyombo vya habari kama tulivyomzoea.

Tunakumbuka jinsi alivyoendesha operesheni ya kuwaondoa wafugaji katika Bonde la Ihefu wilayani humo na kusababisha habari zake kutawala kwenye vyombo vya habari na kusababisha malumbano makali kati ya wafugaji na wanamazingira.

Tunakumbuka pia alivyoendesha operesheni hiyo kwa yeye mwenyewe kutembea kwa miguu akisindikiza ng’ombe kuondoka kwenye bonde hilo hali iliyomfanya achukiwe na wafugaji hao lakini akapendwa na wanamazingira.

Tunashuhudia hivi sasa baada ya kuondoka kwa wafugaji kwenye bonde hilo, hali mazingira ni shwali kwani ukijani na uoto wa asili umeanza kurejea katika bonde hilo.

Hayo aliyafanya akiwa mkuu wa wilaya ya Mbalali kabla hajastaafishwa na kumpisha mwenzake Luteni Cosmas Kayombo.

Hayo yote yanakumbukwa na Ngulume, ambaye hivi sasa yuko katika hali mbaya kiafya nyumbani kwake Goba Kinzudi, jijini Dar es Salaam akisumbuliwa na maradhi ya vichomi na mapafu.

Hata hivyo, bado madaktari hawajathibitisha ni nini hasa kinachomsumbua kutokana na kukosekana kwa kipimo mbadala cha kupima kansa ya mapafu.

Mwananchi lilifika nyumbani kwake na aliamua kueleza yaliyokuwa moyoni mwake: “Nimeona bora nitumie chombo cha habari kufikisha ujumbe wa ugonjwa kabla sijafa.”

Anaongeza: “Kwa miezi mitatu sasa niko hoi kitandani, siwezi kutembea bila kusaidiwa, naiomba serikali inisaidie niweze kwenda India ambako kuna vipimo na tiba ya maradhi yanayonisumbua.”

Anasema ameamua kutumia gazeti hili ili kufikisha ujumbe kwa serikali na CCM kuhusu maradhi yanayomsumbua baada ya njia nyingine kushindikana.

“Nilipeleka taarifa kwenye chama changu kwamba naumwa nahitaji msaada, lakini sikujibiwa, pia nimefanya juhudi za kutaka kumwona Waziri Mkuu ili anisaidie lakini juhudi zangu hazikuzaa matunda, nimeamua nitumie chombo cha habari kabla sijafikwa na mauti,” anasema.

Ngulume ambaye ni kada maarufu wa CCM aliyetumikia nafasi ya ukuu wa wilaya kwa miaka 18, anasema maradhi yanayomsumbua yalianza baada ya kumalizika kwa mchakato wa kura za maoni za chama hicho.

Anasema aliomba ridhaa ya chama hicho kimsimamishe kuwa mgombea ubunge katika Jimbo la Singida Mjini lakini hakufanikiwa.

“Katika mchakato ule, Mohammed Dewji alishinda na mimi nikawa mshindi wa pili, niliporudi Dar es Salaam nikaanza kujiandaa kwenda kumpigia debe Dewji, kama ulivyo utaratibu wa chama chetu, ndipo nikaanza kuumwa ghafla,” anasema na kuongeza:

“Nilipenda kushiriki kwenye kampeni ili kuwasaidia wagombea mbalimbali wa chama changu lakini anadhani Mungu hakupenda nifanye hivyo.”

Ngulume ambaye amewahi kuwa mkuu wa wilaya mbalimbali zikiwemo za Kinondoni, Bagamoyo na Kibaha anasema baada ya kuumwa amekuwa akipata tiba za aina tofauti lakini hazijamsaidia.

“Nasikia maumivu makali tumboni, utadhani kuna msumeno unakata viungo vyangu, usiku kucha sipati usingizi ni maumivu tu ndiyo yanayotawala mwili wangu,” anasema.

Anasema amekwishatibiwa kwenye Hospitali za Lugalo, Ocean Road na Imtu zote za Dar es Salaam lakini mbali ya kutopata nafuu, hali yake inazidi kuwa mbaya siku hadi siku.

“Katika hospitali ya Ocean Road nilitakiwa kupima kama mapafu yana maji ili kuthibitisha kama ni kansa ya mapafu lakini kipimo kilichopo kinatakiwa kukaa katika kinywa nami sina pumzi, hivyo ikashindikana kupima,” anasema.

