Showing posts with label UWEKEZAJI TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label UWEKEZAJI TANZANIA. Show all posts

18 Apr 2011


Mkutano mwingine wa wawekezaji umeanza leo jijini Dar es Salaam.Mkutano huo ni mwendelezo wa mikutano mingine inayopigiwa debe kwa nguvu kuhusiana na umuhimu wa wawekezaji kwa uchumi wetu.

Naamini wengi wet bado tunakumbuka vuguvugu la Mkutano wa Sullivan.Baadaye ukafuatiwa na mkutano mkubwa wa mambo ya uchumi (economic forum).So far,hayo yamebaki kuwa matukio tu ambayo kwa upande mmoja yamewaachia baadhi ya wajanja utajiri wa kutosha baada ya kupewa tenda za chakula,malazi,vifaa,nk huku Watanzania wakiendelea kubaki masikini (na hapo tukiweka kando adha ya usafiri kutokana na barabara kufungwa kwa ajili ya misafara ya waheshimiwa).

Wakati viongozi wetu wakituhadaa na mikutano ya kila mwaka ya wawekezaji,kuna umuhimu wa kufanya uchambuzi wa kina kuhusu suala zima la uwekezaji.Kama uwekezaji mkubwa uliopo hadi sasa hauna manufaa kwa Mtanzania wa kawaida,ni miujiza gani itapelekea wawekezaji wapya walete mabadiliko?

Suala moja la msingi linalopuuzwa na watawala wetu ni ukweli kwamba wawekezaji sio taasisi za hiari za kutuletea maendeleo yetu.Hawa ni wafanyabiashara ambao miaka michache tu iliyopita tuliwaita kila aina ya majina-from watangulizi wa ukoloni to mabeberu.Of course dunian imebadilika,lakini mabadiliko hayo sio yawe at expense of wazawa au wenye nchi.

Tunaingia gharama kubwa kuvutia watu wa aina ya Richmond,Dowans,wezi wa madini huko migodini,na wababaishaji wengine.Wengi wa wanaoitwa wawekezaji wanakuja na briefcase tupu zikiwa na mikataba tupu lakini ikishasainiwa,na baada ya miaka michache wanaondoka wakiwa na mamilioni kwenye akaunti zao-huku wakiacha,kwa upande mmoja, mafisadi wameongeza idadi ya nyumba ndogo zao,mahekalu yao na magari yao ya kifisadi,na upande mwingine walalahoi wakikodolea ardhi yao iliyoachwa mashimo matupu baada ya raslimali yote kuibiwa.

Tunakaribishaje wawekzaji kabla ya kutengeneza sera na sheria mwafaka za kutuwezesha kunufaika na ujio wa wawekezaji hao?Na uwekezaji wa aina ya "kupangisha nyumba kisha mwenye nyumba kulala mtaani" ni uhayawani usiopaswa kuendelea.

Tunafahamishwa wizi unaofanywa na baadhi ya makampuni ya simu ambayo kila baada ya muda flani yanabadili majina ilhali huduma zao mbovu zikiendelea kuwa zile zile za kuchefua.

Tunakaribisha wawekezaji wakati baadhi ya hao waliopo wanapata hadi jeuri ya kuchoma moto wazawa (rejea tukio la Kigamboni)lakini vyombo vya dola vinachelea kuchukua hatua zinazostahili.

Viongozi wetu wanapaswa kuwa makini na kurejea yaliyotokea nchini Afrika Kusini hivi karibuni ambapo wazawa waliamua kuelekeza hasira zao kwa wageni wakiamini kuwa ndio chanzo cha matatizo yao ya kila siku japo ukweli ni kwamba chanzo cha tatizo ni uongozi mbovu wa watawala wa nchi hiyo.

Tumeshuhudia jana baadhi ya wakazi wa Kigamboni wakiamua kupambana na wawekezaji japo kama ilivyo kawaida waliishia kudhibitiwa na polis,na huenda wakafunguliwa mashtaka huku mwekezaji aliyeua akiachwa "anakula kuku kwa mrija".

