17 Mar 2010


KLABU ya soka ya Real Madrid ya nchini Hispania jana imemkabidhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete tuzo ya Jezi ya kiungo mshambuliaji wa timu hiyo Critiano Ronaldo. Akizungumza katika hafura hiyo iliyofanyika Ikuru jana Meya wa jiji la Dar es Salaam, Adam Kimbisa ambaye alimukabidhi Rais jezi hiyo kwa niaba ya viongozi wa klabu ya Real Madrid kutokana kutambua mchango wake katika mchezo wa soka.

"Kwa heshima hiyo Klabu hiyo imetoa tuzo Jezi namba tisa inayovaliwa na mchezaji mahiri wa timu hiyo Cristano Ronado," alisema Kimbisa.

Naye Rais Kikweta mara baada ya kupokea tuzo hiyo ameshukuru klabu hiyo ya Real Madrid kwa zawadi hiyo ambayo alisema kuwa ni hesima kubwa kwa Watanzania.

"Nashukuru sana kwa zawadi hii, Madrid ni timu kubwa duniani kutukumbuka sisi Watanzania ni faraja kubwa kwetu.

"Itabidi tutafute sababu mpya ya kuwaalika upya kuja hapa nchini kufutia ili ya awali kushindikana, ni matumani yetu pia tutapata watu ambao watatusaidia kuwaleta," alisema.

Klabu hiyo ya Real Madrid itarajia kufanya ziara yake hapa nchini kwa ajili ya uzinduzi wa Uwanja wa Taifa mwanzoni mwa mwaka juzi lakini kutokana kuchelewa kukamilika kwa ujenzi wa uwanja huo timu hiyo hakuweza kufanya hivyo.

CHANZO: Mwananchi.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.