29 Jan 2009


HEBU SOMA KWANZA HABARI IFUATAYO KISHA TUIJADILI PAMOJA

MKURUGENZI wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Emmanuel ole Naiko, amesema neno ufisadi linawatisha wawekezaji, hivyo kuwataka wananchi kulitumia kwa umakini huku
wakiweka uzalendo mbele.

Alisema wakati taratibu za kupambana na rushwa zikiendelea, kipaumbele kielekezwe kwenye uchumi na maendeleo kwa ujumla ili kulikwamua taifa, kwani kiwango cha rushwa kilichopo si kama kilichopo katika nchi zilizoendelea.

Naiko alisema hayo jana katika mahojiano maalumu na Tanzania Daima, yaliyofanyika katika ofisi za TIC, jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi huyo alisema hakuna shaka kwamba rushwa na uwekezaji, haviendi pamoja lakini ni vema suala hili likachukuliwa kwa umakini na kutanguliza uzalendo kwa masilahi ya taifa.

“Tunatakiwa tuwe na uzalendo pale penye sifa mbaya, tulichukulie kwa umakini ili tusiendelee kulijengea sifa mbaya taifa letu. Tuziache taratibu na sheria zetu zifanye kazi, ikiwemo kuwapeleka mahakamani watuhumiwa,” alisema.

Alisema Tanzania haiongozi kwa rushwa lakini inaonekana hivyo kutokana na msimamo wa serikali kuweka wazi masuala ya rushwa. Akitolea mfano wa meya aliyeuza kiti cha useneta huko Illinois, nchini Marekani, Ole Naiko alisema hali hiyo inaashiria ni kwa jinsi gani kulivyo na rushwa katika nchi tajiri kuliko zile maskini.

“Sisi tuna rushwa ndogo ndogo, hatuwezi kuongoza kwa rushwa, nchi tajiri ndizo zinazoongoza kwa rushwa. Kwanza tuna taasisi za kupambana na rushwa na tunayaweka haya masuala wazi, wenyewe kamwe hawawezi, kwani hawataki nchi zao
zionekane mbaya,” alisisitiza. Kutokana na hali hiyo, Mkurugenzi aliwataka Watanzania kulifikiria taifa lao wakati likipambana na rushwa na kusisitiza kuwa wananchi wajadili jinsi ya kuliletea taifa maendeleo.

Akizungumzia mafanikio ya mkutano wa Sullivan uliofanyika mwaka jana, alisema huandaliwa kwa lengo la kuwaunganisha Wamarekani na Waafrika katika kujadili mustakabali wa jinsi ya kuondokana na hali ya umaskini inayowakabili.

Pamoja na hilo, alikiri kwamba mafanikio yameonekana hasa kwa wawekezaji wa Kimarekani, kwani mkutano huo umeifanya Marekani itoke nafasi ya nane hadi ya nne kwa uwekezaji nchini, ikifuatiwa na nchi za Uingereza, Afrika Kusini na Kenya.

Kuhusu safari za Rais Jakaya Kikwete nchini Marekani, Naiko alisema zimewawezesha Wamarekani kuifahamu vema Tanzania, hivyo kuvutika kuwekeza zaidi. Alisema kwa sasa kituo chake kina mpango mahususi wa kutumia balozi zake katika kuitangaza Tanzania, ikiwa ni pamoja na kuweka balozi zake katika nchi zenye uwezo wa kuwekeza nchini.


HIVI KIPI CHA BUSARA ZAIDI: KUTOPIGA KELELE KUHUSU UFISADI KWA VILE WAKIFANYA HIVYO WATAWATISHA WAWEKEZAJI AU KUPIGA KELELE KWA NGUVU ILI MAFISADI WATOKOMEE NA KISHA KUWAVUTIA WAWEKEZAJI WENGI ZAIDI? HIVI HUYU OLE NAIKO ANATAKA KUJIFANYA HAELEWI KWAMBA MASLAHI YA MTANZANIA YANA UMHIMU ZAIDI KULIKO HAO WAWEKEZAJI (AMBAO MIONGONI MWAO NI MAFISADI VILEVILE)?

MASLAHI YA TAIFA YATALINDWA TU ENDAPO KELELE DHIDI YA MAFISADI ZITAENDELEA KWA NGUVU KUBWA NA KUWASHIRIKISHA WATU KAMA OLE NAIKO NA WALA SIO KWA KUONGEA CHINICHINI KWA KUHOFIA KUWATISHA WAWEKEZAJI.HIVI MAFISADI WAKISHAIFILISI TANZANIA HAO WAWEKEZAJI WATAKUJA KUWEKEZA KWENYE NINI?

