Showing posts with label JK. Show all posts
Showing posts with label JK. Show all posts

2 Oct 2014

Bado ninakumbuka vizuri maongezi yangu ya mwaka 2005 na mtu mmoja jijini Dar, ambaye sio tu ni mwajiriwa katika taasisi moja nyeti lakini pia ana uelewa mkubwa wa masuala yanayojiri 'nyuma ya pazia' (yaani masuala mbalimbali mazito ambayo kamwe huwezi kuyasikia au kuyaona kwenye vyombo vya habari). Nikiwa huko nyumbani kwa likizo katika kipindi ambacho Tanzania yetu ilikuwa katika harakati za uchaguzi mkuu ambao hatimaye ulimwingiza madarakani Rasi Jakaya Kikwete, mwandamizi huyo alinieleza kwa undani kwanini aliamini JK angeshinda uchaguzi huo kwa ushindi wa kishindo.

Kadhalika, mtu huyo alibashiri kuwa Watanzania watajuta kumwingiza Kikwete Ikulu kwa kile alichokieleza kuwa "mtu huyu hayupo serious kiasi cha kumkabidhi dhamana ya kuongoza nchi hii yenye matatizo kibao." Alikwenda mbali zaidi na kunisimulia masuala kadhaa yaliyojiri katika utawala wa Rais Benjamin Mkapa (ambapo mie nilikuwa nje ya nchi kwa zaidi ya nusu ya awamu ya pili ya utawala wa Mkapa). Alieleza kuwa hali ilikuwa mbaya wakati huo, na laiti JK akiingia madarakani itakuwa mbaya zaidi.

Mtu huyo ameendelea kunijulisha mengi yanayojiri 'nyuma ya pazia,' na hivi karibuni aliniambia kuwa ana uhakika Watzanai wengi watapatwa na mshtuko mkubwa baada ya JK kuondoka madarakani hapo mwakani, pindi watakapopata fursa ya kufahamu jinsi nchi yao ilivyoendeshwa katika kipindi hiki cha miaka 10 (2005-2015). Alidai kwamba kinachofahamika kwa umma ni tone tu la maji kwenye bahari kwani kuna mlolongo wa 'madudu' yanayoendelea lakini nguvu iliyojengwa na mtandao wa JK 1995-2005 inafanya jitihada kubwa kuyadhibiti yasijulikane hadharani.

Lakini sidhani kama kuna Mtanzania anayehitaji kuwa na 'mjuzi wa mambo' kama  huyo jamaa yangu, kufahamu kwamba mwelekeo wa nchi yetu ni shaghalabaghala. Kwa wenye uelewa wa 'kusoma kati ya mistari' (reading between the lines) watabaini kuwa mengi ya yanayojiri huko nyumbani katika medani ya uongozi wa taifa letu ni matokeo ya ombwe kubwa la uongozi wa JK.

Wengi twakumbuka kauli ya Mbunge wa Ubungu kwa tiketi ya Chadema, Mheshimiwa John Mnyika, kuwa 'JK ni dhaifu.' Na kwa hakika watendaji wengi wa serikali ikiwa ni pamoja na mawaziri wake wanautumia vyema udhaifu huo wa bosi wao.

Hebu angalia mfano huu rahisi. Wakati lawama nyingi kuhusu sintofahamu ya hatma ya Katiba Mpya inaelekezwa kwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katika, Samuel Sitta, mtu ambaye hawezi kukwepa lawama katika kuukoroga mchakato huo ni JK mwenyewe. Kana kwamba alilazimishwa kuteua Tume ya Kukusanya Maoni ya Katiba (Tume ya Warioba), JK pasi kujali athri za matendo yake alianzisha upizani wa waziwazi dhidi ya mapendekezo ya Tume hiyo ya Warioba. Mara kadhaa akiwa kama Mweneykiti wa Taifa wa CCM aliweka bayana upinzani wa chama tawala kwa mapendekezo ya Tume hiyo. Lakini yote tisa, kumi ni siku ya uzinduzi wa Bunge Maalum la Katiba ambapo badala ya kuwaunganisha Watanzania, hotuba yake ilipandikiza mbegu ambazo kwa hakika ndizo tunavyna matuonda yake sasa.

Ilipotokea baadhi ya wajumbe wa Bunge hilo kuunda umoja wao wa UKAWA, na hatimaye kususia vikao vya bunge hilo, kauli za kujikanganya za JK hazikusaidia kuleta mwafaka, kwani mara aonekane anayetaka suluhu mara awatupie lawama UKAWA, mara awaombe viongozi wa dini wasaidie kuokoa mchakato huo, mara atumie ubabe kuzima hoja za UKAWA. Kwa kifupi, ukosefu wake wa msimamo wenye kulinda maslahi ya taifa ulitoa fursa kwa kila 'Dick, Toim na Harry' kujiropokea chochote kilichomuijia akilini.

Fast foward hadi hapa tulipo sasa, katika mazingira ya kawaida tu usingetegemea JK aende Marekani TENA kwa wiki mbili ilhali hatma ya Katiba mpya na Bunge Maalum la Katiba ni tata. Tumeshazungumza vya kutosha kuhusu jinsi JK anavyopenda kuzurura nje ya nchi, hususan ziara za Marekani. Kwa wanaofuatilia safari zake watafahamu kuwa alikuwa Marekani hivi majuzi tu kwa siku kibao, lakini hiyo haikumzuwia kwenda tena huko kwa wiki mbili kwa kisingizio cha kuhudhuria kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Je isingewezekana kwenda siku moja kabla ya siku yake ya kutoa hotuba na kisha kurejea nyumbani kushughulikia hatma ya Katiba mpya?

Kituko ni kwamba wakati akiwa ziarani Marekani, alifanya 'safari ndani ya safari' na kuja hapa Uingereza, kabla ya kurejea tena Marekani. Kwa hakika ni vigumu kubashiri maisha ya Rais wetu huyu atakapostaafu mwakani kwani ni wazi kuwa moja ya vitu atakavyovi-miss sana ni hizo safari mfululizo za nje ya nchi. Japo kuwa Rais mstaafu hakutomzuwia kusafiri mfululizo, lakini angalau kwa wakati huo 'hatokuwa na jeuri' ya kuambatana na lundo la watu kwenye misafara yake. Na hatuwezi kujua, huenda Rais ajaye akadhibiti safari za viongozi au viongozi wastaafu nje ya nchi pasipo sababu za msingi.

Ombwe la uongozi wa JK, ukichanganya na mchango wake katika kuukoroga mchakato wa Katiba mpya, ndio moja ya fursa zilizotumiwa kikamilifu na Sitta katika kufanikisha uhuni wa kisiasa/ mzaha wa kidemokrasia unaoendelea huko Dodoma. Kwa lugha nyingine, kiburi, ubishi, nyodo, na kila kisichopendeza kutoka kwa Sitta na uendeshaji wake wa Bunge Maalum la Katiba ni dalili tu za ugonjwa, ilhali chanzo cha ugonjwa huo ni ombwe hilo linalouandama utawala wa JK.

Hivi tuwe wakweli. Laiti JK angemkalisha Sitta kitako kama Waziri wake na ' kumpa darasa la kiutu-uzima' Mwenyekiti huyo wa BMK angeendeleza kufanya madudu tunayoshuhudia? Ni suala jepesi tu la bosi kukaa chini na anayemwongoza, kisha kumwambia bayana kuwa , "No, Mr Sitta, this is wrong." Na hata kama kuna watakaodhani huo ni sawa na udikteta, basi na bora iwe hivyo kwani udikteta kwa maslahi ya umma ni suala linalokubalika.Uzoefu unaonyesha kuwa kumpa mtu uhuru usio na mipaka unaweza kuufanya uhuru huo kuleta madhara yasiyokusudiwa. Rais asipokuwa na uwezo wa kumkaripia Waziri wake, au hata kumshauri tu abadili mwelekeo basi ana ,udhaifu mkubwa.

Twafahamu kuwa JK aliafikiana na Kituo cha Demokrasia kuhusu njia mwafaka za kukamilisha mchakato wa Katiba mpya kwa ufanisi, ikiwa ni pamoja na kuliendesha zoezi hilo taratibu badala ya kuliharakisha kama Sitta anavyofanya sasa. Kwa makusudi kabisa, Sitta akaamua kupuuza ushauri wa JK, na kuendesha BMK atakavyo. Si vigumu kufahamu kuwa kilichompa jeuri Sitta ni ufahamu mzuri kwamba bosi wake, yaani JK, ni dhaifu asiyeweza kumwajibisha kwa kiburi hicho. Na muda wa kumshughulikia Sitta ataupata wapi ilhali yupo bize na safari zake za kuzunguka dunia?

Uongozi katika zama hizi za JK umekuwa kama mzaha flani, mchezo wa kuingiza usiopendeza, yaani a bad comedy, Hebu angalia picha hizi hapa chini kupata uthibitisho wa ninachoandika





Pichani juu ni vimemo vya Sitta akilazimisha matakwa yake.

Lakini tukiangalia kwa upana zaidi kuhusu ombwe lililosababishwa na udhaifu wa JK, tunakutana na kituko hiki hapa chini. Kimsingi, moja ya kumbukumbu za muda mrefu kuhusu utawala wa JK itabaki kuwa kuibuka kwa wanasiasa/viongozi ambao pengine sifa pekee waliyonayo katika uanasiasa/ uongozi wao ni vituko, kashfa, mazingaombwe, na mambo mengine yasiyopendeza. Kama nilivyotanabaisha hapo awali, ombwe hilo liletoa fursa kwa kila Dick, Tom na Harry kufanya atakavyo. Hebu angalia kioja hiki


Nimalizie makala hii kwa kutoa wito kwa Watanzania wenzangu kukazani katika dua/sala ili JK amalize muda wake kwa amani, maana mustakabali wa taifa letu upo hatarini. Ni muhimu kufahamu kuwa amani na utulivu tuliyonayo yahitaji vitendo vya wapuuzi wachache tu kabla haijatokomea. Na uzoefu waonyesha kuwa amani ikipotea ni ngumu sana kuirejesha. Na kubwa tunalohitaji ni kukoma mara moja kwa vitendo vya watawala wetu kuwaona Watanzania kama 'hamnazo' kama tunavyoshuhudia katika BMK huko Dodoma.

Tumtegemee Mungu katika hili, sambamba na jitihada zetu wenyewe kukabiliana na tabia inayozidi kukota mizizi ya kugeuza uongozi kuwa uhuni flani.

MUNGU IBARIKI TANZANIA 


23 Dec 2011


Leon Bahati
RAIS Jakaya Kikwete amemteua Jaji Mstaafu Damian Lubuva kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Jaji Lewis Makame, ambaye uitumishi wake kwa umma ulimalizika Julai, mwaka huu.

