6 Oct 2009


NILIWAHI KUBASHIRI HUKO NYUMA KWAMBA KADRI 2010 INAVYOSOGEA NDIVYO TUTAVYOZIDI KUSHUHUDIA VITUKO.LEO HII MAKAMBA NAE AMEJIUNGA KATIKA VITA DHIDI YA UFISADI!HIVI SI BINADAMU HUYU ALIYEWATAKA WATANZANIA KUACHANA NA MIJADALA YA UFISADI KWA VILE BAADHI YA WAHUSIKA WAMEFIKISHWA MAHAKAMANI?

HEBU MSIKIE ALIVYOGEUKA KINYONGA KATIKA HABARI HII HAPA CHINI:

Makamba ahimiza mapambano dhidi ya ufisadi

na Jacob Ruvilo, Kigoma

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusufu Makamba, amesema ufisadi unapaswa kupigwa vita na kila Mtanzania mzalendo, kwani umechangia kwa kiasi kikubwa kudidimia maendeleo ya nchi.

Makamba alisema hayo juzi kwenye semina ya viongozi wa CCM Jimbo la Kigoma Mjini iliyofanyika katika viwanja vya Lake Tanganyika.

Alisema suala la watu kujipatia mali kinyume cha utaratibu na kuhujumu nchi havina uhusiano wowote na CCM, kwani watuhumiwa wote hawakuagizwa na chama kufanya hivyo, bali ni hulka zao binafsi.

Makamba alifafanua kuwa suala la muumini wa dhehebu fulani kwenda kinyume na maadili au amri ya vitabu vya dini, hapaswi kulaumiwa sheikh au mchungaji, badala yake ni muumini husika ambaye mwisho wa siku ndiye atakayepata adhabu kwa Mungu.

Aidha, Makamba alisema suala la vyama vya upinzani kushika bango na kuidhihaki CCM kuwa ni mafisadi kutokana na viongozi wachache wasio waaminifu, halina maana, bali suala la umoja na mshikamano katika kupinga mafisadi hao ni jukumu la watu wote, ikiwamo CCM.

Mbali na hilo, Makamba alikemea baadhi ya viongozi wa chama hicho kutumia uwezo wao wa fedha kutoa rushwa ili kupita katika chaguzi mbalimbali kuwa ni moja ya upatikana wa viongozi mafisadi na wasiofaa kwa jamii.

Alisema Tanzania haikuandaliwa kutawaliwa na wenye nacho na kwamba hali hiyo inaweka tabaka la mwenye nacho na asiyenacho, hali ambayo isipoangaliwa kwa umakini suala la rushwa litabaki kuwa ndoto.


TATIZO LETU WATANZANIA NI UWEPESI WETU KUAMINI KILA KINACHOAHIDIWA.MWAKA 2005 MAKAMBA NA CCM YAKE WALITAMBUA HILO NA KUJA NA AHADI LUKUKI IKIWEMO ILE MAARUFU YA KULETA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA.SASA WANASEMA KWAMBA SUALA LA MAISHA BORA LILIANZA ZAMA ZA MWALIMU NYERERE,PENGINE KATIKA KUKWEPA KUTUELEZA HAYO MAISHA BORA WALIYOAHIDI ILIKUWA NI KWA MAFISADI PEKEE AU...?MAANA KAMA SUALA HILO LILIASISIWA NA NYERERE BASI WANGETAMKA BAYANA WAKATI ZA KAMPENI ZA 2005 BADALA YA KUIFANYA KAULI-MBIU MUHIMU ILIYOWAZUGA WATANZANIA NA KUTOA USHINDI MKUBWA KWA CCM.

NI MUHIMU KWA WAPIGA KURA KUTAMBUA KUWA WANASIASA WETU WANAWEZA KUAHIDI LOLOTE ILI WAPATE KURA KAMA ILIVYOSANIFISHWA KWENYE WIMBO WA "NDIO MZEE" WA PROFESA JAY.

TUSIREJEE MAKOSA YA 2005,PLEEEEZ!

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.