Anaongeza kuwa hadi sasa hawezi kuweka wazi kuhusu maradhi yanayomsumbua kwa vile vipimo mbadala ya vile vya kuwekwa katika kinywa vinapatikana nje ya nchi.

“Ndiyo maana naomba msaada wa kwenda kutibiwa nje kwani nikipimwa ndipo naweza kupata tiba ya uhakika,” anasema kwa taabu.

Anasema katika kuhangaika kutafuta tiba aliwahi kwenda katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili lakini cha kushangaza alikaa kuanzia saa 8.00 mchana hadi saa 11.00 jioni bila kuhudumiwa.

“Ndipo mtu mmoja anayenifahamu alipopita nilipoketi akanisalimia kwa kuniita mheshimiwa. Muuguzi mmoja jina ninalihifadhi akaja kutaka kunihudumia, nikamwambia ina maana siwezi kuhudumiwa hadi niwe mheshimiwa? Nikaondoka kwa hasira nikakataa kuhudumiwa,” anasema.

Siku moja baada ya kuzungumza na gazeti hilo, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (Tamisemi) aliyokuwa akifanya kazi chini yake ilitoa tamko la kusimamia matibabu yake nje ya nchi.

Ujumbe wa maofisa wa Tamisemi ulifika nyumbani kwa mkuu huyo wa zamani wa wilaya kumjulia hali. Hatua hiyo imekuwa faraja kwa Ngulume ambaye anasema ingawa bado ana maumivu makali, amefurahi kwani kuna maofisa kutoka Tamisemi waliomtembelea na kumpa matumaini kwamba huenda akaenda nje kutibiwa.

“Baada ya gazeti lenu kuandika habari zangu, ujumbe wa Tamisemi umefika nyumbani kwangu kuniangalia na kuniahidi kwamba utafanya mipango kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ili niweze kwenda nje kutibiwa,” alisema.

Alisema mbali na ujumbe huo, watu wengi ambao hawakuwa na taarifa zake, wameanza kumtembelea na wengine kumpigia simu wakimuombea kwa Mungu ili aweze kupona maradhi yanayomsumbua.

“Nawashukuru waandishi wa mwananchi, kwani nyie ndiyo mlioujulisha umma kuhusu hali ya afya yangu, ninaomba kwa Mungu usiku kucha ili niweze kufanikiwa kutibiwa kwani maumivu ninayoyapata ni makali.

CHANZO: Mwananchi


UPDATE: Soma "utetezi" wa serikali HAPA

10 Nov 2010


Muungwana mmoja amenitumia comment ambayo kwa hakika imenigusa sana.Naomba niinukuu
Mbona umekatisha mijadala ya kuendeleza nchi ghafla mno. nilitegemea utakuwa na tasmini ya matokeo ya uchaguzi lakini umezimika ghafla. Vipi au jamani inakuwaje uchungu na nchi unakuwa kwa muda tu? Au wameshakutishia na wewe?
Naelewa kwanini mzalendo huyu anataka tufanye tathmini ya uchaguzi mkuu ambao wengi wetu tuliupa umuhimu wa kipekee kutokana na mwenendo wa mambo ulivyo huko nyumbani.Baada ya kushuhudia taifa likienda mrama kwa kugubikwa na ufisadi ilionekana ni lazima Watanzania wenye uchungu wa dhati kwa nchi yao wachukue hatua zinazostahili.Na hatua mwafaka ilionekana kuwa ni kuing'oa CCM madarakani.

Mgombea urais kwa tiketi ya Chadema,Dkt Wilbroad Slaa,ameweka bayana msimamo wake kuwa uchaguzi huo ulichakachuliwa.Baadhi ya taasisi zilizotuhumiwa kufanya uchakachuaji huo zimejitokeza hadharani na kukanusha tuhuma hizo.Haihitaji hata cheti cha kozi ya siku 1 ya uchambuzi wa siasa kumaizi kuwa hakuna hata mmoja kati ya wanaotuhumiwa atakiri mchango wake katika kuirejesha CCM madarakani.Wakubali ili waadhibiwe?