Amemteua pia Julius Mallaba kuwa Mkurugenzi wa NEC ili kuchukua nafasi ya Rajabu Kiravu ambaye naye amestaafu.Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Phillemon Luhanjo Jijini Dar es Salaam jana, ilieleza kwamba walioteuliwa walianza kazi tangu Jumatatu iliyopita.

Katika uteuzi huo, Rais Kikwete alimteua Jaji Mstaafu Hamid Mahmoud Hamid kuwa Makamu Mwenyekiti wa NEC.

Kabla ya uteuzi wake, Lubuva alikuwa Jaji katika Mahakama ya Rufani Tanzania na baada ya kustaafu aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Maadili ya Viongozi.

Naye Hamid alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar kabla ya kustaafu na anachukua nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Jaji Omari Makungu.

Kwa mujibu wa Luhanjo, Jaji Makungu aliwahi pia kuteuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na baadaye akateuliwa kuwa Jaji Mkuu.

Luhanjo alisema Mallaba kabla ya uteuzi huo, alikuwa Mkurugenzi wa Sehemu ya Mikataba katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

CHANZO: Mwananchi

NAOMBA KUMPONGEZA JK KWA UTEUZI HUU MAKINI.JAJI LUBUVA NI MIONGNI MWWA WATANZANIA WACHACHE WAZALENDO WALIOSALIA.HONGERA SANA MZEE LUBUVA

17 Mar 2010


KLABU ya soka ya Real Madrid ya nchini Hispania jana imemkabidhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete tuzo ya Jezi ya kiungo mshambuliaji wa timu hiyo Critiano Ronaldo. Akizungumza katika hafura hiyo iliyofanyika Ikuru jana Meya wa jiji la Dar es Salaam, Adam Kimbisa ambaye alimukabidhi Rais jezi hiyo kwa niaba ya viongozi wa klabu ya Real Madrid kutokana kutambua mchango wake katika mchezo wa soka.

"Kwa heshima hiyo Klabu hiyo imetoa tuzo Jezi namba tisa inayovaliwa na mchezaji mahiri wa timu hiyo Cristano Ronado," alisema Kimbisa.

Naye Rais Kikweta mara baada ya kupokea tuzo hiyo ameshukuru klabu hiyo ya Real Madrid kwa zawadi hiyo ambayo alisema kuwa ni hesima kubwa kwa Watanzania.

"Nashukuru sana kwa zawadi hii, Madrid ni timu kubwa duniani kutukumbuka sisi Watanzania ni faraja kubwa kwetu.

"Itabidi tutafute sababu mpya ya kuwaalika upya kuja hapa nchini kufutia ili ya awali kushindikana, ni matumani yetu pia tutapata watu ambao watatusaidia kuwaleta," alisema.

Klabu hiyo ya Real Madrid itarajia kufanya ziara yake hapa nchini kwa ajili ya uzinduzi wa Uwanja wa Taifa mwanzoni mwa mwaka juzi lakini kutokana kuchelewa kukamilika kwa ujenzi wa uwanja huo timu hiyo hakuweza kufanya hivyo.

CHANZO: Mwananchi.

30 Jul 2009


Kizitto Noya, Dodoma


SASA ni wazi kwamba sakata la Richmond limeingia katika hatua nyingine baada ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ofisi Rais kutangaza kwamba, Rais Jakaya Kikwete hahusiki kwa namna yoyote na kashfa hiyo ambayo inaendelea kulitikisa taifa kwa muda sasa.

Hatua ya Rais Kikwete kutotaka kuhusishwa na kashfa hiyo ya Richmond kunazidi kuibua maswali mengi kutoka kwa wananchi kwamba, ni nini hatima ya mjadala huo ambao unazidi kupamba moto kila kukicha nje na ndani ya Bunge.

Wakati Rais Kikwete akijivua kutoka katika sakata hilo, Kamati ya Nishati na Madini imetoa maazimio ya kupinga jinsi serikali inavyotekeleza maazimio ya Bunge kuhusu ripoti ya Richmond. Jana jioni Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, ilitoa taarifa ikimuepusha rais na kashfa hiyo.

"Tumepata kusema huko nyuma, na tunapenda kusisitiza kwa mara nyingine kuwa, Rais hana mkono katika Richmond na hata Ripoti ya Bunge iliyotolewa kufuatia uchunguzi katika suala hilo la Richmond, haikumhusisha Rais Kikwete," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa ya Ikulu, imetolewa huku Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba akidai kwamba, Rais Kikwete anahusika na Richmond kwa kuwa maamuzi yalifanyika chini ya serikali anayoiongoza.

Habari kutoka Dodoma zinadai kuwa kutokana na kusuasua kwa utekelezaji wa maazimio ya Bunge kutaka maafisa wa serikali waliohusika kwa njia moja au nyingine na mchakato wa kampuni hiyo kupewa zabuni Tanesco, wachukuliwe hatua.

Kundi mojawapo la wabunge limeeleza kutoridhishwa na ripoti ya serikali iliyotolewa bungeni hivi karibuni kuwasafisha. Kundi hilo limepanga kumchukulia hatua kubwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye ndiye kiongozi mkuu wa serikali bungeni, kutokana na kuwanusuru maafisa waliotuhumiwa kuhusika na kashfa hiyo.

Wakati kamati hiyo ikitoa msimamo huo, wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) walikutana jana usiku katika Ukumbi wa Pius Msekwa kutafakari sakata hilo.

Ingawa tangazo la Mwenyekiti wa Bunge, Job Ndugai jana mchana halikueleza agenda za kikao hicho, vyanzo huru vya habari vililidokeza gazeti hili kuwa wabunge hao wangejadili ripoti ya Richmond na kuweka mkakati wa kuinusuru serikali.

Mjumbe wa Kamati ya Nishati na Madini ambaye hakutaka kutajwa gazetini akihofia kuvunja Kanuni za Bunge kwa kutoa siri za vikao, alisema kamati haikuridhishwa na ripoti ya serikali hasa katika suala la kuwasafisha Mkurugenzi wa Takukuru, Dk Edward Hoseah na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika.

"Kamati haikubaliani na ripoti hiyo hasa pale iliposema Dk Hoseah na Mwanyika hawana hatia. Tumekuwa na vikao kwa siku mbili jana (juzi), leo (jana) na bado tunaendelea kesho (leo),”alisema.

Alisema mapendekezo ya kamati ya Bunge kuhusu Richmond yalijitosheleza kimaamuzi na serikali ilitakiwa kuyatekeleza tu na sio kuendesha uchunguzi mwingine.

"Uchunguzi ulishafanywa na Bunge, serikali ilitakiwa kutekeleza tu. Ilikuaje ifanye tena uchunguzi kwa muda zaidi ya ule uliopangwa na Bunge badala ya kufanya utekelezaji?" alihoji.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, William Shelukindo na Makamu wake, Dk Harrison Mwakyembe hawakupatikana jana kuzungumzia suala hilo na simu zao za mikononi kutopatikana kabisa.

Mjumbe wa kamati iliyoundwa na Bunge kuchunguza suala la Richmond, Habib Mnyaa alikiri kuwa na taarifa ya kamati ya kisekta kukutana na kujadili ripoti hiyo, lakini akaeleza kuwa kikao hicho kilichokaa juzi na jana, kinamalizika leo.

"Kikao kimekuwapo, lakini hakijafikia maamuzi hayo unayosema," alisema Mnyaa akirejea hoja ya mwandishi wa habari aliyetaka kuthibitisha taarifa kwamba, kikao hicho kimejenga hoja ya kutokuwa na imani na serikali katika suala la Richmond.

Hata hivyo, habari nyingine zinadai kuwa kamati hiyo leo inatarajia kumweka kiti moto Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja ili awaeleze ni kwanini serikali imeshindwa kutekeleza mapendekezo ya Bunge.

Hata hivyo, mjumbe mwingine, Lucas Selelii alilieleza gazeti hili kuwa vikao vyote vilivyojadili Richmond, vimemaliza kazi na kuwasilisha hoja zake kwa spika wa Bunge Samuel Sitta ambaye leo atatoa mwongozo bungeni.

"Mjadala wa Richmond umemalizika na mambo yote kesho (leo) yako hadharani. Kamati ya kisekta imekaa na kuandaa taarifa ambayo amekabidhiwa spika wa Bunge leo (jana). Kikubwa jamii ijue kwamba, kamati iko makini, haimwonei wala kumpendelea mtu," alisema Selelii.

Alipotakiwa kuthibitisha kama amepokea hoja za kamati hiyo kuhusu Richmond na kwamba ataruhusu mjadala wake bungeni leo, Spika Sita alisema: "Haijanifikia bado".

Alifafanua kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini anatarajia kuwasilisha hoja za Kiwira na Richmond kesho, siku ambayo pia wenyeviti wa kamati za Miundombinu, Ardhi, Maliasili na Mazingira watawasilisha hoja zao.

Alibanwa zaidi aeleze kama endapo angeipata jana jioni angekuwa tayari kuiwasilisha leo kama ilivyoelezwa, alijibu:

"Hata kama nitaipata sasa, siwezi kuitable kesho (leo) kwani nahitaji muda kuisoma na kuielewa".

Awali mbung wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe alisema suala la Richmond limeanza kuligawa taifa na njia pekee ya kuirudishia jamii imani na serikali, ni Rais kwa mamlaka ya kuwa mkuu wa nchi kuunda jopo la majaji kupitia upya hoja zote na kutoa maamuzi.

"Suala hili limeonekana kuigonganisha mihimili mikuu miwili ya dola, Bunge na Serikali, dawa yake sasa ili liishe, ni Rais kama mkuu wa nchi nasisitiza, mkuu wa nchi sio serikali kuunda tume ya majaji wapitie Maazimio ya Bunge, utekelezaji wa serikali na watoe maamuzi," alisema.

Alisema: "Inavyoonekana kila upande unavutia kwake, wakati Bunge likitaka serikali itekeleze mapendekezo yake ndani ya miezi mitatu, serikali imetumia karibu mwaka na nusu na bado inakuja na majibu ya kubabaisha.
CHANZO: Mwananchi

4 Jun 2009


President Jakaya Kikwete yesterday pointed fingers at businessmen who for years have exploited poor farmers by buying cheap from them and selling dear on the world market, pledging measures to redress the situation.

The President made the remarks in Dar es Salaam when speaking at the 6th Tanzania National Business Council (TNBC) meeting whose theme this year is ‘Agriculture First.’

The meeting hosting more than 400 local and international delegates is discussing and exploring untapped opportunities in the agricultural sector.

