12 Aug 2014


Hali nchini Iraki ni tete kufuatia uamuzi wa Rais wa nchi hiyo Fouadi Masoum (I guess wewe kame mie tulikuwa hatumfahamu mtu huyu wala kujua kama Iraki ina rais) 'kumtimua' Waziri Mkuu Nuri al-Maliki, aliyekuwa madarakani kwa miaka minane, na kumteua Haidar al-Abadi kuchukua wadhifa huo.

Hata hivyo, Maliki sio tu  amegoma kuondoka madarakani bali pia amemwaga wanamgambo na vikosi maalum vya jeshi (special forces) mitaani, na kupelekea kizaazaa cha aina yake.

Marekani, ambayo ilisaidia kumweka madarakani Maliki mwaka 2003 imempongeza Waziri Mkuu mpya al-Abadi, msaidizi wa zamani wa Maliki, kuashiria kuunga mkono mabadiliko hayo.

Akihutubia kwa njia ya televisheni (naam, pamoja na vurugu zote nchini Iraki bado televisheni zinafanya kazi) amesema hatua ya Rais kufanya mabadiliko hayo ni ukiukwaji hatari wa Katiba, huku akiambatana na 'wapambe' wake, ameahidi kutatua 'kero' hiyo.

Mkwe wake, Hussein al-Maliki, ameyaelezea mabadiliko hayo kuwa ni kinyume cha sheria, na kudai yatabadilishwa kortini. "Hatutokaa kimya," alidai.

Hata hivyo, Marekani imemwonya Maliki kutotumia nguvu za dola kung'ang'ania madaraka.

Mwislamu wa madehebu ya Shia, Maliki analaumiwa na washirika wake wa zamani huko Marekani na Iran kwa kuwasukuma waumini wa madhehebu ya SUnni katika mapambano yaliyopelekea 'sintofahamu' inayoendelea sasa kwa kikundi cha Sunni cha ISIS kudhamiria kuigeuza nchi hiyo kuwa taifa la Kiislam. Viongozi wengi wa ki-Sunni na Kikurdi wamekuwa wakipiga kelele kuwa Maliki anastahili kuachia ngazi, huku hata baadhi ya viongozi wenzake wa ki-shia wakiwa na msimamo kama huo.

CHANZO: Habari hii imetafsiriwa kutoka vyanzo mbalimbali mtandaoni

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.