Kadhalika,kuna dhana iliyojengeka kuwa katika uhalisia barani Afrika na katika baadhi ya nchi "za dunia ya tatu" sio rahisi kwa chama tawala kushindwa uchaguzi,na ikitokea kimeshindwa basi yayumkinika kuhitimisha kuwa hayo ni matokeo ya uzembe wa chama husika au migogoro ndani ya chama hicho.Hebu chukulia mfano mazingira ya uchaguzi wetu.Vyombo vya dola vilionyesha waziwazi kuipendelea CCM huku watendaji wa taasisi zinazopaswa kuwa huru wakijibidiisha kumlinda mgombea wa chama tawala.Ndio maana haikumtia hofu Mhariri wa Daily News,gazeti linaloendeshwa kwa kodi za walalahoi,kutamka bayana kuwa Dkt Slaa asingeweza kuwa rais hata baada ya miaka mitano.Kujiamini huko hakukutokana na uimara wa CCM bali ndoa ya kifisadi kati ya taasisi za umma na chama hicho tawala.

Tulisikia taarifa kadhaa kuhusu watendaji wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutowatendea haki wagombea wa vyama vya upinzani.Kadhalika,ilifika mahala Msajili wa Vyama vya Siasa akaamua kuweka wazi mahaba yake kwa CCM na kujipachika jukumubla kuitetea hata pale ilipokosea waziwazi.

Sasa unaweza kujiuliza,"kama tulishaona mwenendo wa aina hiyo ie wa kuitengenezea CCM mazingira ya ushindi,kwanini tulijipa matumaini kuwa Dkt Slaa angeibuka mshindi?".Jibu rahisi kwa mtizamo wangu ni kwamba kulikuwa na matumaini kuwa sauti kubwa ya umma ingeweza kukwaza jitihada zozote za uchakachuaji.Au hata kama jitihada hizo zingefanyika basi zingezidiwa nguvu na sauti hiyo ya umma.

Naomba kukiri hadharani kuwa hofu yangu kubwa haikuwa kwenye mikakati ya kundi dogo lakini lenye nguvu kubwa la mafisadi bali MTAJI MKUU WA CCM yaani umasikini wa Watanzania walio wengi.CCM inategemea sana masikini na hata matokeo "halali" yanathibitisha hilo ambapo maeneo yaliyogubikwa na umasikini ndio yaliyoipa CCM kura nyingi.Huu ni uhusiano ambao kitaaluma unaweza kuelezwa kama wa mnyanyasaji na mnyanywasaji (abuser-abused relationship).Mnyanyasaji anawekeza nguvu nyingi kumwaminisha mnyanyaswaji kuwa pasipo uwepo wake (mnyanyasaji) basi mnyanyaswaji hatakuwa na maisha.Ndio hadithi za amani na utulivu,umoja wa kitaifa,mshikamano,na madude mengine kama hayo.

Kitaaluma,mnyanyaswaji anaweza kufikia mahala akawa anaskia raha kunyanyaswa (punch drunk).Ni kama hali ya kuzowea makonde kwa bondia.Hakuna maelezo mengine mwafaka ya kuelezea namna watu wanaoamka wakiwa hawajui siku iyaisha vipi,wanaotembea maili kadhaa kusaka maji safi japo wafadhili wanamwaga fedha za miradi ya maji,wanaoshinda juani kutwa nzima na kulala vibambazani wakiuza peremende lakini bado wanaandamwa na jeshi la mgambo huku polisi wakiwawinda wawabambikizie kesi,wanaokwenda mahospitalini na kuambulia matibabu hewa kwa vile hakuna madawa,watu wenye watoto ambao makalio yanaota sugu kwa kukaa sakafuni mashuleni,watu ambao haki zao hazipatikani bila kutoa "kitu kidogo" kisha watu haohao wakipigie kura chama kinachostawisha mateso yao.

Na kwa waliodhani akina sie tuliokuwa tukipiga kelele za nguvu kutaka CCM iondoke tulikuwa na chuki binafsi basi matukio mawili yaliyojiri hata masaa 72 hayajapita baada ya CCM kurejea madarakani yanapaswa kuwafumbua macho.Tukio la kwanza ni la mtuhumiwa wa ufisadi wa rada,Mzee wa Vijisenti Andrew Chenge kuchukua fomu ya kugombea Uspika kisha kufanya press conference iliyojaa ngebe,nyodo na dharau kwa wote wanaokerwa na ufisadi.Binafsi,naamini kuwa Chenge katumwa na kundi flani linalotaka kuifakamia keki ya taifa kwa kasi ya marathon hasa kwa vile wanaelewa kuwa Awamu hii ya Tano inaweza kuwa ni lala salama.Chenge ameonyesha bayana kuwa anataka kuwa Spika ili kusafisha majina ya "waliosingiziwa kuwa mafisadi".

