Showing posts with label HATMA YA TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label HATMA YA TANZANIA. Show all posts

14 Oct 2009


Na Fredy Azzah

MAKAMU Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa, amesema kashfa za ufisadi zinazowakabili baadhi ya viongozi wake, zimekiumbua chama hicho pamoja na serikali yake.

Akiwahutubia wanafunzi wa matawi ya CCM ya vyuo vikuu vilivyopo jijini Dar es Salaam, wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 10 ya kifo cha Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere jana, alisema ufisadi ambao umewakumba wengi umesababishwa na tabia ya viongozi kulindana na kutosimamia kikamilifu maadili ya uongozi yaliyoainishwa ndani ya katiba ya CCM.

Alisisitiza kuwa tabia hiyo ni kinyume na misingi ambayo Baba wa Taifa, aliwaachia Watanzania....ENDELEA

WAKATI HUOHUO

WASOMI na wanazuoni nchini, wamesema nchi haina dira na kwamba kuna mpasuko mkubwa ambao usiposhughulikiwa mapema, nchi inaweza kuingia kwenye machafuko.

Wakizungumza juzi katika baraza lililopewa jina la Mbongi, lililoandaliwa na Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Julius Nyerere, walisema mpasuko hiyo ni pamoja na ya udini, ukabila, ukanda, matatizo ya vitambulisho Zanzibar pamoja na hofu ya kuvunjika muungano...ENDELEA

CHANZO: Mwananchi

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.