TUANGALIE KWA MTIZAMO MWINGINE.HIVI SI KWELI KWAMBA NI VITENDO VYA UFISADI,NA SIO KELELE ZA WANANCHI KUHUSU MATENDO YAO,YANAYOCHAFUA SIFA YA TANZANIA NA HIVYO KUWATISHA WAWEKEZAJI?HUYU JAMAA VIPI?LAKINI SIMSAHNGAI SANA KWA VILE ALISHAWAHI KUCHEMKA HUKO NYUMA ALIPOHUSISHWA NA TUHUMA ZA MATAPELI WA RICHMOND NA AKAKIMBILIA KUDAI KWAMBA ANAFANYIWA HIVYO (KUHUSISHWA) KWA VILE YEYE NI MTU WA MONDULI (KAMA LOWASSA).
MFANO WAKE KWAMBA GAVANA (NA SIO MEYA KAMA ALIVYODAI) WA ILLINOIS,ROD BLAGOJEVICH,KUKABILIWA NA TUHUMA ZA "KUUZA KITI" CHA USENETA INAASHIRIA KUWA RUSHWA NI KUBWA KATIKA NCHI TAJIRI KULIKO MASIKINI UNASHINDWA KUZINGATIA UKWELI KWAMBA RUSHWA NI RUSHWA,IWE MAREKANI AU TANZANIA,TENA PENGINE RUSHWA KATIKA NCHI TAJIRI INAWEZA KUWA NA ATHARI NDOGO KULINGANISHA NA NCHI ZA MASIKINI KWA VILE ANGALAU WENZETU WANA MECHANISM KADHAA ZINAZOWEZA KUM-BANA MTU ALIYEPATA MADARAKA KWA NJIA YA RUSHWA.LA MUHIMU HAPO SIO GAVANA HUYO KUWA KISHIRIO KWAMBA RUSHWA IPO MAREKANI BALI NAMNA WENZETU WANAVYOJITAHIDI KUPAMBANA NAYO.SIJUI SIE TUNA AKINA BLAGO WANGAPI...KUBWA ZAIDI NI KILE WAINGEREZA WANACHOSEMA TWO WRONGS DO NOT MAKE A RIGHT.KUWEPO KWA RUSHWA MAREKANI,AU KWINGINEKO KOKOTE KULE HAKUWEZI KUHALALISHA RUSHWA WALA KUWA SABABU YA SIE KUPUNGUZA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA ETI KWA VILE TU "MBONA HATA KWA WENZETU IPO"!

WAKATI OLE NAIKO ANASEMA (NAMNUKUU) "Sisi tuna rushwa ndogo ndogo....nchi tajiri ndizo zinazoongoza kwa rushwa....wenyewe kamwe hawawezi, kwani hawataki nchi zao zionekane mbaya..." INAELEKEA ANASAHAU KWAMBA HIYO ANAYOITA RUSHWA NDOGO NDOGO (SIJUI KAPATA WAPI KIPIMO CHA KUJUA RUSHWA KUBWA NA NDOGO) INA MADHARA MAKUBWA SANA KWA NCHI MASIKINI KAMA AMBAVYO HIZO RUSHWA KUBWA ZINAVYOWEZA KUWA NA MADHARA KATIKA NCHI TAJIRI.HALAFU MBAONA ANAJICHANGANYA ANAPODAI KUWA NCHI TAJIRI "ZINAZOONGOZA KWA RUSHWA" (KWA MUJIBU WAKE) HAZIWEZI KUWEKA RUSHWA HADHARANI KWA VILE HAZITAKI ZIONEKANE MBAYA LAKINI HAPO HAPO AMETOA MFANO WA HUYO GAVANA WA ILLINOIS!?JE WANGEKUWA HAWATAKI HAYO YAONEKANE YEYE OLE NAIKO NA SIE TULIO NJE YA MAREKANI TUNGEJUAJE?

HALAFU ARGUEMENTS ZA HUYU MHESHIMIWA ZINAWEZA KUWA NA MADHARA KULIKO HICHO ANACHOJARIBU KUTUELEZA.HIVI TUMWELEWEJE ANAPODAI KUWA NCHI TAJIRI ZINAONGOZA KWA RUSHWA,HALAFU WAWEKEZAJI ANAOTAKA TUSIWATISHE KWA NENO UFISADI WANATOKA KWENYE NCHI HIZOHIZO ANAZODAI ZINAONGOZA KWA RUSHWA!!!!ANATAKA TUSIWATISHE ILI WAJE KUENDELEZA RUSHWA TANZANIA?

HOJA YENYE UZITO NI KWAMBA UFISADI SIO TU UNAATHIRI SEKTA YA UWEKEZAJI BALI PIA UNAATHIRI TAIFA LENYEWE AMBALO TUNATAKA KUWAVUTIA WAWEKEZAJI HAO.KWA MWENYE BUSARA ZA KUTOSHA HOJA YA MSINGI NI KUZIDISHA MAPAMBANO DHIDI YA UFISADI NA WALA SIO HOFU KWAMBA NENO MAFISADI LITAWATISHA WAWEKEZAJI.JINGINE LA MUHIMU NI KILE ALICHOSEMA MWENYEKITI MAO KWAMBA NO RESEARCH NO RIGHT TO SPEAK.KUTUHUMU MATAIFA TAJIRI KUWA YANAONGOZA KWA RUSHWA PASIPO KUTOA TAKWIMU ZA KUSAPOTI HOJA HIYO,SIO TU INAWEZA KUWACHUKIZA HAO WAWEKEZAJI KWA VILE WANAWEZA KUDAI WANATUHUMIWA PASIPO SUPPORTING EVIDENCE,BALI PIA KUNAMPUNGUZIA CREDIBILITY MTOA HOJA HASA IKIZINGATIWA KUWA ENEO ANALOZUNGUMZIA NDILO ALILOKABIDHIWA DHAMANA NA TAIFA KULISIMAMIA KWA UMAKINI.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.