Nikirejea tukio hilo la Kigamboni,nilifadhaika kusoma tweet ya Mbunge wa jimbo hilo akieleza bila aibu kuwa "maandamano yamekuwa SUPPRESSED na CULPRITS watachukuliwa hatua za kisheria".Huyu ni mwakilishi wa watu haohao waliompoteza mwenzao kwa kuchomwa moto na mwekezaji!

Anyway,ujio wa wawekezaji ni habari njema kwa mafisadi kwani unapanua fursa za kupata teni pasenti na vijizawadi vya likizo huko ughaibuni,huku the so called wawekezaji wakigeuza nchi yetu kuwa shamba la bibi.

12 Apr 2011


Nimekumbana na habari ifuatayo katika gazeti la Tanzania Daima ambapo inaelezwa kuwa mwekezaji mmoja mwenye asili ya Kiasia amemchoma moto mwanamke mmoja kwa kosa la kuingia hotelini mwa mwekezaji husika bila kulipa kiingilio.

Kinachojidhihirisha katika habari husika ni dalili kwamba jeshi la pilisi linasuasua kumtendea haki mwananchi huyo.Nimewasiliana na bloga mwenzangu ambaye pia ni mwandishi mwandamizi wa gazeti moja la jamii huko nyumbani kumwomba tushirikiane kulipigia kele suala hili hadi haki ya mwananchi mwenzetu ipatikane.Kwa sie Watanzania tulio nje tunashuhudia namna raia wa nchi za wenzetu wanavyothaminiwa na sheria zao lakini kwetu ni hadithi tofauti hususan linapokuja suala la hao wanaoitwa wawekezaji.

Uwezo wa kifedha isiwe sababu ya kunyanyasa wananchi wasio na uwezo.Natoa wito kwa kila Mtanzania atakayeguswa na habari hii kuchangia kwa namna moja au nyingine kudai haki itendeke na ikiwezekan mwekezaji husika atimuliwe kabisa nchini.Hatuhitaji wababaishaji wanaoifanya nchi yetu kama pori lisilo na sheria.

Habari husika ni hii:

Mwekezaji amchoma moto raia Dar



na Hellen Ngoromera




RAIA wa Kiasia anayehusishwa kumiliki hoteli moja maarufu iliyopo Kigamboni anadaiwa kumjeruhi kwa kumchoma moto mkazi wa Mjimwema, Lila Hussein (25), baada kuingia hotelini hapo bila kulipa kiingilio.

Akizungumza na Tanzania Daima jana, ndugu wa majeruhi huyo, Abdullah Saiwaad,alisema tukio hilo lilitokea Jumamosi majira kati ya saa 5:00 na 6:00 usiku.

Alisema kabla ya kuchomwa moto, Lila ambaye amelazwa wodi namba 7 katika Hospitali ya Temeke akiwa hajitambui, alivuliwa nguo kisha kumwagiwa mafuta ya petroli na kwamba amejeruhiwa vibaya kuanzia sehemu za magotini hadi shingoni.

Alisema chanzo cha tukio hilo ni Lila kuingia kwenye muziki hotelini hapo bila kulipa kiingilio.

“Hali ni tete, Lila yupo hospitali ya Temeke akipigania maisha yake baada ya kuchomwa moto na mhindi ambaye ni mmiliki wa hoteli ya South Beach, ameungua vibaya tunamwomba Mungu anusuru maisha yake,” alisema Saiwaad.

Alisema baadaye aliokolewa na wafanyakazi wawili baada ya kuamua kupeleka taarifa kijijini Mjimwema.

Kutokana na tukio hilo wanakijiji wametishia kuchoma moto hoteli hiyo na kwamba hali hiyo imesababisha mkuu wa kituo cha Kigamboni kupeleka askari wa doria kusimamia usalama hotelini hapo.

Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Davis Misime, alikiri kuwepo kwa taarifa hizo na kuahidi kuzifuatilia kwa kina.

Kwa mujibu wa Misime, usiku askari walipata taarifa kuwa kuna mtu amechomwa moto hotelini hapo ndipo walipokwenda na kumchukua majeruhi na kumpeleka katika kituo cha afya Kigamboni kisha baadaye kupelekwa Temeke.

Hata hivyo, habari zinapasha zaidi kwamba baadaye jioni ya jana, Lila alihamishiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kutokana na hali yake kuwa mbaya.

