Showing posts with label ROLE OF RELIGION IN FIGHT AGAINST CRRUPTION IN TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label ROLE OF RELIGION IN FIGHT AGAINST CRRUPTION IN TANZANIA. Show all posts

16 Apr 2009

Mke wa Lowassa azindua kitabu

Na Mwandishi Wetu,
MTANZANIA, Aprili 15, 2009.

Watu mbali mbali jana jioni walimiminika nyumbani kwa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, kushuhudia uzinduzi wa kitabu kilichotungwa na mkewe Regina, uliofanywa na Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo.

Regina aliandika kitabu hicho wakati akiwa katika matembezi binafsi inchini Israel, siku chache baada ya mumewe kujiuzulu uwaziri mkuu Februari mwaka jana kutokana na sakata la Richmond.

Kitabu hicho kilichoandikwa kwa lugha ya Kiingereza kiitwacho “Walk The Path With Diary in Israel, The Holy Land” kina kurasa 15 na dibaji yake imeandikwa na Monsinyori Julian Kangalawe kutoka Kanisa la Mtakatifu Joseph la Dar es Salaam.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Kardinali Pengo, bila kufafanua, aliwataka Watanzania waache tabia ya kusulubiana. “Yesu alikuja duniani, akasulubiwa na hadi leo watu wanaendelea kusulubiana. Tuache mchezo huo,” alisema.

Mhubiri maarufu mwenye makazi yake mjini Arusha, Christopher Mwakasege, ambaye pia alihudhuria hafla hiyo, alisema ni yeye aliyetoa wazo kwa Lowassa na mkewe kutembelea Israel baada ya matatizo yaliyowakuta.

Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Alex Malasusa, ambaye pia alihudhuria hafla hiyo, aliwahimiza watu kujenga moyo wa kupendana ili kujenga nchi yenye maelewano.

Mbali na Mlasasusa, Askofu Mstaafu wa KKKT Dayosisi ya Mashariki ni Pwani, Elinaza Sendoro, pia alihudhuria hafla hiyo, na akatumia nafasi hiyo kuwashawishi watu kutembelea Israel kujionea namna watu wa dini tofauti wanavyoishi.

Akizunmgumza katika hafla hiyo, Lowassa mwenyewe alisema baada ya kupata matatizo nayo, yeye na familia yake waliamua kumgeukia Mungu na kwamba ndio maana wakaamua kwenda Israel kutembelea maeneo takatifu.

LET'S BE HONEST.LOWASSA ALIJIUZULU KUTOKANA NA UFISADI WA RICHMOND.HILO HALINA MJADALA.SINA TATIZO NA HIYO ZIARA YAKE YA KUTEMBELEA ISRAEL.KAMA KWELI ALIENDA KUTUBU AU LA,ANAJUA YEYE NA MUNGU WAKE .LAKINI NASHINDWA KUWAELEWA HAO MAASKOFU WALIOJITOKEZA KATIKA SHUGHULI HIYO.NAELEWA KUWA DINI INAHUBIRI UPENDO NA KUSAMEHE WAKOSAJI LAKINI SIDHANI KAMA HIYO INAMAANISHA VIONGOZI WA DINI KUWA KARIBU NA WATUHUMIWA WA UFISADI.
NA MHASHAMU PENGO ANAPOTOA MFANO WA YESU KUSULUBIWA ANATAKA KUTUELEZA NINI?KWAMBA LOWASSA NAE ALISULUBIWA KAMA YESU?HIVI SIO RICHMOND NA BINAMU YAKE DOWANS ILIYOWASULUBU WALALAHOI WA TANZANIA KWA MAMILIONI YA SHILINGI!YESU ALISULUBIWA MSALABANI ILI KUWANUSUBURU WANYONGE,MASIKINI,WAJANE,YATIMA,NK KUTOKA KWA MINYORORO WANAYOFUNGWA NA MAFISADI.

JAPO NINA HESHIMA KUBWA KWA VIONGOZI HAO WA DINI LAKINI YAYUMKINIKA KUELEZA KWAMBA UHUDHURIAJI WAO HUO KATIKA HAFLA YA MTUHUMIWA WA UFISADI UNAWEZA KUTAFSIRIWA NA WAUMINI WAO KUWA NAO WANASAPOTI UFISADI.
IN A WIDER CONTEXT,UFISADI NI MATOKEO YA KUMOMONYOKA KWA MAADILI YA KIROHO.KITACHOTUPA IMANI KUWA WATUHUMIWA WA UFISADI WAMEAMUA KUMREJEA MUNGU SIO PUBLICITY STUNTS BALI FIRM COMMITMENT KATIKA KUHURUMIA NAFSI NA ROHO ZINAZOANGAMIA KUTOKANA NA MATENDO YA MAFISADI HAO.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.