17 Feb 2008

Muda mchache uliopita,Kosovo imejitangazia uhuru wake ikiahidi kuwa nchi ya kidemokrasia,katika hatua inayoungwa mkono na Marekani na nchi nyingine za Magharibi lakini ikipingwa vikali na Russia na Serbia.

Spika wa Bunge Jakup Krasniqi,Waziri Mkuu Hashim Thaci na Rais Fatmir Sejdiu,ndio waliosaini tangazo hilo la uhuru ambalo limepokelewa kwa nderemo na vifijo katika nchi hiyo,hususan katika mji mkuu Pristina ambapo maandalizi ya shughuli hiyo yalianza kwa siku kadhaa.

Wakati hayo yakitokea,Rais wa Serbia Boris Tadic amelaani hatua hiyo ya Kosovo kujitangazia uhuru na kubainisha kuwa nchi yake haitambui uhuru huo wa Kosovo.Akijibu mashambulizi,Waziri Mkuu Thaci alisema kwamba kamwe Kosovo haiwezi kuwa tena chini ya himaya ya Serbia.Thaci,mpiganaji wa zamani wa Jeshi la Ukombozi la Kosovo ambalo kati ya mwaka 1998 hadi 1999 lilipambana na majeshi ya Serbia katika vita ya kudai uhuru iliyogharimu zaidi ya maisha 10,000.

Kwa undani zaidi kuhusu kuvunjika kwa nchi iliyokuwa ikijulikana kama Yugoslavia (unamkumbuka Tito!?) hadi kufikia Kosovo,bonyeza KIUNGANISHI hiki

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.