CHANZO: Tanzania Daima

11 Apr 2009

MAELEZO YA PICHA KUTOKA KATIKA GAZETI LA HABARI LEO YANASOMEKA:

Behewa la mafuta la TRL liliacha njia eneo la Kurasini, Dar es Salaam na kuanguka.Wafanyakazi wa kampuni hiyo walikutwa wakikinga mafuta hayo ili kuyahifadhi katika mapipa chini ya ulinzi mkali wa polisi. (Picha na Yusuf Badi).
NADHANI MWENZANGU PIA UKIANGALIA PICHA HIYO KWA MAKINI UTABAKI UNAJIULIZA KWAMBA HAO WAHINDI WA TRL NI WAWEKEZAJI KWELI AU VIINIMACHO?TALKING OF VIINIMACHO,YAYUMKINIKA KUJIULIZA IWAPO HAWA JAMAA HAWAJAWAROGA HAO WANAONG'ANG'ANIA KUENDELEZA MKATABA WA KIMAZINGAOMBWE NA TRL.KAMA ILIVYO DESTURI YETU YA ZIMAMOTO,TUNASUBIRI WALIKOROGE KWANZA,KISHA WAINGIE MITINI HALAFU KUNYWA TULINYWE SIE!NA HAPA NENO "KULIKOROGA" LINAMAANISHA KU-MESS UP NA MAISHA YA ABIRIA WANAOTEGEMEA USAFIRI WA RELI YA KATI.

5 Mar 2009

Picha kwa hisani ya Mjengwa
MWAKA 2006,MANISPAA YA TEMEKE ILITANGAZA AZMA YAKE YA KULIBORESHA SOKO LA TEMEKE.LAKINI KATIKA HALI YA KUSTAAJABISHA,KUNA TAARIFA KWAMBA SASA SOKO HILO LIMEUZWA KWA MWEKEZAJI.KWA MWENENDO HUU,SI AJABU SIKU YA SIKU MTU AKAAMKA NA KUKUTA MTAA ANAOISHI UMEUZWA KWA MWEKEZAJI.

29 Jan 2009


HEBU SOMA KWANZA HABARI IFUATAYO KISHA TUIJADILI PAMOJA

MKURUGENZI wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Emmanuel ole Naiko, amesema neno ufisadi linawatisha wawekezaji, hivyo kuwataka wananchi kulitumia kwa umakini huku
wakiweka uzalendo mbele.

Alisema wakati taratibu za kupambana na rushwa zikiendelea, kipaumbele kielekezwe kwenye uchumi na maendeleo kwa ujumla ili kulikwamua taifa, kwani kiwango cha rushwa kilichopo si kama kilichopo katika nchi zilizoendelea.

Naiko alisema hayo jana katika mahojiano maalumu na Tanzania Daima, yaliyofanyika katika ofisi za TIC, jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi huyo alisema hakuna shaka kwamba rushwa na uwekezaji, haviendi pamoja lakini ni vema suala hili likachukuliwa kwa umakini na kutanguliza uzalendo kwa masilahi ya taifa.

“Tunatakiwa tuwe na uzalendo pale penye sifa mbaya, tulichukulie kwa umakini ili tusiendelee kulijengea sifa mbaya taifa letu. Tuziache taratibu na sheria zetu zifanye kazi, ikiwemo kuwapeleka mahakamani watuhumiwa,” alisema.

Alisema Tanzania haiongozi kwa rushwa lakini inaonekana hivyo kutokana na msimamo wa serikali kuweka wazi masuala ya rushwa. Akitolea mfano wa meya aliyeuza kiti cha useneta huko Illinois, nchini Marekani, Ole Naiko alisema hali hiyo inaashiria ni kwa jinsi gani kulivyo na rushwa katika nchi tajiri kuliko zile maskini.

“Sisi tuna rushwa ndogo ndogo, hatuwezi kuongoza kwa rushwa, nchi tajiri ndizo zinazoongoza kwa rushwa. Kwanza tuna taasisi za kupambana na rushwa na tunayaweka haya masuala wazi, wenyewe kamwe hawawezi, kwani hawataki nchi zao
zionekane mbaya,” alisisitiza. Kutokana na hali hiyo, Mkurugenzi aliwataka Watanzania kulifikiria taifa lao wakati likipambana na rushwa na kusisitiza kuwa wananchi wajadili jinsi ya kuliletea taifa maendeleo.