He said businessmen have been profiting from the farmers’ sweat by underpaying them on the pretext that prices in the world market have gone down.

We will not tolerate them any more…their days are numbered,” he said, adding that businessmen should buy farmers’ produce at a reasonable price.

“There are instances when a businessman buys produce at 200/- per kilo and sells it at 800/- in the world market…this is pure exploitation which must be stopped,” he said.

President Kikwete said the government would soon put in place a mechanism that would force business people to comply with farmers’ set price, a move that would help reduce the scale of the problem.


He however pointed out that the country’s agricultural sector can only move forward if irrigation farming would be fully deployed. Kikwete told participants that it was prime time for Tanzania’s farmers to shift from traditional to modern farming.

We, in the government, believe that the Agricultural Sector Development Programme embraces almost all the basic theoretical frameworks about why Tanzania’s agriculture is backward and what needs to be done. What remains is doing what is envisaged in the programme in terms of actualization and time frame,” he said, adding:

“ASDP seeks to see a number of interventions to deal with constraints in agriculture. One is to increase use of irrigation in farming. Overdependence on rain has kept our agriculture backwards for many years. Two is to increase the use of high yield seeds by farmers. We need to build local capacity in research and seed production.” He also noted that there was a need to increase the use of fertilizer among farmers.

“Low use of fertilizer has kept productivity low,” he stressed.

The President also underscored the need to increase the use of insecticides and pesticides as well as enabling farmers to use modern skills and techniques in production through extension services and use of agricultural research findings.

President Kikwete said that there was a need to improve crop marketing infrastructure; as well as all other services that will impact on agriculture, including improvement on physical infrastructure, access to finance for agriculture, facilitating growth of manufacturing and industries which add value to agriculture.

The other critical factor is the promotion of the large scale agriculture in Tanzania to complement smallholder and peasant agriculture. He noted that there is plenty of land which can be utilized by large scale farmers to increase agricultural production and productivity in the country.

I would like us to discuss how best we can leverage private capital into large scale farming in Tanzania. I want us to discuss ways and means of attracting investors both local and foreign in farming and livestock development,” he said.

SOURCE: ippmedia.com


DO WE STILL NEED A MINISTER FOR AGRICULTURE,FOOD AND CO-OPERATIVES?BY THE WAY,WHERE'S STEPHEN WASSIRA?

3 Jun 2009


By Costantine Sebastian

President Jakaya Kikwete is set to announce a bail out package worth billions of shillings to rescue local companies that have been hit hard by the global economic crisis.

The Government's stimulus package, which awaits cabinet approval on Thursday, could be unveiled by Saturday, Finance and Economic Affairs minister Mustafa Mkulo said yesterday.

He said the bail out plan, compiled by a team of experts led by Bank of Tanzania (BoT) governor Prof Benno Ndulu, would be the major point in President Kikwete's address to the Parliament next week.

The Citizen has established that the package primarily seeks to keep the current economic growth on track and provide a form of social security amid fears of massive job losses due to looming company closures.

Addressing members of the Parliamentary Committee on Finance and Economy yesterday, Mr Mkulo said the stimulus package was critical "given the weight and importance of the current situation".

"The stimulus plan will target companies-mainly banks - to help them sustain their operations for a period of between six months and two years,"the minister said.

He also announced the approval of a $224 million (approx. Sh292 billion) advance from the $336 million (over Sh436 billion) released to the Government by the International Monetary Fund (IMF) to help fight the adverse effects of the global crisis.

Treasury officials, who spoke on condition of anonymity since they were not allowed to divulge details of the rescue package to the media, said the plan also targeted to control food prices.

And Prof Ndulu said the Government was trying to boost the economy amid concerns the slowdown could reverse nearly a decade of buoyant economic growth in the country.

He said Tanzania would do whatever was possible to "protect the hard-earned macroeconomic stability".

"The most crucial thing for us to do is to minimise the possible interruption in the growth process during the 2009/10 financial year, and cushion workers against lay offs and high costs of food," the central bank chief said early this year in a presentation on the crisis.

Prof Ndulu urged cooperation between the private sector and Government saying the downturn posed a real challenge to the country's economy and food security.

This was despite earlier remarks by the Government that the recession would not have any major effect on Tanzania since the country was remotely linked to the global economic system.

But there seems to be consensus now between key economic stakeholders in the country that the downturn is a major threat to Tanzania's economy.

However, some economic analysts criticise the Government for "dragging its feet" and taking too long to wake up to the reality of the magnitude of the economic crisis.

Dr Honest Ngowi, a lecturer at Mzumbe University warned that if not properly administered, the bail out plan could spark massive spending, which could lead to hyperinflation.

"While it is important to stimulate the economy through bailing out specific key industries, there is need to guard against the negative implications of such interventions," he said.

Prof Ndulu, who headed the team that drew up the stimulus package, said the Government, which had poor revenue collections this year, would seek collaboration with banks in its response to the crisis.

The banks would be encouraged to open lines of credit, especially to local horticultural, cotton, coffee and sisal farmers, whose exports have plunged due to falling demand from the traditional European markets.

The other major focus area of the rescue plan would be promoting infrastructure investments to boost agricultural production, which is projected to decline to 2.4 per cent in 2009 from 3.6 per cent in 2008.

Prof Ndulu also said there were efforts to eliminate red tape, aimed at attracting investments at a time some foreign investors are either rescheduling or cancelling their projects.

In a paper titled The Global Financial and Economic Crisis: Challenges and Responses, the central bank chief said the Government would not bail out companies that had solvency problems, which only got worse due to the crisis.

"Beneficiaries of the stimulus package should be sectors, projects and organisations with systematic risks and whose demise will negatively affect the economy and lives of ordinary people," he said.

Additional reporting by Damas Kanyabwoya and Ray Naluyaga


SOURCE: The Citizen

LET'S HOPE THE BAILOUT PLAN WON'T BECOME ANOTHER EPA,RICHMOND,AND THE LIKE.I AM STILL UNCONVINCED IF THE PLAN IS ACTUALLY FOOLPROOF TO MAFISADI,ESPECIALLY AS THE NATION IS HEADING FOR POLLS IN A YEAR'S TIME.CAN'T CONNECT THE DOTS?WELL,IT'S RUMOURED THAT THE LAST ELECTION WAS "EFFECTIVELY" USED BY THE FISADIs TO CONVINCE THE POWERS THAT BE TO RELEASE THE EPA LOOT.


JUST THINKING ALOUD!

4 May 2009

PICHA HII NILOPATA KWA HISANI YA MJENGWA INAMWONYESHA JK AKIONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM HAPO IKULU.HIVI KWANINI VIKAO VYA CCM VIFANYIKIE IKULU KATIKA ZAMA HIZI ZA MFUMO WA VYAMA VINGI?KWANINI ISIWE MAKAO MAKUU YA CCM DODOMA AU HATA PALE LUMUMBA DAR?


18 Apr 2009


Riyadh, April 16 - Saudi investors have asked Tanzania if they can lease 500,000 hectares of farmland mainly for rice and wheat farming as part of a plan to secure food supplies for the desert kingdom, officials said.

Senior officials from the Saudi capital's chamber of commerce made the request on the sidelines of a meeting with visiting Tanzanian President Jakaya Kikwete.

"Tanzania is ready to do business with you ... There is 100 million acres (40.5 million hectares) of good arable land," Kikwete told Saudi businessmen.

Samir Ali Kabbani, head of the chamber's agriculture committee, said: "We had very positive feedback."

"He (Kikwete) told us that Tanzanian authorities can lease us plots each of which covers up to 10,000 hectares for a 99-year period," he told Reuters after the meeting.

The Saudi government has joined private operators to invest in farm projects abroad after a long and costly food sufficiency plan threatened to deplete the desert kingdom's water supplies.

Saudi businessmen and officials will visit Tanzania in the next few weeks.

"They can lease the land from the government," January Makamba, an aide to President Kikwete, told Reuters.

"But we have to make sure we don't end up in a situation similar to that of Nigeria: Huge oil reserves but long queues in front of petrol stations," Makamba said.

Saudi officials are particularly interested in Tanzania because of its geographic proximity, political stability and the availability of water resources and farmland.

Several Saudi firms have already started investing in agricultural projects from Indonesia to Ethiopia.

Indonesia said in August that Saudi BinLadin Group would invest $4.3 billion on 500,000 hectares for rice farming.

Saudi Arabia's annual wheat needs are estimated at about 2.5 million tonnes and it imported a little over 1 million tonnes of rice in 2008, according to the U.S. Department of Agriculture.


SOURCE: Reuters

"TANZANIAN AUTHORITIES CAN LEASE THE SAUDIS PLOTS EACH OF WHICH COVERS UP TO 10K HECTARES FOR A 99-YEAR PERIOD!?"

DID I QUOTE THAT RIGHT? YES I DID.

CALL ME ONE OF THE DOUBTING THOMASES BUT IF THIS STORY IS TRUE,THEN PERHAPS THE LIKE OF CHIEF MANGUNGO WERE NOT SO DUMB WHEN THEY WERE DUPPED INTO SIGNING SOME CRAZY LAND CONTACT WITH KARL PETERS&co..AT LEAST THE CHIEFS COULD HAVE AN EXCUSE...IT'S DURING THE "DARK AGES" AND THE FORE-RUNNERS OF COLONIALISM TOOK OF ADVANTAGE OF THE CHIEFS' ILLITERACY AND LACK OF SUFFICIENT KNOWLEDGE IN GOVARNANCE OF THEIR PEOPLE AND PROPERTY.

BY THE WAY,INSTEAD OF BEGGING THE SAUDIS,WHY SHOULDNT THE PRIORITY BE IN EMPOWERING THE LOCAL FARMERS IN A COUNTRY WHERE THE ECONOMY DEPENDES HEAVILY ON AGRICULTURE THAT ACCOUNTS FOR MORE THAN 40% OF GDP?

17 Apr 2009

KWA MUJIBU WA GAZETI LA Uhuru,KATIBU MKUU WA CCM,YUSUPH MAKAMBA,AMEAGIZA UONGOZI WA CCM NA JUMUIYA ZAKE NGAZI ZA MIKOA KUANDAA MAPAMBANO YA KUMPONGEZA JK NA SERIKALI KWA KAZI NZURI KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA.....
Nadhani muda si mrefu kutakuwa na tangazo jingine la kuagiza maandamano ya kupongeza mafanikio ya kutimizwa kwa ahadi ya MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA sambamba na pongezi za kuwabainisha wamiliki wa Kagoda.
CCM HOYEEEE!!!!!

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI!!!!!

That's all I can say!

