22 Jun 2016


Mini-supermarket ya aina yake, The Farm Fresh Market, inafunguliwa leo jijini Dar es Salaam saa sita mchana kwa saa za Tanzania. Mini-supermarket hiyo ni ya kwanza na ya kipekee nchini Tanzania kuuza vyakula, mbogamboga, matunda na bidhaa kama hizo zikiwa fresh kuoka shambani na zote zikizalishwa nchini mwetu.

Mini-supermarket hiyo ipo eneo la VICTORIA mkabala na MERRY WATER inaangaliana na Barabara ya ALI HASSAN MWINYI.

Bidhaa zinazopatikana katika mini-supermarket hiyo zinatoka sehemu mbalimbali nchini Tanzania ambapo mbogamboga zinaletwa moja kwa moja kutoka kwa wakulima wa Arusha na Lushoto, viungo (spices) kutoka Zanzibar, ilhali matunda mbalimbali, nazi, mayai, kuku, nk vikitoka katika mashamba na vitalu vilivyopo jijini Dar.

Kadhalika, kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania, mini-supermarket hiyo itakuwa na 'baa' maalum (sio ya kuuza kilevi) kwa ajili ya 'smoothies', yaani juisi ya matunda halisi iliyotengenezwa kiasili pasi kuchanganya kemikali. 

Kana kwamba hiyo haitoshi, mini-supermarket hiyo ya kwanza ya aina yake nchini Tanzania itakuwa pia na sehemu ya ushauri wa tiba ya kisasa kwa kutumia vyakula au matunda. Yaani, vyakula na matunda mbalimbali ni tiba ya maradhi mbalimbali, na mini-supermarket hiyo itatoa ushauri kwa wateja kuhusu aina hiyo ya tiba ambayo ina umaarufu mkubwa kwa nchi zilizoendelea hasa kwa vile nyingi ya tiba za hospitali huambatana na kemikali fulani zinazoweza kuwa na athari kidogo kwa mwili. 



Huduma ya kufikishiwa bidhaa nyumbani au ofisini (delivery) inapatikana kwa gharama nafuu

Mazingira safi ya kiwango cha juu yaliyothibitishwa na Mamlaka ya Vyakula na Madawa Tanzania (TFDA)

Baa ambayo si ya kilevi bali smoothies (juisi asilia isiyo na kemikali)

Vitafunwa vinavyotengenezwa kwa spinachi, karoti, ufuta, nk

Vyakula, mbogamboga, matunda ,nk katika mafriji maalum yanayohakikisha virutubisho vinabaki inavyostahili kuwa kama shambani au ardhini...yaani unakula kitu asilia haswa.

Vitafunwa vya kisasa ambavyo licha ya kuhakikisha ladha na shibe kwa mteja vinaweka kipaumbele kwa virutubisho vinavyotumika vyenye manufaa kwa afya ya mlaji

Kila mahitaji ya mlo na afya ya mteja yanapatikana katika mini-supermarket hiyo ya aina yake nchini Tanzania

Viungo (spices) mbalimbali ambavyo ni fedha kutoka Zanzibar

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.