Akizungumzia mafanikio ya mkutano wa Sullivan uliofanyika mwaka jana, alisema huandaliwa kwa lengo la kuwaunganisha Wamarekani na Waafrika katika kujadili mustakabali wa jinsi ya kuondokana na hali ya umaskini inayowakabili.

Pamoja na hilo, alikiri kwamba mafanikio yameonekana hasa kwa wawekezaji wa Kimarekani, kwani mkutano huo umeifanya Marekani itoke nafasi ya nane hadi ya nne kwa uwekezaji nchini, ikifuatiwa na nchi za Uingereza, Afrika Kusini na Kenya.

Kuhusu safari za Rais Jakaya Kikwete nchini Marekani, Naiko alisema zimewawezesha Wamarekani kuifahamu vema Tanzania, hivyo kuvutika kuwekeza zaidi. Alisema kwa sasa kituo chake kina mpango mahususi wa kutumia balozi zake katika kuitangaza Tanzania, ikiwa ni pamoja na kuweka balozi zake katika nchi zenye uwezo wa kuwekeza nchini.


HIVI KIPI CHA BUSARA ZAIDI: KUTOPIGA KELELE KUHUSU UFISADI KWA VILE WAKIFANYA HIVYO WATAWATISHA WAWEKEZAJI AU KUPIGA KELELE KWA NGUVU ILI MAFISADI WATOKOMEE NA KISHA KUWAVUTIA WAWEKEZAJI WENGI ZAIDI? HIVI HUYU OLE NAIKO ANATAKA KUJIFANYA HAELEWI KWAMBA MASLAHI YA MTANZANIA YANA UMHIMU ZAIDI KULIKO HAO WAWEKEZAJI (AMBAO MIONGONI MWAO NI MAFISADI VILEVILE)?

MASLAHI YA TAIFA YATALINDWA TU ENDAPO KELELE DHIDI YA MAFISADI ZITAENDELEA KWA NGUVU KUBWA NA KUWASHIRIKISHA WATU KAMA OLE NAIKO NA WALA SIO KWA KUONGEA CHINICHINI KWA KUHOFIA KUWATISHA WAWEKEZAJI.HIVI MAFISADI WAKISHAIFILISI TANZANIA HAO WAWEKEZAJI WATAKUJA KUWEKEZA KWENYE NINI?

TUANGALIE KWA MTIZAMO MWINGINE.HIVI SI KWELI KWAMBA NI VITENDO VYA UFISADI,NA SIO KELELE ZA WANANCHI KUHUSU MATENDO YAO,YANAYOCHAFUA SIFA YA TANZANIA NA HIVYO KUWATISHA WAWEKEZAJI?HUYU JAMAA VIPI?LAKINI SIMSAHNGAI SANA KWA VILE ALISHAWAHI KUCHEMKA HUKO NYUMA ALIPOHUSISHWA NA TUHUMA ZA MATAPELI WA RICHMOND NA AKAKIMBILIA KUDAI KWAMBA ANAFANYIWA HIVYO (KUHUSISHWA) KWA VILE YEYE NI MTU WA MONDULI (KAMA LOWASSA).
MFANO WAKE KWAMBA GAVANA (NA SIO MEYA KAMA ALIVYODAI) WA ILLINOIS,ROD BLAGOJEVICH,KUKABILIWA NA TUHUMA ZA "KUUZA KITI" CHA USENETA INAASHIRIA KUWA RUSHWA NI KUBWA KATIKA NCHI TAJIRI KULIKO MASIKINI UNASHINDWA KUZINGATIA UKWELI KWAMBA RUSHWA NI RUSHWA,IWE MAREKANI AU TANZANIA,TENA PENGINE RUSHWA KATIKA NCHI TAJIRI INAWEZA KUWA NA ATHARI NDOGO KULINGANISHA NA NCHI ZA MASIKINI KWA VILE ANGALAU WENZETU WANA MECHANISM KADHAA ZINAZOWEZA KUM-BANA MTU ALIYEPATA MADARAKA KWA NJIA YA RUSHWA.LA MUHIMU HAPO SIO GAVANA HUYO KUWA KISHIRIO KWAMBA RUSHWA IPO MAREKANI BALI NAMNA WENZETU WANAVYOJITAHIDI KUPAMBANA NAYO.SIJUI SIE TUNA AKINA BLAGO WANGAPI...KUBWA ZAIDI NI KILE WAINGEREZA WANACHOSEMA TWO WRONGS DO NOT MAKE A RIGHT.KUWEPO KWA RUSHWA MAREKANI,AU KWINGINEKO KOKOTE KULE HAKUWEZI KUHALALISHA RUSHWA WALA KUWA SABABU YA SIE KUPUNGUZA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA ETI KWA VILE TU "MBONA HATA KWA WENZETU IPO"!