Habari nyingine ndani ya gazeti hilo ni pamoja na "UFISADI MALIASILI:Sh Bil 2.4 zayeyuka kiutatanishi;Mil 790 zatumika kununua pikipiki hewa;Watumishi watimuliwa,wachunguzwa"





16 Apr 2009

Raiamwema Merged
Raiamwema Merged JIMMY PHILEMON Habari katika toleo la wiki hii la jarida la Raia Mwema

Picha kwa hisani ya KENNEDY

Mwanahalisi Merged
Mwanahalisi Merged JIMMY PHILEMON Article ya Mwanahalisi kuhusu ufisadi na 2010.

Picha kwa hisani ya Kennedy

2 Apr 2009



Gazeti la Mwananchi linaandika:


MKURUGENZI wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hosea jana alikuwa kwenye wakati mgumu baada ya wabunge kumhoji uhalali wake wa kuiongoza taasisi hiyo wakati akikabiliwa na tuhuma za kusafisha kashfa ya zabuni ya mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura.

Mkurugenzi huyo, ambaye alitajwa kwenye taarifa ya tume teule ya bunge iliyochunguza kashfa hiyo na serikali kutakiwa kumchukulia hatua, alikumbwa na mtafaruku huo katika semina ya Miundombinu ya Uadilifu iliyoandaliwa na Takukuru na Chama cha Wabunge wa Afrika (APNAC) na kufanyika kwenye hoteli ya Whitesands jijini Dar es salaam.

Ilifikia wakati Dk Hosea alionekana kukerwa sana na maswali kiasi cha kulazimika kuwaonya kuwa anao uwezo wa kuwachafua kama wakiendelea kufanya mambo yanayoonekana kumvua nguo.

Mbunge wa Busega, Raphael Chegeni ndiye aliyeanzisha kizaazaa hicho baada ya kumhoji Dk Hosea akisema ilikuwaje taasisi yake iliisafisha kampuni tata ya kuzalisha umeme wa dharura Richmond Development (LLC) iliyokuwa inakabiliwa na kashfa ya kushinda zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura wakati kamati teule ya Bunge iliyoundwa kuchunguza mkataba wake, iligundua kuwepo kwa mazingira ya rushwa.

“Inakuwaje wakati wa mjadala wa Richmond, wewe mkururugenzi wa Takukuru ulikanusha kuwapo rushwa na uchunguzi wa kamati ya bunge ulibaini kuwepo rushwa ndani ya kampuni hiyo? Je ni nani mwenye dhamana ya kukuadhibu wewe na taasisi yako kuhusu rushwa’’ aliuliza Chageni.

Swali hilo halikutegemewa na Dk Hosea na lilionekana kumuudhi na kulazimika kuchukua kipaza sauti na kusitisha maswali na kuanza kujibu kwa ghadhabu.

“Hapa siyo jukwaani hivyo tusilete siasa. Nipo hapa kwa ajili ya kufundisha na kama ni suala la Richmond waziri mkuu alishaliongelea na ndiyo mwenye dhamana ya kujibu hilo. Mimi sina jibu kwa hilo na kama mtu hapendi kuvuliwa nguo kwanini umvue mwenzako,” alisema Dk Hosea.

"Mjadala huu aachiwe Waziri Mkuu Mizengo Pinda na aliyeuliza swali hilo hanitendei haki kwani hakuna hoja nyingine ya maendeleo kwa jamii ambalo inaweza kujadiliwa... mbona mnang’ang’ania kujibu hilo pekee.

“Najua kuna watu wanatumiwa ili niongee halafu nibabaike katika kujibu nanishindwe kufanya kazi yangu. Mbona mnang’ang’ania jambo hilo tu wakati kuna hoja nyingine za maendeleo kwa jamii. Kuhusu suala la Richmond sijibu ng’o.”.



Nalo Tanzania Daima linaripoti:


MKURUGENZI wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU), Edward Hosea, jana aliwashambulia wabunge katika semina ya kukabiliana na rushwa iliyoandaliwa na taasisi yake na kuwashirikisha wabunge wa Chama cha Kupambana na Rushwa (APNAC).

Akitoa mada katika semina hiyo, Dk. Hosea aliwashambulia wabunge hao hadharani, kwamba wamekuwa wakichangamkia posho za semina wakati hakuna uwajibikaji.

Katika mada hiyo iliyoonekana dhahiri kuwakera wabunge hao, Dk. Hosea alisema baadhi yao wamekuwa wakihudhuria na kusaini posho zaidi ya tatu katika semina tofauti kwa siku moja, huku wakishindwa kuwajibika, jambo ambalo alisema ni aina mojawapo ya rushwa.

“Wapo wabunge wanaohudhuria semina zaidi ya tatu kwa siku moja na kusaini posho, lakini hata baada ya kuwezeshwa kwa posho hizo, hakuna uwajibikaji. Kwa kweli kuna mambo mengi yanayotokea, lakini tunayafumbia macho,” alisema Dk. Hosea.

Mbali na kusaini posho kwenye semina tatu kwa siku, Dk. Hosea pia alisema wapo wabunge ambao wanatumia vibaya ubunge wao kwa kutokaa kwenye foleni wawapo sehemu za huduma kama benki.

Pia aliwapasha wabunge kuwa hivi sasa siri nyeti za serikali ziko wazi, na kwamba inatokana na ukosefu wa maadili miongoni mwao.

Hata hivyo, baada ya kumaliza kutoa mada hiyo, baadhi ya wabunge walionekana dhahiri kukerwa na mada hiyo na kutaka kujibu mapigo kwa kuhoji utendaji wa taasisi hiyo na mafanikio yake tangu ilipoanzishwa.

Mbunge wa kwanza kutoa dukuduku lake, alikuwa Dk, Raphael Chegeni (Busega-CCM) ambaye alihoji utendaji wa TAKUKURU na kueleza kutoridhishwa kwake.

Dk. Chegeni alianza kujibu mapigo kwa kuhoji uwajibikaji wa Dk. Hosea na taasisi yake kuwa, iliwahi kuchunguza kashfa ya zabuni ya kampuni ya kufua umeme wa dharura, Richmond, na kuitangazia jamii kwamba hakukuwa na rushwa katika zabuni hiyo.

Kama hiyo haitoshi, Dk. Chegeni alisema TAKUKURU pia ilishindwa kuchunguza kashfa ya minara pacha ya majengo ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na badala yake Kampuni ya nje ya Ernest & Young ilibua ufisadi mkubwa na hatimaye leo baadhi ya watuhumiwa wamefikishwa mahakamani.

Huku akishangiliwa na baadhi ya wabunge, Dk. Chegeni alihoji ujenzi wa gharama wa ofisi za TAKUKURU nchini pamoja na magari ya kifahari wanayotumia wakati haiwajibiki ipasavyo katika kukabiliana na rushwa.

“TAKUKURU mnawajibika nini? Mlisema kwenye Richmond hakuna rushwa, lakini baadaye Bunge lilibaini kuwapo kwa rushwa, kwenye ujenzi wa minara pacha ya BoT mmeshindwa kuchunguza hadi kampuni ya nje ndiyo iliyokuja kuibua kashfa hiyo,” alisema Dk. Chegeni.

Kutokana na hoja hiyo, Dk. Hosea alikuja juu na kuwataka wabunge hao kuacha kuhoji mambo hayo, kwani wakianza kuchambuana, hakuna atakayebaki salama.

“Hapa hatukuja kulumbana, tumekuja kwenye semina, si mahala pake, lakini nyie wabunge ndio mlioamua kupitia Kamati Teule ya Bunge na mapendekezo yenu yapo, kwa hiyo iulizeni serikali, lakini hatuko hapa kushambuliana,” alisema Dk. Hosea.

Hata hivyo, baada ya malumbano hayo makali, wabunge na maofisa wa TAKUKURU, waliendelea na semina yao inayofanyika katika ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam, inayotarajia kumalizika leo.



Wakati huo huo viongozi wawili wakuu wa Chadema,

Freeman Mbowe na Dr Wilbroad Slaa wametoa matamshi mazito kuhusiana na ishu ya Dowans.Gazeti la Mwananchi linaripoti




KATIBU mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amesema kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kumtetea mkurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Dk Idris Rashid kinamtia wasiwasi na kuhoji uhalali wa kufunga mjadala wa Dowans.

Dk Slaa alikuwa mmoja wa watu waliohojiwa na Mwananchi kuhusu maoni yao juu ya hotuba ya kila mwezi ya Rais Kikwete aliyotoa juzi kuzungumzia mambo mbalimbali, likiwemo suala la mpango uliokwama wa serikali kununua mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura ya kampuni ya Dowans Tanzania Limited.

Ingawa Dk Rashid alionekana kushutumu wabunge waliopinga kutekelezwa kwa azma hiyo wakati akitangaza uamuzi wa Tanesco kuachana na mpango wa kununua mtambo huo, Rais Kikwete aliipongeza Tanesco kwa uamuzi huo huku akionekana kutaka malumbano juu ya suala hilo yaishe.

Lakini Dk Slaa anaona kauli hizo zinalenga kumlinda Dk Rashid, gavana wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

"Tuna mashaka naye Kikwete kwa kauli yake ya kumtetea Dk Idris ambaye pia sisi tuna mashaka naye kuwa alihusika katikasakata la ununuzi wa rada," alisema Dk Slaa.

"Kikwete hawezi kueleweka kwa kumtetea mtu aliyedaiwa kuhusika na kampuni ya nchini Uingereza, akidai inatuhumiwa kupokea fedha kupitia akaunti inayodaiwa kuwa ya mwanasheria wa zamani."

Dk Slaa alisema hofu yake inakuwa kubwa zaidi kutokana na kile alichodai kuwa wakati sakata la Tanesco na ununuzi wa mitambo ya Dowans likipamba moto, Kikwete alikwenda nje ya nchi na aliporejea alitoa kauli kumtetea mkurugenzi huyo.

Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini iliishauri serikali isinunue mitambo hiyo ya Dowans kwa kuwa kufanya hivyo ni kukiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma, ambayo inazuia kununuliwa kwa vitu vilivyotumika.

Hata hivyo, Tanesco na serikali hawakuridhika na ushauri huo wa Bunge na badala yake wakazunguka na kuliwasilisha suala hilo kwenye Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma, ambayo ilishindwa kutoa maamuzi hasa baada ya bunge kueleza kuwa maoni ya kamati ya awali ndio msimamo wa chombo hicho cha kutunga sheria.

Kukwama kwa mpango huo kulimfanya Dk Rashid kuitisha kikao na waandishi na kulaumu wabunge, akidai kuwa waligeuza suala hilo kuwa la kisiasa na kudai asilaumiwe iwapo nchi itaingia gizani.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, ambaye aliunga mkono mpango wa serikali kununua mitambo hiyo akitaka watu waangalie kwa umakini tatizo lililo mbele, hakuwa na maoni yoyote alipotafutwa na Mwananchi.

