26 Jul 2014

Tanzania yetu haina uhaba wa vituko, na si vituko vya kupendeza bali vya kukera.Kuna baadhi ya taasisi,ile ukiskia tu jina unatambua nini kinafuata.Kwa mfano Tanesco: kila ninaposkia kuhusu Tanesco ninatambua ni aidha ishu ya ulaji wa fedha za miradi hewa ya uzalishaji umeme usipo,au ni mgao wa umeme.

Benki Kuu ya Tanzania nayo ni miongoni mwa taasisi zilizojipatia umaarufu mkubwa katika ufisadi.Ni nani amesahau kuhusu moja ya skandali kubwa kabisa katika historia ya ufisadi Tanzania, yaani EPA? Nani amesahau mazingaombwe yaliyozunguka ishu ya EPA, kuanzia kufichwa jina la mmiliki wa jambazi mkubwa zaidi katika skandali hiyo, yaani Kampuni ya Kagoda hadi 'kifo' cha aliyekuwa Gavana wa Benki hiyo, Daudi Ballali (kama kweli alikufa basi ni vema mwili wake ukatumika kama kuni za kuchoma watenda maovu huko motoni).

Lakini Benki Kuu pia inajijengea sifa nyingine ya ubabaishaji, pengine kutokana na ukweli kwamba ubabaishaji ni moja ya kumbukumbu muhimu katika utendaji wa Serikali ya Awamu ya Nne ya Rais Jakaya Kikwete. Katikia 'toleo jipya' la ubabaishaji wa Benki Kuu, taasisi hiyo nyeti 'imelamba matapishi yake' baada ya kutoa taarifa za kujikanganya ndani ya wiki moja kuhusu hatma ya benki ya FBME. Angali mtiririko wa matukio:

Jumapili Julai 20,2014: Benki Kuu yasambaza taarifa kwamba tetesi kuhusu benki ya FBME kufungwa' na uendeshaji wake kuwekwa mikononi mwa Benki Kuu si sahihi, ni uzushi tu. Tamko hilo lipo hapa


Lakini katika hali inayoweza kuelezwa tu kama UBABAISHAJI,Benki Kuu hiyo hiyo, jana Ijumaa,iltoa tangazo linalokinzania kwa asilimia zaidi ya  100 na hilo hapo juu, ambapo sasa ilieleza kuwa FBME imewekwa chini ya uangalizi wake (Benki Kuu). 


Sidhani kama kuna neno sahihi la kuelezea sintofahamu hii zaidi ya UBABAISHAJI uliokithiri. Lakini nani anajali? Kama ambavyo Tanesco wanaweza kukata umeme kila wanapowashwa na vidole na Watanzania wakaishia kuitukana matusi ya nguoni kana kwamba matusi yatasaidia kumaliza mgao wa umeme, ndivyo habari hii ya ubabaishaji wa BoT ilivyopita kimyakimya kana kwamba walichofanya ni sawia.

TUMEROGWA?



0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.