19 May 2011

Makala yangu katika toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inazungumzia "usanii" wa CCM kujivua magamba,na kuwaingiza mkenge watu kama Nape Nnauye walioamini kuwa chama hicho kimeamua kufanya kweli,kabla ya "moto wa karatasi" haujazimika wenyewe.

Kadhalika,katika makala hiyo nimejaribu kuwashauri CCM watambue kuwa kamwe ugonjwa hautibiki kwa kuukwepa bali kuutambua na kuutibu.Kwa chama hicho,tatizo la msingi ni mwenyekiti wake wa taifa,Rais Jakaya Kikwete,ambaye aliletwa madarakani kwa nguvu za "magamba" na aliposhika hatamu za madaraka akayalea "magamba" hayo.The so-called magamba ni sehemu muhimu ya uhai wa kisiasa wa Kikwete.Kwahiyo kama CCM ina dhamira ya kweli ya kuondokana na ufisadi (magamba) hawana budi kuanza na Kikwete.

Pamoja na makala hiyo ni habari moto moto na makala nyingine zilizokwenda shule ndani ya jarida hili mwanana la Raia Mwema.BONYEZA PICHA HAPO JUU KUSOMA MAKALA HIYO.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.