"Sina maoni yoyote," alisema Zitto ambaye mkoa wake wa Kigoma uko kwenye matatizo makubwa ya umeme na ambao Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja aliahidi bungeni kuwa utakuwa umefungiwa mtambo wa megawati 6 ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.

Naye kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, Hamad Rashid alisema tatizo la umeme nchini limetokana na serikali kushindwa kufanyia kazi maeneo 15 ambayo iliyaainisha ili kukabiliana nalo na ndiyo inayostahili kubeba mzigo wa lawama.

Alisema serikali inapaswa kulaumiwa kwa tatizo la umeme kwa kuwa imeshindwa kufanyia kazi suala hilo tangu mwaka 2006 na kwamba iwapo maeneo hayo yangefanyiwa kazi, kero ya umeme ingemalizika na wala mjadala kuhusu mitambo ya Dowans usingekuwepo.

“2005/2006 tulikumbwa na tatizo kubwa la ukame na kusababisha mgao mkubwa wa umeme. Katika juhudi za kutafuta njia mbadala, serikali iliainisha maeneo 15 ya kuyafanyia kazi ili kuondoa tatizo hilo,” alisema Rashid.

Alisema moja ya maeneo hayo ni ununuzi wa mitambo ya kufua umeme wa dharura, ambalo ndilo lililosababisha mjadala mkubwa wa kitaifa kutokana na Tanesco kutaka kununua mitambo ya Dowans, ambayo ilirithishwa mkataba wa kampuni ya Richmond Development (LLC) iliyoshinda katika mazingira ya utata zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura.

“Maeneo hayo yapo katika hansard (vitabu maalum vya kuhifadhia kumbukumbu za bunge) na nitayatoa kwa waandishi katika mkutano wangu nao kesho au keshokutwa," alisema Rashid.

Alisema anaunga mkono hotuba ya Kikwete kwa kuwa alichozungumza ndicho alichotaka kukieleza kwa wananchi akiongeza kwamba mkutano wake na waandishi hautakuwa tena wa kutoa msimamo wa kambi ya upinzani kama alivyodhamiria awali bali kuikumbusha serikali kuyafanyia kazi maeneo hayo.

Hata hivyo alisema hotuba hiyo ya Kikwete inathibitisha kuwa serikali iliridhia uamuzi wa bunge juu ya mjadala wa ununuzi
wa mitambo ya kampuni ya Dowans.

Alisema bunge lilitoa maamuzi yake kuishauri Tanesco isinunue mitambo hiyo kutokana na utata uliopo kati ya uhusiano wa Dowans na kampuni ya Richmond na kwamba iwapo haikuridhia ingerudi bungeni na kuliomba bunge libadilishe maamuzi yake.

“Hotuba ya rais ni ushahidi kuwa serikali imeridhia maamuzi halali ya bunge na ndio maana rais akamaliza mjadala wa Dowans na kuwapongeza Tanesco kwa kuachana na nia ya kununua mitambo hiyo,” alisema Rashid.

Lakini Dk Slaa hakukubaliana na kauli ya Rais Kikwete kutaka malumbano kuhusu ununuzi wa mitambo ya Dowans yaachwe.

"Ametumia udikteta kufunga mjadala," alisema Dk Slaa ambaye ni mwanasheria. "Wananchi hawakumpa mamlaka hayo ya kuwazuia kujadili rasilimali zao na nchi yao.

"Siku zote nasema Kikwete asituamulie... wananchi wanazungumza juu ya rasilimali na nchi yao, wanasiasa ni wadau katika maslahi ya nchi, asituamulie juu ya rasilimali zetu.

"Hakupewa mamlaka ya kutuamlia nini cha kujadili. Hatuwezi kukubali... kwa sababu gani analazimisha kufunga mjadala? Lazima kuna kitu."


Nalo Tanzania Daima linaandika:


MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amemtaka Rais Jakaya Kikwete, kutofunga mjadala wa suala la mitambo ya kampuni ya kuzalisha umeme wa dharura, Dowans, bila kuwaeleza wananchi ukweli kuhusu wamiliki wake na mahala walipo.

Mbowe aliyasema hayo jana katika mahojiano maalum na Tanzania Daima, akitoa maoni yake kuhusu baadhi ya masuala aliyoyazungumza Rais Kikwete juzi usiku, wakati akilihutubia taifa kwa njia ya
redio na televisheni.

Alisema hatua ya Rais Kikwete kutangaza kufunga mjadala wa Dowans ni ya kuungwa mkono kwa kuwa mjadala huo si jibu la matatizo ya umeme nchini, lakini alimtaka kwanza awaeleze Watanzania ukweli wote kuhusu Kampuni ya Dowans, ndipo aufunge mjadala huo vizuri.

“Tunakubaliana na ushauri wake wa kutaka mjadala wa Dowans uishe. Tunakubaliana naye kwa sababu Dowans si jibu la matatizo ya msingi ya sekta ya nishati nchini. Hata hivyo, Kikwete asikimbilie kufunga mjadala bila kuwaeleza wananchi, Dowans ni nani. Watoe tamko, waueleze umma wa Watanzania, wamiliki wa Dowans ni nani, wako wapi, wanafanya nini, wataje watu wote wanaonufaika na Dowans, kisha ndipo atufungie mjadala huo vizuri. Kikwete anataka kuficha ukweli,” alisema Mbowe.

Akizungumzia tatizo la uhaba wa umeme nchini, alisema si mara ya kwanza kwa Rais Kikwete kuahidi kumaliza tatizo la umeme, kwani wakati wa sakata la kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond, alishaahidi kuwa tatizo la umeme lingekuwa historia.

“Si mara ya kwanza rais kuahidi kwamba nchi haitakuwa gizani. Ameshaahidi hivyo wakati wa vuta nikuvute ya Richmond, ameshasema hivyo karibu mara tatu. Alishasema kwamba matatizo ya umeme yatakuwa historia, lakini hadi leo nchi haina umeme wa uhakika. Rais anaendelea kutoa maneno matamu, hatuwezi kupata umeme kwa maneno yake….”

“Asitazame tu uchaguzi wa 2010, na kuwapa watu maneno matamu, atazame mbele. Tunahitaji mkakati wa muda mrefu na mfupi. Na si mkakati tu, tunahitaji mpango wa utekelezaji, maana sera ya nishati imeainisha yote hayo, lakini tatizo utekelezaji. Serikali inapaswa kuwa na uhakika wa kulipatia taifa umeme hata kwa miaka zaidi ya 50 ijayo,” alisema Mbowe.

Alisema kwa kiasi kikubwa sekta ya umeme nchini inaathiriwa na wafanyabiashara wakubwa ambao ni maswahiba wa Rais Kikwete na Chama Cha Mapinduzi (CCM), wanaoigeuza sekta hiyo kuwa chanzo chao cha mapato, kwa kuanzisha kampuni za kufua umeme wa dharura na kuiuzia TANESCO kwa gharama kubwa.

Alisisitiza kuwa, msingi wa tatizo la nishati ya umeme nchini ni kutokuwapo kwa sera endelevu na mikakati yakinifu na inayotekelezeka, ya muda mrefu na mfupi, ya kuzalisha na kusambaza umeme.

Alisema pamoja na uhaba wa umeme unaozalishwa, bado sehemu kubwa ya umeme huo imekuwa ikiibwa na kusababisha wananchi wengi kukosa haki ya kupata umeme.

“Na tatizo hapa si uhaba wa umeme unaozalishwa tu. Bado kuna umeme mwingi sana unaibwa, lakini serikali halizungumzii hili,” alisema Mbowe.

Alisema tatizo jingine ni umeme unaozalishwa kuwa wa gharama kubwa kiasi cha wananchi wengi kushindwa kuupata na kuutumia.

“Tuna network (mtandao) kubwa sana ya umeme. Maeneo mengi nyaya za umeme zinapita jirani na nyumba za watu, lakini wenye uwezo wa kuunganisha umeme huo kwenye nyumba zao ni wachache sana. Gharama za kufunga umeme majumbani ni kubwa mno kwa Mtanzania maskini kumudu. Gharama za kuutumia, kulipa ankara pia ni kubwa.

“Kwa hiyo Rais Kikwete na serikali yake, wasiishie tu kuzungumzia uzalishaji, lakini pia lazima waeleze ni jinsi gani watapunguza gharama za umeme ili Watanzania maskini nao waweze kuutumia,” alisema Mbowe.

Akizungumzia tahadhari ya Rais Kikwete, kwamba kwenye baadhi ya mikoa kuna uwezekano wa kutokea tatizo la chakula kwa sababu ya kuchelewa kwa mvua za masika, Mbowe alisema ni aibu na fedheha kubwa kwa nchi yenye maji mengi yanayotiririka kama Tanzania, kutangaza njaa ndani ya msimu mmoja wa matatizo ya mvua.

“Sikio la kufa halisikii dawa. Tatizo la chakula ni tatizo la kujitakia. Kukosa mvua msimu mmoja, halafu rais anatangaza njaa, ni jambo la kutia aibu sana. Tuna maji mengi sana yanatiririka, tuna mito na maziwa, ardhi yenye rutuba nzuri sana. Tuna kila kitu, tatizo ni ukosefu wa sera nzuri na uongozi bora,” alisema Mbowe.

Alisema Rais Kikwete anapaswa kumfukuza mara moja Waziri wake wa Kilimo na Chakula kwa kushindwa kusimamia programu za kilimo cha uwagiliaji nchini.

“Walipoingia madarakani walikutana na tatizo la chakula. Kikwete na Lowassa waligawa chakula na kuahidi kwamba njaa ile isingetokea tena, sasa leo wanatuambia nini? Wamefanya nini? Na hii ndiyo kawaida yake, anaahidi halafu anasahau. Nchi hii ikipata viongozi wazuri serikalini, kilimo cha umwagiliaji kinaweza kabisa kumaliza tatizo la njaa za mara kwa mara,” alisema Mbowe.

Alisema serikali inapaswa kuwa na mpango wa makusudi wa muda mrefu wa kuzalisha na kuhifadhi chakula kwa wingi, ili kiwe kinaingia katika mtandao wa matumizi ya wananchi, pindi kunapokuwa na uhaba wa chakula.

Katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi uliopita, Rais Kikwete pamoja na mambo mengine, alitaka mjadala wa kununua au kutonunua mitambo ya Dowans, ufungwe baada ya wahusika (TANESCO), kutangaza kuachana na uamuzi wa kutaka kuinunua.

Alisema anashangazwa na malumbano ya baadhi ya viongozi wa siasa kuhusu jambo hilo.