Lakini kubwa zaidi ni hisia zangu kuwa Chenge ana baraka kamili za uongozi wa juu wa CCM ikiwa ni pamoja na Mwenyekiti Jakaya Kikwete.Si bado tunakumbuka jinsi Kikwete alivyokwenda jimboni kwa Chenge kumpigia debe na kisha akatetea uamuzi wake wa kuwapigia debe watuhumiwa wa ufisadi kwa kudai kuwa kinachowakabili ni tuhuma tu.Kama tuhuma si tatizo mbona Bashe aliondolewa kwenye mchakato wa mchujo wa kupata wagombea ubunge kwa tiketi ya CCM kwa tuhuma kuwa sio raia wa Tanzania?Kwahiyo tuhuma kwa Chenge,Mramba,nk zinapaswa kubaki tuhuma tu lakini kwa wengine tuhuma ni sawa na hukumu!

Na kwa wanaidhani Chenge anafanya utani mbaya ( a bad joke) basi labda hawaielewi CCM vizuri.Chenge anaweza kabisa kupitishwa katika mfumo wa "kidemokrasia" wa CCM.Yea,kama ameendelea kuongoza kamati ya maadili ya chama hicho na kupitishwa kugombea ubunge (na kushinda) iweje basi kuukwaa uspika liwe suala gumu?Nguvu anayo,sababu anazo,sapoti anayo na VIJISENTI anavyo.Kipi cha kumzuwia kumrithi Samuel Sitta?

Tukio la pili linahisiana na hilo la kwanza ambapo Taasisi ya Kuzuwia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imekurupuka na kudai kuwa Chenge alishasafishwa katika tuhuma za ufisadi wa rada.Yaleyale ya kuisafisha Richmond japo angalau katika ishu ya Richmond serikali ya Kikwete ilikuwa na umri wa zaidi ya mwaka madarakani.Safari hii vimbwanga vimeanza hata kabla ya wiki kumalizika tangu iingie madarakani!Maumivu ya kichwa huanza polepole...

Na kwa kuthibitisha kuwa kura za kuirejesha CCM madarakani zilikuwa kura za kuubariki ufisadi,Ubalozi wa Uingereza umeishushua TAKUKURU kwa kutoa ufafanuzi kuhusu suala la ufisadi wa rada.Sijui nani ameipa TAKUKURU madaraka ya kusafisha watuhumiwa lakini hata sie tusio na uelewa mkubwa wa masuala ya sheria tunafahamu kuwa jukumu la kuhukumu ni la mahakama.Badala ya taasisi hiyo kumpeleka Chenge mahakamani ili kama kusafishwa asafishwe huku,yenyewe imekurupuka na utetezi wake wa kifisadi pasipo hoja za msingi.Hii yote ni katika kuandaa mazingira mazuri kwa Chenge kuwa Spika wa Bunge jipya.

Nitaendelea na tathmini yangu kadri siku zinavyosonga mbele.Najua kuna mengi tu ya kuyazungumzia hasa tukizingatia mazingaombwe yaliyotawala Awamu iliyopita hivyo ni suala la muda tu kabla hayajajiri mengine mengi ya kuwasuta wale wote waliotarajia miujiza kutoka kwa CCM.

6 Nov 2010


Urban Pulse Inawaletea video fupi kuhusu ziara ya Diamond hapa UK kwa ajili ya kuchangia vita dhidi ya Malaria. Tarehe 03.11.2010 Timu nzima Ya Urban Puse ikiwa na Diamond walipata fursa ya Kutembelea Ubalozi wa Tanzania kwa ajili ya kumtambulisha Diamond na kutoa shukrani.



Urban Tour itaanza Rasmi jumamosi tarehe 6.11.10 Milton keynes Club Opus ikifuatana na Croydon London tarehe 12.11.10


Asante sana,

Urban Pulse



Picha zote hapo juu ni za mtu mmoja.Alipanda ndege huko Hong Kong akiwa "kibabu" na kuteremka Kanada akiwa kijana.Actually,huyu ni kijana halisi lakini alijivika kinyago na kuonekana kikongwe,lengo lake likiwa kuingia nchini Kanada kuomba ukimbizi.