WAKATI OLE NAIKO ANASEMA (NAMNUKUU) "Sisi tuna rushwa ndogo ndogo....nchi tajiri ndizo zinazoongoza kwa rushwa....wenyewe kamwe hawawezi, kwani hawataki nchi zao zionekane mbaya..." INAELEKEA ANASAHAU KWAMBA HIYO ANAYOITA RUSHWA NDOGO NDOGO (SIJUI KAPATA WAPI KIPIMO CHA KUJUA RUSHWA KUBWA NA NDOGO) INA MADHARA MAKUBWA SANA KWA NCHI MASIKINI KAMA AMBAVYO HIZO RUSHWA KUBWA ZINAVYOWEZA KUWA NA MADHARA KATIKA NCHI TAJIRI.HALAFU MBAONA ANAJICHANGANYA ANAPODAI KUWA NCHI TAJIRI "ZINAZOONGOZA KWA RUSHWA" (KWA MUJIBU WAKE) HAZIWEZI KUWEKA RUSHWA HADHARANI KWA VILE HAZITAKI ZIONEKANE MBAYA LAKINI HAPO HAPO AMETOA MFANO WA HUYO GAVANA WA ILLINOIS!?JE WANGEKUWA HAWATAKI HAYO YAONEKANE YEYE OLE NAIKO NA SIE TULIO NJE YA MAREKANI TUNGEJUAJE?

HALAFU ARGUEMENTS ZA HUYU MHESHIMIWA ZINAWEZA KUWA NA MADHARA KULIKO HICHO ANACHOJARIBU KUTUELEZA.HIVI TUMWELEWEJE ANAPODAI KUWA NCHI TAJIRI ZINAONGOZA KWA RUSHWA,HALAFU WAWEKEZAJI ANAOTAKA TUSIWATISHE KWA NENO UFISADI WANATOKA KWENYE NCHI HIZOHIZO ANAZODAI ZINAONGOZA KWA RUSHWA!!!!ANATAKA TUSIWATISHE ILI WAJE KUENDELEZA RUSHWA TANZANIA?

HOJA YENYE UZITO NI KWAMBA UFISADI SIO TU UNAATHIRI SEKTA YA UWEKEZAJI BALI PIA UNAATHIRI TAIFA LENYEWE AMBALO TUNATAKA KUWAVUTIA WAWEKEZAJI HAO.KWA MWENYE BUSARA ZA KUTOSHA HOJA YA MSINGI NI KUZIDISHA MAPAMBANO DHIDI YA UFISADI NA WALA SIO HOFU KWAMBA NENO MAFISADI LITAWATISHA WAWEKEZAJI.JINGINE LA MUHIMU NI KILE ALICHOSEMA MWENYEKITI MAO KWAMBA NO RESEARCH NO RIGHT TO SPEAK.KUTUHUMU MATAIFA TAJIRI KUWA YANAONGOZA KWA RUSHWA PASIPO KUTOA TAKWIMU ZA KUSAPOTI HOJA HIYO,SIO TU INAWEZA KUWACHUKIZA HAO WAWEKEZAJI KWA VILE WANAWEZA KUDAI WANATUHUMIWA PASIPO SUPPORTING EVIDENCE,BALI PIA KUNAMPUNGUZIA CREDIBILITY MTOA HOJA HASA IKIZINGATIWA KUWA ENEO ANALOZUNGUMZIA NDILO ALILOKABIDHIWA DHAMANA NA TAIFA KULISIMAMIA KWA UMAKINI.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.