Mjadala wa Dowans, hivi karibuni uliwaingiza katika malumbano makali, Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, wote wa CCM





PENGINE DR HOSEA ANA HAKI YA KUWA MKALI KWANI YEYE HAKUJITEUA KATIKA WADHIFA HUO BALI ALITEULIWA...NA PIA KWA VILE KWA MUJIBU WA "UTAMADUNI WETU" KUJIUZULU NI MITHILI YA KUMKOSEA ADABU ALIYEKUTEUA BASI HUENDA KUMSAKAMA DR HOSEA NI KUMWONEA KWANI YAELEKEA ALIYEMTEAU KARIDHIKA NAE.AMA KWA HAKIKA TANZANIA BILA UFISADI INAWEZEKANA!!!

27 Mar 2009


KWA MTU YEYOTE MWENYE AKILI TIMAMU,HATA AKIAMSHWA USINGIZINI AU AKIWA BWII KWA ULEVI,HAIINGII KICHWANI KUSIKIA HOJA ZA KIFISADI ZA KUNUNUA MITAMBO ILIYONGIZWA NCHI KITAPELI NA MAJAMBAZI WA RICHMOND NA HATIMAYE KURITHISHWA KISANII KWA WENZAO WA DOWANS.TUKIRUHUSU HILI LITOKEE,KUNA MAHALA ITAFIKA NCHI YETU NAYO ITAUZWA NA KISHA TUTATAKIWA KUINUNUA BACK....


Tausi Mbowe na Elias Msuya

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Dk Wilbroad Slaa ameitaka serikali kuitaifisha mitambo ya Kampuni ya kuzalisha umeme ya Dowans badala ya kujadili manunuzi yake.

Dk Slaa aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam baada yakutopa taarifa ya kamati kuu kilichokutana kwaajili ya kuandaa mkutano wa baraza kuu.

Alisema kuwa mitambo ya Dowans ilirithiwa kutoka kwenye kampuni ya Richmond ambayo ilibainika bungeni kuwa ni ya kifisadi kwahiyo hakuna haja ya kuinunua tena bali kuitaifisha.

“Msimamo wangu siku zote ni kutaifishwa kwa mitambo ile na siyo kuinunua. Naishangaa serikali, kutaka kuinunua mitambo ya Dowans wakati mitambo ile ilishabainishwa Bungeni kuwa ni ya kifisadi. Kama mtu umekamata kitu chako cha wizi utakinunua tena?" alihoji

Akizungumzia malumbano kati ya Mbunge wa Kyela Dk Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Igunga Rostam Aziz, Dk Slaa alisema,

“Mradi wa kuzalisha umeme nimeushughulikia kwa miezi minane. Nilikwenda hadi kijiji cha Kisesida mkoni Singida ambako ndiko kampuni mbili za Power Pool East Africa ya Dk Mwakyembe na wenzake na Wind East Africa ya Rostam Aziz zimewekeza.

Kampuni ya Power Pool East Afrika ni ya wazalendo na imeshalipa fidia kwa wakazi wa kijiji cha Kisesida lakini ile ya Wind East Africa haijafanya hivyo, badala yake inabebwa na kiongozi wa ngazi za juu mkoani ambaye amekuwa akiwakejeli wanakijiji wa Kisesida. Ndiyo maana kuna kuwa na malumbano kati ya Rostam Aziz na Dk Mwakyembe,” alisema Dk Mwakyembe.

Akizungumzia tatizo la mgawo wa umeme ambalo litangazwa na Tanesco hivi karibuni, Dk Slaa alisema,"Baada ya kubainika kwa kashfa ya Richmond, Rais Kiwete alitangaza kuwa suala la mgawo wa umeme litakuwa historia katika nchi hii, sasa mgawo huu unatoka wapi tena? nendeni mkamwulize,” alisema Dk Slaa.

Aidha alimshangaa Rais Kikwete kwa kuendelea kumwacha madarakani Mkurugenzi wa Tanesco, Idriss Rashid wakati anatuhumiwa kwa ufisadi.

"Dk Rashid (PICHANI JUU) alihusishwa na ufisadi alipokuwa Gavana wa Benki kuu. Tumeshatoa vilelezo vyote kuthibitisha jinsi alivyoshiriki kwenye ununuzi wa rada na ndiyo maana sasa hivi anashirkiana na Dowans ili kununua mitambo yake kiufisadi. Tunashangaa kwanini Rais Kikwete hamchunguzi, wala kumwajibisha. Eti wanasema Serikali ya Uingereza inachunguza, wakati si kweli. Uingereza wanachunguza ushiriki wa BAE system siyo watu wetu,” alisema Dk Slaa.



CHANZO: Mwananchi
IT MAKES A LOT OF SENSE,DOESN'T IT?UNAMKAMATA KIBAKA NA MALI YAKO,BADALA YA KUMKWINDA AKUREJESHEE NA HATIMAYE KUMFIKISHA POLISI ETI UNAKUBALI AKUUZIE ALICHOKUIBIA!IT COULD ONLY HAPPEN IN TANZANIA,I SUPPOSE!

2 Mar 2009

UAMUZI WA SERIKALI KUHUSU KURA YA MAONI DHIDI YA WAUAJI WA ALBINO-ULIOTANGAZWA NA RAIS JK KWENYE HOTUBA YAKE YA MWISHO WA MWEZI FEBRUARI- UMEPOKELEWA KWA HISIA TOFAUTI NA BAADHI YA WANANCHI KAMA INAVYOELEZWA KATIKA HABARI NAMBARI 2 HAPO CHINI.KWA MTAZAMO WANGU,NADHANI WANANCHI WANA KILA SABABU YA KUHOJI UAMUZI HUO WA SERIKALI HASA KWA VILE IMEKUWA NI KAMA DESTURI KWA NCHI YETU KUTANGAZA HATUA KALI ZA KISIASA AMBAZO HUISHIA KUBAKI HISTORIA TU PASIPO MAFANIKIO.WENGI TUNAKUMBUKA KUHUSU DEADLINE WALIYOPEWA WALA RUSHWA MWANZONI MWA MWAKA 2006 NA ORODHA YA MAJINA YA WANAOJIHUSISHWA NA BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA ILIYOKABIDHIWA KWA (ALIYEKUWA )WAZIRI BAKARI MWAPACHU....LAKINI HADI LEO HAKUNA HATUA YOYOTE ILIYOCHUKULIWA.KWANZA SOMA HABARI HUSIKA KISHA TUJADILI ZAIDI:

Kikwete:Wanaoua albinokuanza kutajwa kwa kura
mwezi huu

Claud Mshana

RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa, maandalizi ya zoezi la upigaji kura za maoni za kung'amua wauaji wa albino na vikongwe, limekamilika na litazinduliwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda. Akizungumza jana kwenye hotuba yake ya mwisho wa mwezi wa Februari, Rais Kikwete alisema kuwa maandalizi ya kutekeleza zoezi hilo yamekamilika na kwamba, waziri mkuu atafanya uzinduzi rasmi wa zoezi hilo mwishoni mwa wiki ya kwanza ya mwezi huu.

Alisema kuwa alitoa maagizo ya kufanyika kwa zoezi hilo mwezi Desemba mwaka jana kwamba wananchi wapige kura kutaja majina ya waovu hao, akiwa na dhamira ya kuwapa nafasi wananchi kushiriki kikamilifu.

"Maandalizi ya kutekeleza uamuzi wangu huo yanaelekea kukamilika, mheshimiwa waziri mkuu atafanya uzinduzi rasmi wa zoezi hilo mwishoni mwa wiki ya kwanza ya mwezi Machi, 2009 na zoezi lenyewe la kupiga kura kufanyika kuanzia wiki ya pili ya Machi, 2009."

Alifafanua kuwa katika zoezi hilo pia wauaji wa vikongwe, majambazi wa kutumia silaha na wauzaji wa dawa za kulevya nao watahusishwa. Alitaja utaratibu wa kuendesha zoezi hilo utakuwa ni kufuata kanda na kwamba mikoa imegawanywa katika kanda saba ambazo ni Kanda ya Ziwa inayojumuisha mikoa ya Kagera, Mara, Mwanza na Shinyanga.

Kanda ya Nyanda za Juu Kusini yenye mikoa ya Iringa, Mbeya, Rukwa na Ruvuma; Kanda ya Kati (Dodoma na Singida), Kanda ya Kusini (Lindi na Mtwara), Kanda ya Magharibi (Kigoma na Tabora), Kanda ya Kaskazini (Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara), na Kanda ya Mashariki (Dar es Salaam, Pwani na Morogoro).
Wakuu wa mikoa yote nchini wameshapewa mwongozo wa jinsi ya kutekeleza zoezi hilo na kutaja miongoni mwa mambo watakayotakiwa kuzingatia ni pamoja na kuelimisha na kuhamasisha wananchi kushiriki katika zoezi hilo, upigaji kura ufanyike mwezi Machi kwa tarehe zitakazopangwa kwa kuzingatia kanda hizo.

"Kamati za ulinzi na usalama za mikoa zikiongozwa na wakuu wa mikoa zisimamie zoezi hili kwa makini. Kadhalika, kamati za ulinzi na usalama za wilaya zikiongozwa na wakuu wa wilaya zitaongoza utekelezaji katika wilaya zao na kushirikisha serikali za vijiji na mitaa," alisema Rais Kikwete.

"Napenda kuitumia fursa hii kuwasihi Watanzania; wake kwa waume; vijana na wazee tujitokeze kwa wingi kuwataja watu wanaojihusisha na maovu hayo katika jamii. Kura ni siri, hakuna atakayejua umemtaja nani. Hata msimamizi wa kituo hawezi kujua," alisema......
CHANZO: Mwananchi

NA IFUATAYO NI HABARI KUHUSU REACTION YA BAADHI YA WANANCHI JIJINI DAR ES AALAAM KUHUSIANA NA UAMUZI HUO WA KURA YA MAONI KUWATAMBUA WAUAJI WA MAALBINO.


Dar wataka serikali iweke wazi chanzo cha mauaji ya
albino


Na Boniface Meena

WANANCHI wa Mkoa wa Dar es Salaam wameiomba serikali itafute na kuewaleza chanzo cha mauaji ya albino, badala ya kuendelea kutoa kauli za kisiasa wakati hali inaendelea kuwa mbaya.

Pia wamesema hawadhani kama upigaji kura kuhusu mauaji hayo kama utasaidia kwa kuwa hata kesi za waliokamatwa kwa kuhusishwa na mauaji hayo hazijasikika. Mbali na hilo wameitaka serikali kuanzisha mahakama maalum kwaajili ya kusikiliza kesi za mauaji hayo ili waweze kujua maamuzi yanayotolewa na mahakama. Wakizungumza mbele ya Mkuu wa wilaya ya Temeke ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Kihato wananchi hao walidai serikali inaoneka kutokuwa makini na suala hilo kwa kuwa hakuna hata kesi moja ya mauaji ya albino iliyotolewa hukumu hadi hivi sasa.

