19 Jul 2010

Foleni za magari ni maisha bora-JK
Monday, 19 July 2010 05:33
*Asema watakakamatwa kwa rushwa CCM haitawatetea

Na Peter Mwenda

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Kikwete ametamba kuwa chama hicho kwa miaka mitano iliyopita kimeinua maisha ya Watanzania akitoa mfano wa Jiji la Dar es Salaam kuwa foleni za magari zinatokana na wananchi kuwa na maisha bora.

Alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza katika mkutano ulioandaliwa na CCM Mkoa wa Dar es Salaam kwa ajili ya kumpongeza Rais Kikwete kuchaguliwa kuwa mgombea pekee wa urais kwa asilimia 99.16, Dkt. Ali Mohammed Shein kuchaguliwa kuwa mgombea wa Urais Zanzibar na Dkt. Mohamed Gharib Bilal kuteuliwa kuwa Makamu wa Rais.

"Hapa Dar es Salaam taabu ya msongamano wa magari inaonesha hali ya maisha ni bora, sasa tunahangaika jinsi ya kuondoa msongamano, kuanzia mwakani tutaanza kujenga barabara za juu," alisema Rais Kikwete.

CHANZO: Majira

Hivi kumbe maendeleo yanapimwa kwa msongamano na foleni za magari!Vipi kama foleni hizo ni matokeo ya mindombinu isiyoendana na mahitaji?Vipi kama wingi wa magari hayo ni matokeo ya ufisadi-aidha ya wizi na ubadhirifu wa mali ya umma na ukiukwaji wa taratibu mbalimbali eg ukwepaji kodi stahili bandarini na TRA?

Na je,foleni hizo za magari zinaendana vipi na idadi ya Watanzania wanaumudu mlo wao kila siku?Je wingi wa magari unaendana na idadi ya wamiliki wa magari?Nauliza hivyo kwa sababu wengi tunafahamu kuwa wakati kuna wachache wenye msururuwa magari na majumba ya kifahari kuna wengine wengi tu ambao hata fedha ya kununulia baiskeli hawana,achilia mbali uhakika wa nauli ya daladala.

Na je inawezekana Rais hajafahamishwa na wasaidizi wake kuhusu ongezeko la 'TZ ELEVEN' i.e. watembea kwa miguu ambao hawafanyi hivyo kama sehemu ya mazoezi ya viungo mbali ukosefu wa nauli?Au hawajamwambia kuhusu idadi ya 'mikweche' ambayo licha ya kusababisha foleni inachangia uwezekano wa ajali?Na inawezekana pia wasaidizi wake hawajamfahamisha kuwa mingi ya 'mikweche' hiyo iko barabarani baada ya wamiliki kutoa 'kitu kidogo' kwa askari wa usalama barabarani?

KAMWE MAJIBU RAHISI KWENYE MASWALI MAGUMU HAYAWEZI KULETA UFUMBUZI WA MATATIZO YETU!SINTOSHANGAA TUKISKIA HATA KUONGEZEKA KWA WENYE VITAMBI (INCLUDING WALE WENYE VITAMBI VYA KWASHAKOO) NAKO NI DALILI YA MAISHA BORA!

1 comment:

  1. Kweli inasikitisha kama raisi anaweza akasimama mbele za watu na kutamka kwamba yeye anayaona maendeleo kupitia foleni kuongezeka,watanzania tunahitaji kuwa makini sana na watu tunaowachagua kutuongoza.Shame upon him!!!!!!!!!!

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.