12 Dec 2007


Wiki hii nimejaribu kulinganisha unazi wa wapenzi wa michezo wa Uingereza na baadhi ya kasumba za wanasiasa wetu wa huko nyumbani Tanzania.Alfajiri ya Jumapili iliyopita,bondia Mmarekani Floyd Mayweather alitoa kichapo kikali kwa bondia Ricky Hatton wa Uingereza,huko Las Vegas.Kama kawaida yao,na pasipo kujali umahiri wa Mayweather,Waingereza wengi walikuwa na uhakika mkubwa kuwa bondia wao angeibuka kidedea na kudumisha rekodi yake ya kutopoteza pambano.Lakini,Mayweather aliwasaidia kutofautisha kati ya "pub fighter" na "boxer in the ring",na kuwakumbusha kuwa wanaomuita "best pound-for-pound boxer in the world" hawafanyi hivyo kwa upendeleo.

Nimeulinganisha ubishi wa Waingereza na ule wa baadhi ya wanasiasa huko nyumbani ambao wamepinga matokeo ya utafiti wa REDET ambao unaonyesha wananchi wengi wamepoteza imani na taasisis kama Bunge na Baraza la Mawaziri.Ndondi na siasa wapi na wapi?Ni hivi,kama vile ambavyo mashabiki hao wa ndondi walivyokuwa hawataki kukubali ukweli kuwa mpinzani wa bondia wao ni bora zaidi na hivyo alikuwa na nafasi nzuri zaidi ya kushinda,wapinzani wa matokeo ya utafiti wa REDET hawataki kukubali ukweli kwamba wananchi hawaridhishwi na utendaji wao,sio kwa vile utafiti huo una walakini,bali ni kwa vile tu matokeo hayo yako kinyume na matarajio yao

Bingirika nayo hapa kwa makala nzima ndani ya gazeti la RAIA MWEMA



0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.