4 Nov 2010


Scores of iPhone users were late to work on Monday, after a bug in the software meant the device's alarm clock feature failed to adjust to Daylight Saving Time. Skip related content

Hundreds of angry comments were posted on the social networking website Twitter about the glitch on the Apple device, which occured even though the rest of the phone's features updated the time automatically.

"Well done Apple - you've made me decide I need to use a proper alarm clock rather than relying on my iPhone," one user tweeted.

"Stupid iPhone alarm clock went off an hour late. What a great start to the week," said another.

Australian iPhone users experienced similar problems three weeks ago, although alarms went off an hour early there rather than an hour late.

Apple said at the time that a software patch was being developed to resolve the issue. The technology giant has not yet issued an official response to the British version of the glitch.

The popular gadget has suffered a turbulent year. The latest iPhone 4 model has been blighted by problems with its antennae, proximity sensor and security system.

The latest fault can apparently be avoided by using one-off alarms instead of pre-set daily wake-up calls.


Baada ya kutua na kutulia ndani ya UK Diamond alifanikiwa kufanya promo pamoja na kuongea na fans wake





asante

Urban Pulse creative

3 Nov 2010

MGOMBEA urais kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo, (Chadema), Dk Willibrod Slaa amesema, atayakataa matokeo ya urais yatakayotangazwa na Tume ya Uchaguzi (NEC) kwa kuwa kumefanyika wizi mkubwa wa kura.Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Dk Slaa alisema, kama NEC inaitakia mema nchi hii, ifute matokeo yote ya urais na uchaguzi urudiwe upya.

Dk Slaa ambaye pia ni Katibu Mkuu wa chama hicho, alisema wamekuwa wakifuatilia matokeo ya nchi nzima kwa umakini mkubwa na wamegundua kuna wizi mkubwa wa kura kwenye nafasi za urais na ubunge.

"Kuna uchakachuaji mkubwa wa kura na kazi hiyo inafanywa na usalama wa taifa,"alisema Dk Slaa

Chanzo: Mwananchi
ENDELEA KUFUAtILIA BLOGUNI HAPA



Habari za kuthibitisha kutoka Urban Pulse zinathibitisha kuwa Msanii Diamond tayari katua Ndani ya UK tayari kwa ajili ya kukamua show ya Urban Tour kwa ajili ya kuchangia kupigana vita dhidi ya Malaria. Show yake ya kwanza itafanyika katika Mji wa Milton keynes Jumamosi hii tarehe 6.11.10 ndani Ya Club OPUSPRICE  

Price £10.00 BEFORE MIDNIGHT MORE AFTER
VIP £20.00

WOTE MWAKARIBISHWA,

URBAN PULSE CREATIVE MEDIA

Promo

30 Oct 2010



Ndugu Watanzania wenzangu wote kwa ujumla mtakaosoma ujumbe huu, Salaam toka Mbeya Vijijini, ndio tumeanza mikutano midogo ya kufunga kazi asubuhi hii na tutahitimisha baadaye.

Ninashukuru sana kwa maneno ya heri kwa siku yangu ya kuzaliwa hapo jana na ningekuwa sina shukrani kama ningeacha ipite bila kusema asante kwa maneno mema mliyonipatia humu na kwenye facebook na hata waliopata nafasi kwa njia ya simu. Ninawashukuru vile vile kwa mashauri mbalimbali, na pia kwa sala na dua zenu.

Ninashukuru sana na ninaona fahari kuwa ni mwanachama mwenzenu.

Kampeni zote zinaisha leo na kesho ni siku ya Uchaguzi Mkuu kama mnavyofahamu. Kwa upande wangu nimetembelea karibu maeneo yote ya nchi yetu kubwa, nimekutana na watu mbalimbali na nimeona mengi. Nimeona mengi yenye kutia matumaini na faraja na nimena mengine ya kuhuzunisha na kukatisha tamaa. Yote kwa ujumla yake yamenipa picha ya kuelewa zaidi Taifa letu hasa kuhusu mafanikio tuliyoyapata mpaka hivi sasa na changamoto tulizonazo.