Mbunge wa kuteuliwa, Al-Shaimar Kweiger alidai kuwa kuna mtandao mkubwa wa matajiri unaohusika na mauaji hayo ambao alisema hadhani kama unaweza kuishinda serikali katika kupambana nao. "Hili suala limeshazungumziwa sana, tumezunguka na Waziri Mkuu sehemu nyingi, lakini hawakomi nadhani kuna mtandao mkubwa wa watu wenye fedha uko nyuma ya jambo hili," alisema Kweiger.

Josephat Torner ambaye ni mwanaharkati wa kupinga mauaji ya albino alisema suala hilo linaonekana kuwa la kisiasa kwa kuwa hakuna hatua za haraka zilizochukuliwa kuwasaisdia wahanga wa mauaji hayo. "Tunataka kujua serikali imefikia wapi tangu suala hili lilipotangazwa kuwa ni la kitaifa," alihoji Torner. Torner ambaye ni albino alisema hawadhani kama upigaji kura utasaidia, kwani wanaona kama ni mchezo wa kisiasa hivyop wangependa kujua wako katika hali gani hivi sasa kuhusu mauaji hayo.

Christopher Andendekisye ambaye ni Mkurugenzi wa Shirikisho la Vyama vya Walemavu Tanzania (Shivyawata) alisema, kama serikali haitakuwa makini na mauaji hayo yanaweza kuendelea kwa muda mrefu kwa kuwa chanzo chake bado hakijajulikana. "Itabidi tuwe na wiki maalum au mahakama maalumu kwaajili ya kusikiliza kesi za mauaji haya na kama haiwezekani tuambiwe chanzo ni nini," alisema Andendekisye. Maria Chale ambaye ni albino alidai kuwa inaonekana serikali mpaka sasa haijui chanzo kitu ambacho kinatia wasiwasi kama zoezi hilo litafanikiwa.

Steven pascal ambaye ni katibu wa Albino muungano Investiment Trust(Amit), alisema ni bora jeshi (JWTZ) watumike kuwaska wanaohusika na mauaji hayo. "Ni bora Jeshi lihusishwe kwani hawa jamaa (wanajeshi) akipigwa mwenzao mmoja kijiji kizima kinazingira mpaka wapatikane wahusuka," alisema Pascal. Wananchi hao walisemas hayo jana wakitoa maoni yao mbele ya DC Kihato ambaye alikutana nao kuwaeleza juu ya uzinduzi wa upigaji kura za maoni dhidi ya mauaji ya albino utakaofanyika jijini Dar es Salaam Machi 5, mwaka huu.

Akijibu baadhi ya maoni yaliyotolewa na wananchi hao, Kihato ni kweli serikali haijatatua tatizo hilo kama wananchi wanavyotaka lakini inajitahidi kuhakikisha mauaji hayo yanatokomezwa, ndiyo maana wameitisha kura ya maoni.


CHANZO: Mwananchi

KATIKA HABARI YA KWANZA,KUNA MANENO NIMEYAONYESHA KWA RANGI NYEKUNDU KWA SABABU MAALUMU.PAMOJA NA NIA NZURI YA SERIKALI KUTAFUTA UFUMBUZI WA KUDUMU WA MAUAJI YA MAALBINO,WAZO LA KURA YA MAONI LINAWEZA LISIWE NA MAFANIKO YANAYOKUSUDIWA.KWANZA,KAMA MANENO YENYE RANGI NYEKUNDU YANAVYOONYESHA "...Alifafanua kuwa katika zoezi hilo pia wauaji wa vikongwe, majambazi wa kutumia silaha na wauzaji wa dawa za kulevya nao watahusishwa..." KUTANUA WIGO WA WALENGWA KUNALIFANYA ZOEZI HILO KUWA PANA ZAIDI ILHALI MAANDALIZI YAKIWA DUNI.ZAIDI,IWAPO KWELI DHAMIRA NI KUWASAKA WAUAJI WA MAALBINO,KUNA HAJA GANI KUINGIZA HABARI ZA WAUZA MADAYA YA KULEVYA,KWA MFANO,AMBAO HUKO NYUMA TULISHAAMBIWA KUWA ORODHA YAO ILIKABIDHIWA KWA WAZIRI MWAPACHU NAE AKADAI KUWA AMEIKABIDHI KWA RAIS?

JINGINE AMBALO LINAHITAJI TAFAKURI NI UTATA KATIKA KAULI ZA VIONGOZI WETU.RAIS ANASEMA ALITOA AGIZO MWEZI DESEMBA,LAKINI TUNAKUMBUKA KAULI ZA WAZIRI MKUU HAPO KATIKATI KWAMBA WAUAJI WA MAALBINO NAO WAUAWE (JAPO BAADAYE ALIOMBA MSAMAHA KWA MACHOZI HUKO BUNGENI)....INA MAANA AGIZO LA DESEMBA LILIPUUZWA NA KUBADILISHWA KUWA "JINO KWA JINO" KABLA HALIJAFUTWA KUFUATIA KELELE ZA WADAU KUHUSU HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA WA SHERIA?

NA KAMA AGIZO LILITOLEWA DISEMBA,KWANINI BASI ICHUKUE MIEZI MITATU MIZIMA KUTOA UAMUZI HUU AMBAO KWA HAKIKA UNAHITAJI MAANDALIZI MAZURI NA YA KUTOSHA (HUSUSAN UHAMASISHAJI)?JE WIKI MBILI ZINATOSHA ?RAIS ANASEMA "...maandalizi ya kutekeleza zoezi hilo yamekamilika na kwamba, waziri mkuu atafanya uzinduzi rasmi wa zoezi hilo mwishoni mwa wiki ya kwanza ya mwezi huu...zoezi lenyewe la kupiga kura kufanyika kuanzia wiki ya pili ya Machi, 2009."ARE WE ARE WE REALLY SERIOUS?KURA YA MAONI WIKI MOJA BAADA YA UZINDUZI!?JE MAANDALIZI YANAYODAIWA KUKAMILIKA HAYAKUPASWA KUJUMUISHA UHAMASISHAJI WA WANANCHI?PASIPO UMAKINI,ZOEZI HILI LITAISHIA KUTUNISHA POSHO ZA WAHUSIKA NA WAUAJI WA MAALBINO,WAUZA UNGA NA MAJAMBAZI WAKAENDELEA "KUPETA."

SWALI JINGINE LA MSINGI NI KUHUSU MATOKEO YA KURA HIYO YA MAONI.HIVI KWA MFANO BLOGU HII IKIPIGIWA KURA NYINGI KUWA NDIO SPONSOR WA WAUAJI WA MAALBINO (GOD FORBID),NINI KINAFUATA?MHUSIKA ATAKAMATWA NA KUHOJIWA KWA VILE KURA NYINGI ZIMESEMA HIVYO?MHUSIKA ATATAKIWA AJIELEZE KWANINI WANANCHI WENGI WAMEMPIGIA KURA "ZA CHUKI"?AU WAPELELEZI WATAINGIA UWANJANI KUANZA UCHUNGUZI?VIPI ILE TASK FORCE ILIYOUNDWA HUKO NYUMA?

KWA NCHI INAYOHESHIMU UTAWALA WA SHERIA INATARAJIWA KUWA MATOKEO YA KURA HIYO HAYATACHUKULIWA KUWA NDIO HUKUMU DHIDI YA WATAJWA.HIYO ITAMAANISHA KUFANYIA UCHUNGUZI MAJINA YA WALIOPATA KURA NYINGI.KISHA UCHUNGUZI UTAPOKAMILIKA NA USHAHIDI WA KUTOSHA KUPATIKANA NDIPO ZIANZE HATUA ZA KISHERIA KWA VILE,KWA MUJIBU WA SHERIA, NI MAHAKAMA PEKEE (NA SIO MATOKEO YA KURA YA MAONI) INAYOWEZA KUMTIA MTUHUMIWA HATIANI AU KUMWACHIA HURU.

MWISHO,NI MUHIMU PIA KUKUMBUKA NAMNA UTAMADUNI WA RUSHWA UNAVYOATHIRI MWENENDO WA MAISHA YA MTANZANIA KILA SIKU.HIVI KAMA BAADHI YA WAHESHIMIWA WANAWEZA KUNUNUA KURA ILI WATUWAKILISHE HUKO BUNGENI,KWA MFANO,ITASHINDIKANA VIPI KWA MATAJIRI WANAOFADHILI MAUAJI YA MAALBINO KUNUNUA KURA "ZA KUPENDWA" NA WAPIGA KURA?VIPI IWAPO MATOKEO YA KURA YATAONYESHA MAJINA YA BAADHI YA WAHUSIKA WA KAMPUNI YA KAGODA?HAKUTAKUWA NA KIGUGUGMIZI KAMA KILICHOPO KWENYE UFISADI WA KAMPUNI HIYO KWENYE FEDHA ZA EPA?

NA VIPI IWAPO WANYONGE WATAPIGIWA KURA ZA CHUKI?

MASWALI NI MENGI KULIKO MAJIBU.KWA HAKIKA DHAMIRA KUHUSU KURA YA MAONI NI NZURI LAKINI WASIWASI WANGU MKUBWA NI KATIKA UTEKELEZAJI WAKE.NA KAMA WALIVYOSEMA BAADHI YA WAKAZI WA DAR KATIKA STORI NAMBA 2,MAFANIKIO KATIKA HARAKATI ZA KUKOMESHA MAUAJI YA ALBINO YANAHITAJI JITIHADA ZA ZAIDI YA KAULI ZA KISIASA.

26 Nov 2008


Watendaji wa Ifakara wametakiwa kuangalia uwezekano wa kuzungumza na uongozi wa Kanisa Katoliki juu ya ughali wa tiba unaotolewa katika Hospitali yao ya Mtakatifu Francis. Rai hiyo imetolewa na Rais Jakaya Kikwete katika mkutano wa upokeaji taarifa ya wilaya, mkutano uliofanyika Ikulu Ndogo ya Ifakara juzi. 

Kauli hiyo ilitokana na rai ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini hapo ambao walitoa kilio cha tiba ghali katika hospitali hiyo na kutaka serikali iingilie kati. Hospitali hiyo inayomilikiwa na Kanisa Katoliki inadaiwa kutoa huduma kwa bei ghali baada ya wafadhili wake wakubwa wa Uswisi kujiondoa na kuingia Wataliano. 

Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya, Evaristo Ndikilo akichangia hoja ya afya, alisema kwamba kwa upande wao walikuwa wakifikiri kupandisha hadhi kituo chao cha afya kukifanya kuwa hospitali. Hoja hiyo pia ilizungumzwa na Mbunge wa Ulanga Mashariki, Celina Kombani juu ya kuwapo kwa haja ya kupandisha kituo hicho, na kueleza mchakato umeshaanza. Kombani pia ni Waziri wa Tamisemi. 

Mwenyekiti wa Halmadhauri ya Ifakara, Hassan Goagoa, alisema ughali wa hospitali hiyo ambayo inatumika pia na mikoa mingine na shughuli za utafiti, kunatokana na kuongezeka kwa gharama za uendeshaji na ingawa walishauriwa kuomba udhamini zaidi wa serikali kwa kuongeza idadi ya vitanda, hali imebaki kwao kama kitendawili. Hospitali ya Ifakara tayari ina vitanda vingi kwa hadhi yake ya kuwa hospitali teule ya rufaa. Rais aliendelea na ziara yake ya Mkoa wa Morogoro ambapo jana alitarajia kuzuru Wilaya ya Kilosa.

CHANZO: Habari Leo

31 Oct 2008


*Yataka sheria ziachwe zifuate mkondo wake
*Yasubiri uamuzi kuhusu sakata la ufisadi
*Yaguswa na usanii wa kampuni ya Richmond
*Yaahidi Rais Obama au McCain kuja nchini

Na Hassan Abbas


BALOZI wa Marekani nchini, Bw. Mark Green amekuwa mwanadiplomasia wa kwanza nchini kumshauri Rais Jakaya Kikwete kuhusu nini anachopaswa kukifanya saa chache kabla hajaamua hatima ya waliokwapua mabilioni kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA). 

Balozi Green aliyesisitiza kuwa mafisadi si watu wa kuachwa hata kama ni vigogo na kutaka sheria zichukue mkondo wake, ameifafanulia Majira jinsi alivyoguswa baada ya kuona kampuni ya kimarekani ya Richmond ilivyohusika katika utata kwenye sekta ya umeme nchini. 

Balozi Green alisema hayo jana katika mahojiano maalumu na gazeti hili ofisini kwake Dar es Salaam kuzungumzia masuala mbalimbali kuhusu uchaguzi wa Marekani, mtikisiko wa uchumi, hali ya kisiasa nchini na mtazamo wake kuhusu wagombea, maseneta Barack Obama na John McCain. 

EPA na Richmond 

Balozi Green alisema hawezi kujinasibu kuwa Marekani ni Taifa la mfano katika kupambana na rushwa, lakini alisisitiza kuwa katika miaka 232 ya Uhuru wa Taifa hilo, ujenzi wa jamii yenye kuwajibika kwa kufuata utawala wa sheria usiomwogopa mtu ndio msingi. 

"Rais Kikwete anafanya kazi kubwa ya kujenga Taifa. Lakini vita dhidi ya ufisadi inahitaji kutowaacha watu wakatamba. Sheria ichukue mkondo wake hata kama mtu ni mashuhuri kiasi gani. 

"Sisi Marekani tumekuwa na azma ya wazi kuwa kiongozi wa umma akiiba fedha za watu, anachunguzwa na kuchukuliwa hatua. Wamarekani ni wakarimu sana kutoa fedha zao kusaidia watu, lakini ni wakali sana wanapoona inafanyiwa ufisadi. Rais Kikwete akitumia sheria atafanikiwa," alisema Balozi Green na kusisitiza kuwa katika sakata la EPA, waliopoka fedha hizo wanapaswa kuwajibishwa. 

Akifafanua kuhusu hilo, Balozi Green alisema Rais Kikwete alitaja mikakati mizuri alipozungumza bungeni kuhusu namna atakavyowashughulikia mafisadi wa EPA. 

"Rais alitaja mikakati mizuri. Tunasubiri kuona atakavyoitekeleza," alisema. Akizungumza bungeni Agosti 21 mwaka huu, Rais Kikwete aliwapa mafisadi hao hadi Oktoba 30 (jana) wawe wamerejesha fedha hizo, vinginevyo ifikapo Novemba mosi (kesho) wawe wameburutwa kortini. 

Sakata la Richmond, kampuni iliyoshinda zabuni ya kufua umeme wa mamilioni nchini ikijieleza kuwa ilitokea Marekani, ni moja ya matukio yaliyoitikisa Serikali ya Rais Kikwete mwanzoni tu mwa utawala wake. 

Akilizungumzia sakata hilo, Balozi Green alisema Serikali ya Tanzania katika kupambana na rushwa inapaswa kufuata sheria bila kujali mhusika au kampuni husika imetoka nchi gani. 

"Suala la Richmond najua ilikuja ikafanya kazi kupitia kampuni iliyosajiliwa nchini. Lakini bila kujali kampuni hiyo ilitoka wapi, Serikali inapaswa kuchukua sheria haraka inapoona kuna ufisadi," alisema huku akikiri kuwa ukweli kwamba kampuni hiyo ilijieleza kutoka Marekani, ulimsumbua wakati wa sakata hilo, ingawa ubalozi wake hauwajibiki moja kwa moja katika mikataba inayohusu kampuni binafsi. 

Uchaguzi wa Marekani 

Balozi Green alikiri kuwa uchaguzi wa mwaka huu wa nchi hiyo umekuwa na hamasa kubwa hasa kutokana na ushiriki wa Seneta Obama, Mmarekani mwenmye asili ya Afrika wa kwanza kuteuliwa na chama kikuu kuwania urais. 

"Ni kweli kwamba ushiriki wa Seneta Obama umeibua hamasa miongoni mwa Wamarekani wengi, hilo ni suala lisilo na ubishi. Lakini pia hata uteuzi wa Seneta McCain naye umeibua ushawishi katika baadhi ya nchi. 

"Wakati huku Afrika Obama anaonekana kuwa na ushawishi, McCain naye ni kivutio hasa katika nchi za Mashariki ya Mbali ambako kutokana na historia yake ya kushiriki vita ya Vietnamu na kwa miaka mingi aliyokaa kwenye Kamati ya Mambo ya Nje kwenye Bunge la Seneti, alishiriki masuala mengi yanayohusu eneo hilo," alisema Balozi Green ambaye ni mfuasi wa Republican. 

Alisema, akiwatathmini wagombea hao wawili, anaona kuwa wote kwa sera zao, wana uwezo wa kuisaidia Marekani iwapo mmojawapo ataingia Ikulu. 

"Ukiangalia sera zao, hakuna shaka kwamba wote (McCain na Obama) wana mikakati ya dhati kuisaidia Marekani na historia zao zinaonesha wana uwezo mkubwa," aliongeza. 

Akizungumzia somo ambalo nchi za Afrika zinaweza kujifunza kutokana na kampeni zinazoendelea sasa nchini Marekani, Balozi Green alisema kubwa ni umuhimu wa watu kujadiliana masuala ya kitaifa kwa uwazi na mwishowe kila mwananchi akawa na fursa ya kupiga kura na kumchagua kiongozi anayemtaka. 

"Siwezi kusema kuwa Marekani ina demokrasia ya kuigwa, sote bado tunajifunza kutoka kwa kila mmoja. Lakini kama ilivyoonekana, mijadala ya wazi ni kitu muhimu ili kujadili masuala ya kitaifa na mwishowe kuheshimu uhuru wa kupiga kura. Naamini mkiimarisha hili, Afrika na Tanzania zitafanikiwa," aliongeza. 

Msukusuko wa uchumi na Afrika 

Balozi Green alikiri kuwa uchumi wa Marekani umetikisika, lakini akazitoa wasiwasi nchi za Afrika hususani Tanzania, kuwa kiwango cha misaada ya Marekani hakitaathirika kutokana na hali hiyo. 

"Kwa mfano, miradi ambayo tumekubali kuisaidia Tanzania ilishapitishwa na fungu lake lipo, kwa hiyo haitaathirika, sioni sababu ya Watanzania kuwa na wasiwasi," alisisitiza. 

Pia alisema hofu ya miradi mingi iliyoanzishwa chini ya utawala wa chama cha Republican nayo kubatilishwa, iwapo kitaingia madarakani chama cha Democrat haina msingi, kwani wakati wa upitishaji wa miradi hiyo Wamarekani hukubaliana kwa pamoja bila kujali itikadi ya vyama. 

"Kwa bahati nzuri nilikuwa kwenye Baraza la Wawakilishi, ni mmoja wa wawakilishi waliopigania kupitishwa kwa sheria iliyounda shirika la Millenium Challenge Account, linalotoa misaada mbalimbali kwa Afrika ikiwamo Tanzania. 

"Bahati nzuri wakati wa kujadili masuala haya, wabunge walikuwa wamoja bila kujali itikadi. Kwa hiyo hakuna atakayeweza kuzuia miradi hii, iliamuliwa kwa sauti ya Wamarekani wote," alisema.

Obama au McCain kuja Tanzania 

Akizungumzia ushirikiano mzuri baina ya Tanzania na Marekani, Balozi Green aliisifu kazi nzuri iliyofanywa na Rais wa zamani wa Marekani, Bw. Bill Clinton, ambaye ujio wake nchini na kazi za taasisi zake, ziliwafanya Wamarekani wengi kuijua au kuwa na nia ya kuijua Tanzania. 

"Hata ujio wa Bush, watu wanaweza kunipongeza kwa kufanikisha kuja kwake, lakini historia nzuri iliyowekwa na Clinton ndiyo iliyowazindua Wamarekani wengi kisha akaja Bush na baadaye mkutano wa Sullivan, lakini pia wadhifa wa Rais Kikwete kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, vimeifanya Tanzania kujulikana zaidi. 

Akizungumzia uwezekano wa ofisi yake kuhakikisha Rais ajaye wa Marekani anafuata nyayo hizo kwa kufika nchini, Balozi Green alisema: 

"Nitafurahi kuona siku moja Rais ajaye wa Marekani awe Seneta McCain au Seneta Obama anaitembelea Tanzania, kuimarisha uhusiano mzuri uliopo. Niko tayari kushughulikia hilo ili afike hapa. 

"Bahati nzuri Seneta McCain nimeshawahi kukutana naye wakati nikiwa kwenye Baraza la Wawakilishi, Obama hatujaweza kukutana kwa sababu wakati huo nikiwa kwenye siasa, yeye alikuwa bado yuko chini, lakini naamini wote watakuwa tayari kuja kuiona nchi hii nzuri," aliahidi. 

Balozi Green kitaaluma ni mwanasheria aliyepata kujaribu kuwania ugavana wa jimbo la Wisconsin kupitia chama cha Republican mwaka juzi akapoteza.

Chanzo:Majira

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.