Ninaelewa vizuri zaidi sasa kupitia mang’amuzi binafsi hali ya Taifa letu ilivyo na ya kwamba ni lazima tubadili mwendo na huko tunakokwenda maana tutafika mahali ambapo tutashindwa hata kujiuliza tulifikaje. Watu makini hawawezi kuendelea na njia ambayo wanajua wamepotea. Kuendelea kung’ang’ania kwenda wakati mnajua mmeshapotea ni kutukuza kiburi cha kujiona. Taifa letu limepotea njia na hata kama tukijitahidi kwa nyimbo na masimulizi mbalimbali kuhalalisha huko tunakokwenda bado tutakuwa tumepotea.

Ni kwa sababu hiyo nilipoombwa kugombea Urais nilitambua uzito wa mzigo huu mkubwa kwani utahusiana moja kwa moja na kubadilisha mwelekeo wa taifa letu na kuanza kutengeneza pale palihorabiwa, kuinua kilichoanguka na kumwagilia kilichoanza kunyauka. Hili linahitaji mawazo mapya, uthubutu wa kiuongozi na mtazamo mpya wa nini Taifa letu linahitaji. Ndugu zangu, Taifa letu linahitaji mabadiliko makubwa ili tuweze kujipa sisi wenyewe na watoto wetu nafasi ya kuweza kufanikiwa huko mbeleni.

Mabadiliko haya siyo mabadiliko ya mapambo yaani kuhamimisha maua na vitambaa sebuleni wakati nyumba inanuka na nichafu. Wote mliosikiliza au kumwangalia mgombea mwenzangu jana ni wazi hana ahadi ya mabadiliko yoyote makubwa isipokuwa mwendelezo wa yale yale yaliyotufikisha hapa. Ni kutokana na hilo natambua kuwa kura ya kesho siyo kura ya kawaida; siyo kura kama ya 2005 au ya miaka kabla yake.

Kura ya kesho ni kura ya kuchagua kuendelea na vile tulivyo kwa miaka mitano ijayo au kubadilika ili tuanze upya kwa njia sahihi na kwenda ambako sote tunakujua tunataka kwenda. Ninaamini tunachohitaji ni mabadiliko yatakayoanzisha mwamko wa kuanza kulijenga upya taifa letu. Hili ndilo lililonifanya nikubali pale Chama changu kiliponiomba ninyanyue bendera ya Chadema kwenye uchaguzi huu katika nafasi ya Urais.

Naweza kuwaahidi mengi na kwa maneno matamu ya kila aina. Hata hivyo ninawaahidi kitu kimoja kwa uhakika wa asilimia 100. Mkinichagua kuwa Rais wenu na mkiwashawishi ndugu, jamaa na marafiki zenu kufanya hivyo nami nikachaguliwa, nitawapatia uongozi ambao utaifanya miaka 49 iliyopita kuwa ni ya masimulizi ya njozi za jinamizi kwani nitaongoza timu ya watu ambao watakuwa wamejitokea muda, elimu, ujuzi na vipya vyao katika kujenga taifa letu upya. Katika miaka mitano ijayo tutafanya mambo ambayo CCM na utawala wake imeshindwa kufanya kwa karibu miaka hamsini.

Tutawapa nafasi Watanzania hatimaye nao wafurahia matunda ya uhuru wao na vile vile kuweza kuanza kujenga Taifa la kisasa ambalo litakuwa ni tamanio nakinara cha mabadiliko ya kiutawala, kiuchumi na kiutendaji katika Bara letu. Tuna uwezo, tuna sababu na tuko tayari kuwatumikia.

Naomba sana kura zenu hapo kesho ili niwe Rais wenu katika awamu ya tano. Kura yako ina nguvu ya kubadilisha mwelekeo wa taifa letu. Usiuze, usiache kuitumia na pale utakapoitumia itumie kwangu, kwa wagombea Ubunge Chadema na wagombea wetu wa Udiwani ili tuweze kuhakikisha yote tuliyowaahidi tutayatimiza na zaidi.

Msiwe na shaka, hata toka Ikulu nitaendelea kuwa mwanachama mwaminifu wa mitandao hii na kuwapa taarifa mbalimbali moja kwa moja na kujibu maswali mtakayokuwa nayo kuhusu serikali yenu pale inaponipasa mimi kutolea kauli. Asanteni!!


Mungu Ibariki Tanzania Mungu Ibariki Afrika.


DR W P SLAA - MGOMBEA WA URAISI CHADEMA

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.